< 욥기 22 >
Ndipo Elifazi Mtemani akajibu:
2 사람이 어찌 하나님께 유익하게 하겠느냐 지혜로운 자도 스스로 유익할 따름이니라
“Je, mwanadamu aweza kuwa wa faida kwa Mungu? Je, hata mtu mwenye hekima aweza kumfaidi?
3 네가 의로운들 전능자에게 무슨 기쁨이 있겠으며 네 행위가 온전한들 그에게 무슨 이익이 있겠느냐
Je, Mwenyezi angefurahia nini kama ungekuwa mwadilifu? Au je, yeye angepata faida gani kama njia zako zingekuwa kamilifu?
4 하나님이 너를 책망하시며 너를 심문하심이 너의 경외함을 인함 이냐
“Je, ni kwa ajili ya utaua wako ndiyo maana anakukemea na kuleta mashtaka dhidi yako?
5 네 악이 크지 아니하냐 네 죄악이 극하니라
Je, uovu wako si mkuu? Dhambi zako si hazina mwisho?
6 까닭없이 형제의 물건을 볼모 잡으며 헐벗은 자의 의복을 벗기며
Umedai dhamana kwa ndugu zako bila sababu; umewavua watu nguo zao, ukawaacha uchi.
7 갈한 자에게 물을 마시우지 아니하며 주린 자에게 식물을 주지 아니하였구나
Hukumpa maji aliyechoka, nawe ulimnyima chakula mwenye njaa,
8 권세있는 자가 토지를 얻고 존귀한 자가 거기서 사는구나
ingawa ulikuwa mtu mwenye uwezo ukimiliki nchi: mtu uliyeheshimiwa, ukiishi ndani yake.
9 네가 과부를 공수로 돌아가게 하며 고아의 팔을 꺾는구나
Umewafukuza wajane mikono mitupu na kuzivunja nguvu za yatima.
10 이러므로 올무들이 너를 둘러있고 두려움이 홀연히 너를 침범하며
Ndiyo sababu mitego imekuzunguka pande zote, hatari ya ghafula inakutia hofu,
11 어두움이 너로 보지 못하게 하고 창수가 너를 덮느니라
ndiyo sababu ni giza sana huwezi kuona, tena ndiyo sababu mafuriko ya maji yamekufunika.
12 하나님이 높은 하늘에 계시지 아니하냐 보라 별의 높음이 얼마나 높은가
“Je, Mungu hayuko katika mbingu za juu? Juu kuliko nyota zilizo juu sana!
13 그러나 네 말은 하나님이 무엇을 아시며 흑암 중에서 어찌 심판 하실 수 있으랴
Hivyo wewe wasema, ‘Mungu anajua nini?’ Je, yeye huhukumu katika giza kama hilo?
14 빽빽한 구름이 그를 가리운즉 그가 보지 못하시고 궁창으로 걸어다니실 뿐이라 하는구나
Mawingu mazito ni pazia lake, hivyo hatuoni sisi atembeapo juu ya anga la dunia.
Je, utaifuata njia ya zamani, ambayo watu waovu waliikanyaga?
16 그들은 때가 이르기 전에 끊어버리웠고 그 터는 하수로 인하여 함몰되었느니라
Waliondolewa kabla ya wakati wao, misingi yao ikachukuliwa na mafuriko.
17 그들이 하나님께 말하기를 우리를 떠나소서 하며 또 말하기를 전능자가 우리를 위하여 무엇을 하실 수 있으랴 하였으나
Walimwambia Mungu, ‘Tuache sisi! Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini?’
18 하나님이 좋은 것으로 그 집에 채우셨느니라 악인의 계획은 나와 판이하니라
Lakini ndiye alizijaza nyumba zao na vitu vizuri, hivyo ninajitenga mbali na mashauri ya waovu.
19 의인은 보고 기뻐하고 무죄자는 그들을 비웃기를
“Wenye haki wanaona maangamizi yao na kufurahi, nao wasio na hatia huwadhihaki, wakisema,
20 우리의 대적이 끊어졌고 그 남은 것이 불사른 바 되었다 하느니라
‘Hakika adui zetu wameangamizwa, nao moto umeteketeza mali zao.’
21 너는 하나님과 화목하고 평안하라 그리하면 복이 네게 임하리라
“Mjue sana Mungu ili uwe na amani, ndipo mema yatakapokujia.
22 청컨대 너는 그 입에서 교훈을 받고 그 말씀을 네 마음에 두라
Uyapokee mafundisho toka kinywani mwake, na maneno yake uyaweke moyoni mwako.
23 네가 만일 전능자에게로 돌아가고 또 네 장막에서 불의를 멀리 버리면 다시 흥하리라
Kama ukimrudia Mwenyezi, utarudishwa upya: Kama ukiuondoa uovu uwe mbali na hema lako,
24 네 보배를 진토에 버리고 오빌의 금을 강 가의 돌에 버리라
kama dhahabu yako ukiihesabu kama mavumbi, dhahabu yako ya Ofiri kama miamba ya mabondeni,
25 그리하면 전능자가 네 보배가 되시며 네게 귀한 은이 되시리니
ndipo Mwenyezi atakuwa dhahabu yako, naye atakuwa fedha yako iliyo bora.
26 이에 네가 전능자를 기뻐하여 하나님께로 얼굴을 들 것이라
Hakika ndipo utakapojifurahisha kwa Mwenyezi, nawe utamwinulia Mungu uso wako.
27 너는 그에게 기도하겠고 그는 들으실 것이며 너의 서원한 것을 네가 갚으리라
Utamwomba yeye, naye atakusikia, nawe utazitimiza nadhiri zako.
28 네가 무엇을 경영하면 이루어질 것이요 네 길에 빛이 비취리라
Utakusudia jambo nalo litatendeka, nao mwanga utaangazia njia zako.
29 네가 낮춤을 받거든 높아지리라고 말하라 하나님은 겸손한 자를 구원하시느니라
Watu watakaposhushwa, nawe ukasema, ‘Wainue!’ ndipo atamwokoa aliyevunjika moyo.
30 무죄한 자가 아니라도 건지시리니 네 손이 깨끗함을 인하여 그런자가 건지심을 입으리라
Atamwokoa hata yule ambaye ana hatia, ataokolewa kwa sababu ya usafi wa mikono yako.”