< 1 Wathesalonike 5 >

1 Henu, kwa habari sya muda ni nyakati, ndhongo, iyelepi haja Kujo kenu kihoakela kiyandikibhwa kwa yhomo.
Sasa, kwa habari ya muda na nyakati, ndugu, hamna haja kwamba kitu chochote kiandikwe kwenu.
2 kwa ndabha ya muenga mwayhomo mmanyili kiusahihi kujo magono gha Bwana ghihida kama mm'eji paihida pakilu.
Kwa kuwa ninyi wenyewe mwajua kwa usahihi ya kuwa siku ya Bwana inakuja kama mwizi ajapo usiku.
3 pala pabhijoba kuye” Amani ni usalama”, ndo pauhalibifu pawihida ghafula. Ndo kawawa ukamkabha mabhu mwenye luleme. bhabhiye puka hee kwa njela yioayela.
Pale wasemapo kuna “Amani na usalama”, ndipo uharibifu huwajia ghafla. Ni kama utungu umjiavyo mama mwenye mimba. Hawataepuka kwa njia yeyote.
4 Lakini muenga, ndhongo muyelepi mukitita hata ligono elu libhahidilai Kama mm'eji.
Lakini ninyi, ndugu hampo kwenye giza hata ile siku iwajie kama mwizi.
5 Kwa ndabha muenga mwabhoa ni Bhana bha nuru ni bhana bha pamusi. Tete sio bhana bhapakilu au bhamkitita.
Kwa maana ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi siyo wana wa usiku au wa gizani.
6 Elu basu, tusigoni Kama bhamana kabhigona. Bali tukeshai ni kuya makini.
Hivyo basi, tusilale kama wengine walalavyo. Bali tukeshe na kuwa makini.
7 Kwa ndabha by bhabhigona bhigona pakilu na bhabigala bhigala pakilu.
Kwa kuwa wanaolala hulala usiku na wanao lewa hulewa usiku.
8 Kwa ndabha tete Ndo bhana bhapamusi, tuyelai makini. Tufwalai ngao ya imani ni upendo, na, kofia ya lichuma, ambayo ndo bhwokovu wa magono ghaghihida.
Kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, tuwe makini. Tuvae ngao ya imani na upendo, na, kofia ya chuma, ambayo ni uhakika wa wokovu wa wakati ujao.
9 Kwa ndabha kyala atuchaguililepi muandi kwajia ya gadhabu, bali kwakutupela bhuokovu kwa njela ya Bwana Yesu Kristu.
Kwa kuwa Mungu hakutuchagua mwanzo kwa ajili ya gadhabu, bali kwa kupata wokovu kwa njia ya Bwana Yesu Kristo.
10 Muene ndo atufwelili ili kwa ndabha, tukayelai mihu au tugonili, tulaishi pamonga ni muene.
Yeye ndiye aliyetufia ili kwamba, tukiwa macho au tumelala, tutaishi pamoja naye.
11 Kwa hiyo, mjifalijiayi ni kujibhomba yhomo kwa yhomo, kama ambafyo kammalili kuketa.
Kwa hiyo, farijianeni na kujengana ninyi kwa ninyi, kama ambavyo tayari mnafanya.
12 Ndhongo, tukabhasoma mbhatambulai bhala bhahitumika miongoni mwa yhomo ni bhala bhabha yelae panani pa muenga kup'etela Bwana na bhabhi shauri bhala.
Ndugu, twawaomba muwatambue wale wanaotumika miongoni mwenu na wale walio juu yenu katika Bwana na wale wanao washauri.
13 Tukabhasoma kabhele mbhatambulai ni kubhapela heshima kwa upendo ndabha ya mbhombho yabhi. Muyela ni amani miongoni mwa yhomo.
Tunawaomba pia muwatambue na kuwapa heshima katika upendo kwa sababu ya kazi yao. Muwe na amani miongoni mwenu ninyi wenyewe.
14 Tukabhasii, ndhongo: mubhaonyai bhabhilotalepi molimoli, mbhapelai miteema yabhakatili tamaa, mbhasaidilai bhabhayele bhayonge, muyelai mm'bhavumilivu kwa bhoa.
Twawasihi, ndugu: muwaonye wasio kwenda kwa utaratibu, watieni moyo walio kata tamaa, Wasaidieni walio wanyonge, na muwe wavumilivu kwa wote.
15 Mulangai akotokuya munu yuoayola yailepa libaya kwa libaya kwa munu yuoayola. Badala yake, mfwanyai ghaghayele ni mema kwakila mmonga bhinu ni bhanu bhoa.
Angalieni asiwepo mtu yeyote anayelipa baya kwa baya kwa mtu yeyote. Badala yake, fanyeni yaliyo mema kwa kila mmoja wenu na kwa watu wote.
16 Muhobholelai magono ghoa.
Furahini siku zote.
17 Musomai bila kukoma.
Ombeni bila kukoma.
18 Munshukulai kyala kwa lijambo, kwandabha agha ghoa ndo mapenzi gha kyala kwayhomo kup'etela Yesu Kristu.
Mshukuruni Mungu kwa kila jambo, kwa sababu hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kwenu katika Yesu Kristo.
19 Msiuyemeki Roho.
Msimzimishe Roho.
20 Msiudhalau bhunabii.
Msiudharau unabii.
21 Mghajalibuayi mambo ghoa. Mlikamulai laliyele liyema.
Yajaribuni mambo yote. Mlishike lililo jema.
22 Mjiyepusiayi kwa lalibhonekana kiuovu.
Epukeni kila mwonekano wa uovu.
23 kyala wa amani abhakamilisiayi kup'etela utakatifu. Roho, nafsi ni mbhele vifunzibhwai papayehe ni mawaa kwa kuhida Bwana wayhoto Yesu Kristu.
Mungu wa amani awakamilishe katika utakatifu. Roho, nafsi na mwili vitunzwe pasipo mawaa katika kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24 Muene ya abhakutili ndo muaminifu, muene ndo wakuliketa.
Yeye aliyewaita ni mwaminifu, naye ndiye mwenye kutenda.
25 Ndhongo, mtusomelai kabhele.
Ndugu, tuombeeni pia.
26 Mbhasalimilai bhalongo bhoa kwa libusu lakitakatifu.
Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
27 Nikabhasii kup'etela Bwana kuwa barua eye isomebhua you kwa bhalongo bhangu bhoa.
Nawasihi katika Bwana kwamba barua hii isomwe kwa ndugu wote.
28 Neema ya Bwana Yesu Kristu iyelai pamonga ni muenga.
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi.

< 1 Wathesalonike 5 >