< Ufunuo 12 >
1 Ishara mbaha jhabhonekene kumbinguni: N'dala jha afwekibhu ni lijobha, na ajhele ni muesi pasi pa magolo gha muene; ni taji jha matondo kumi ni mabhele jhajhele panani pa mutu ghwa muene.
Kukaonekana ishara kuu mbinguni: Palikuwa na mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ukiwa chini ya miguu yake, na taji ya nyota kumi na mbili ilikuwa kichwani mwake.
2 Ajhele ni luleme na aleleghe kwa ndabha jha maumivu gha kuhogola- mu uchungu bhwa kwifungula.
Alikuwa na mimba naye akilia kwa uchungu kwa kuwa alikuwa anakaribia kuzaa.
3 Ni ishara jhenge jhabhonekene kumbinguni: Langayi! kwajhele ni liyoka lidung'u libhaha ambalo lyajhele ni mutu saba ni mang'eru kumi, na kwajhele ni taji saba mu mitu ghiake.
Kisha ishara nyingine ikaonekana mbinguni: Likaonekana joka kubwa jekundu lenye vichwa saba na pembe kumi na taji saba katika vichwa vyake.
4 N'kela ghuake ghwakokuili theluthi jhimonga jha matondo kumbinguni ni kusitagha pasi pa dunia. Lijhoka lyajhemili palongolo pa n'dala jhaakaribireghe kuhogola, ili kwamba wakati ihogola, abhwesiajhi kumila muana ghwa muene.
Mkia wake ukakokota theluthi ya nyota zote angani na kuziangusha katika nchi. Ndipo lile joka likasimama mbele ya yule mwanamke aliyekuwa karibu kuzaa ili lipate kumla huyo mtoto mara tu atakapozaliwa.
5 An'hoguili muana, muana n'gosi, ambajhe ibeta kughatawala mataifa ghoha kwa ndonga jha chuma. Mwana munu anyakulibhu kunani kwa K'yara ni mu kiti kya enzi,
Yule mwanamke akazaa mtoto mwanaume, atakayeyatawala mataifa yote kwa fimbo yake ya utawala ya chuma. Lakini huyo mtoto akanyakuliwa na kupelekwa kwa Mungu kwenye kiti chake cha enzi.
6 ni n'dala ajumbili munyika, mahali ambapo K'yara aandele lieneo kwa ndabha jha muene, ili abhwesiajhi kuhudumibhwa kwa magono 1, 260.
Yule mwanamke akakimbilia jangwani, ambako Mungu alikuwa amemtayarishia mahali ili apate kutunzwa huko kwa muda wa siku 1,260.
7 Henu kwajhele ni vita kumbinguni. Mikaeli ni malaika bha muene bhakakomana ni lela lijhoka; Niliene lijhoka libhaha ni malaika bha muene bhakomene nabhu.
Basi palikuwa na vita mbinguni: Mikaeli na malaika zake wakapigana na hilo joka, nalo joka pamoja na malaika zake likapigana nao.
8 Lakini lijhoka lyajhelepi ni nghofu sya kutosha kushinda. Henu jhajhelepi kabhele nafasi kumbinguni kwa ndabha jha muene ni malaika bha muene.
Lakini joka na malaika zake wakashindwa, na hapakuwa tena na nafasi yao huko mbinguni.
9 Lijhoka libhaha - lela lijhoka lya muandi lyalikutibhweghe ibilisi au shetani ambajhe likofya - dunia jhioha ataghibhu pasi pa dunia ni malaika bha muene bhataghibhu pasi pamonga ni muene.
Lile joka kuu likatupwa chini, yule nyoka wa zamani aitwaye ibilisi au Shetani, aupotoshaye ulimwengu wote. Akatupwa chini duniani, yeye pamoja na malaika zake.
10 Kisha napeliki sauti mbaha kuhoma kumbinguni: “Henu wokovu uhidili, nghofu - ni ufalme bhwa K'yara ghwitu, ni mamlaka jha Kristu ghwake kwa kujha mshitaki ghwa bhalongo bhitu bhataghibhu pasi- ambajhe abhatakili mbele sya K'yara ghwitu pamusi ni pakiru.
Kisha nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema: “Sasa wokovu na uweza na Ufalme wa Mungu wetu umekuja na mamlaka ya Kristo wake. Kwa kuwa ametupwa chini mshtaki wa ndugu zetu, anayewashtaki mbele za Mungu usiku na mchana.
11 Bhan'shindili kwa damu jha mwanakondoo ni kwa lilobhi lya ushuhuda ghwa bhene, kwa ndabha bhalondeghe lepi sana maisha gha bhene, hata kufwa.
Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo na kwa neno la ushuhuda wao. Wala wao hawakuyapenda maisha yao hata kufa.
12 Kwa hiyo, muhobhokayi, muenga mbingu, na bhoha bhamwitama mugati mwake. Lakini ole bha nchi ni bahari kwa ndabha mwovu asilili kwa muenga. Amemili ni ligoga likali, kwa ndabha amanyili kujha ajhe ni muda udebe to.
Kwa hiyo, furahini ninyi mbingu na wote wakaao humo! Lakini ole wenu nchi na bahari, kwa maana huyo ibilisi ameshuka kwenu, akiwa amejaa ghadhabu, kwa sababu anajua ya kuwa muda wake ni mfupi!”
13 Wakati lijhoka limanyili kujha litaghibhu pasi pa nchi an'kesili n'dala ambajhe ahoguili muana n'gosi.
Lile joka lilipoona kuwa limetupwa chini duniani, lilimfuatilia yule mwanamke aliyekuwa amezaa mtoto mwanaume.
14 Lakini n'dala apelibhu mababatilu mabhele gha tai mbaha, ili abhwesiajhi kuruka hadi mu lieneo lya lyaandalibhu kwandabha jha muene k'ola ku jangwa lieneo ambalyo agalibhwesi kutunzibhwa kwa kwa wakati nyakati ni nusu wakati - mahali paabhwesilepi kupafikila lijhoka e'lu.
Lakini huyo mwanamke akapewa mabawa mawili ya tai mkubwa, kusudi aweze kuruka mpaka mahali palipotayarishwa kwa ajili yake huko jangwani, ambako atatunzwa kwa wakati na nyakati na nusu, ya wakati ambako yule joka hawezi kufika.
15 Lijhoka lyajhitisi masi kuhoma mu ndomo mwa muene kama kiholo ili akhetai gharika jha kun'gharikisha.
Ndipo lile joka likamwaga maji kama mto kutoka kinywani mwake, ili kumfikia huyo mwanamke na kumkumba kama mafuriko.
16 Lakini ardhi jhan'tangatili n'dala. Jhafunuili kinywa kya muene ni kuumila kiholo kyalyafunyili lijhoka kuhoma mu kinywa kya muene.
Lakini nchi ikamsaidia huyo mwanamke kwa kufungua kinywa na kuumeza huo mto ambao huyo joka alikuwa ameutoa kinywani mwake.
17 Kisha lijhoka likan'dadila n'dala ni muene akabhoka ni kukheta vita ni uzao bhwa muene bhuoha- bhala bhabhitii amri sya K'yara ni kukamulela ushuhuda kuhusu Yesu.
Kisha lile joka likapatwa na hasira kali kwa ajili ya huyo mwanamke na likaondoka ili kupigana vita na watoto waliosalia wa huyo mwanamke, yaani, wale wanaozitii amri za Mungu na kuushika ushuhuda wa Yesu Kristo.