< 1 Yohana 5 >

1 J'hoj'hioha j'he ikiera kuj'ha Yesu ndo Kristu ahogoliki ni K'yara. Na j'hoj'hioha j'haan'ganili muene ambaj'he ahomili kwa tata pia akabhagana bhana munu.
Kila mtu anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo amezaliwa na Mungu, na yeyote ampendaye Baba humpenda pia mtoto aliyezaliwa naye.
2 Kwa e'le tumanyili kuj'ha tubhaganili bhana bha K'yara— patukan'gana K'yara ni kutekelasya amri syake.
Hivi ndivyo tunavyojua kwamba tunawapenda watoto wa Mungu, kwa kumpenda Mungu na kuzitii amri zake.
3 Naha ndo kyatukan'gana K'yara kwa kusikamula Amri syake mbepe.
Huku ndiko kumpenda Mungu, yaani, kuzitii amri zake. Nazo amri zake si nzito.
4 kwa kuj'ha kila j'ha ahogoliki nu K'yara akabhushinda bhulimwengu. Na obho ndo bhushindi bhwa kubhushinda bhulimwengu, imani j'hitu.
Kwa maana kila aliyezaliwa na Mungu huushinda ulimwengu. Huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, yaani, hiyo imani yetu.
5 Niani j'ha abhushindi bhulimwengu? Ndo j'hola j'ha ij'hamini kuj'ha Yesu ndo muana ghwa K'yara.
Ni nani yule aushindaye ulimwengu? Ni yule tu aaminiye kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.
6 O'j'ho ndo j'haahadili kwa masi ni muasi- Yesu Kristu. Ahidili lepi kwa masi tu bali kwa masi ni muasi.
Huyu ndiye alikuja kwa maji na damu, yaani, Yesu Kristo. Hakuja kwa maji peke yake, bali kwa maji na damu. Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli.
7 Kwa kuj'ha bhaj'he bhadatu bhabhashuhudili.
Kwa maana wako watatu washuhudiao[ mbinguni: hao ni Baba, Neno na Roho Mtakatifu. Hawa watatu ni umoja.
8 Roho, masi ni muasi. Abha bhadatu bhikakubaliana. (Zingatilai: Malobhi agha “Tata, Lilobhi, ni Roho Mtakatifu” ghibhonekana lepi mu nakala sinofu sya muandi).
Pia wako mashahidi watatu duniani]: Roho, Maji na Damu; hawa watatu wanakubaliana katika umoja.
9 Kama twikabhaj'ham'belela bhushuhuda bhwa bhanadamu bhushuhuda bhwa K'yara ndo mmbaha kuliko obho- kwa kujha aj'he nabhu bhushuhuda kuhusiana nu mwanabhe.
Kama tunaukubali ushuhuda wa wanadamu, basi ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi, kwa kuwa huu ndio ushuhuda wa Mungu kwamba amemshuhudia Mwanawe.
10 Muene j'haikamwamini mwana ghwa K'yara aj'he ni bhushuhuda mugati mwake muene. Na j'hej'hioha j'haabelili kumwamini K'yara am'bombali kuj'ha n'desi, kwa kuj'ha abhwaminilepi bhushuhuda ambabho K'yara abhulatili kup'hetela mwanabhe.
Kila mtu amwaminiye Mwana wa Mungu anao huu ushuhuda moyoni mwake. Kila mtu asiyemwamini Mungu amemfanya yeye kuwa mwongo, kwa sababu hakuamini ushuhuda Mungu alioutoa kuhusu Mwanawe.
11 Ni bhushuhuda ndo obho— kuj'ha K'yara atupele bhusima bhwa milele, ni bhusima obho bhuj'hele mugati mwa Mwanabhe. (aiōnios g166)
Huu ndio ushuhuda: kwamba Mungu ametupa uzima wa milele, nao huo uzima umo katika Mwanawe. (aiōnios g166)
12 J'ha aj'he nu mwanabhe aj'he ni bhusima. Na g'haabeli kuj'ha nu mwanabhe aj'helepi ni bhusima.
Aliye naye Mwana wa Mungu anao uzima, yeye asiye na Mwana wa Mungu hana uzima.
13 Nibhalembili agha ili mbwesiagha kumanya kuj'ha muj'henabhu bhusima bhwa milele— Muenga j'ha mwikuera mu lihina lya mwana ghwa K'yara. (aiōnios g166)
Nawaandikia mambo haya ninyi mnaoliamini Jina la Mwana wa Mungu ili mpate kujua ya kuwa mnao uzima wa milele. (aiōnios g166)
14 Na obho ndo bhujasiri bhwa tujhe nabhu pa mihu pa muene, kuj'ha Kama tus'okuli k'henu kyokyoha k'hela sawasawa ni mapenzi ghake, akatup'heleka.
Huu ndio ujasiri tulio nao tunapomkaribia Mungu, kwamba kama tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia.
15 Na Kama tumenye kuj'ha akatup'heleka— kyokyoha kyatukans'oma, tumanyili kuj'ha tuj'he naku kyatuns'omili.
Nasi kama tunajua atusikia, lolote tuombalo, tunajua ya kwamba tumekwisha kupata zile haja tulizomwomba.
16 Kama twikabhaj'ham'belela bhushuhuda bhwa bhanadamu bhushuhuda bhwa K'yara ndo mmbaha kuliko obho- kwa kujha aj'he nabhu bhushuhuda kuhusiana nu mwanabhe. Muene j'haikamwamini mwana ghwa K'yara aj'he ni bhushuhuda mugati mwake muene. Na j'hej'hioha j'haabelili kumwamini K'yara am'bombali kuj'ha n'desi, kwa kuj'ha abhwaminilepi bhushuhuda ambabho K'yara abhulatili kup'hetela mwanabhe.
Kama mtu akimwona ndugu yake akitenda dhambi isiyo ya mauti, inampasa aombe, naye Mungu atampa uzima mtu huyo. Ninamaanisha wale ambao dhambi yao si ya mauti. Iko dhambi ya mauti, sisemi kwamba utaomba kwa ajili ya hiyo.
Jambo lolote lisilo la haki ni dhambi, lakini iko dhambi isiyo ya mauti.
18 Tumanyili j'ha kuj'ha j'haahogoliki nu K'yara ibhomba lepi sambi. Bali j'haahogoliki nu K'yara itunzibhwa nu muene salama daima, ni j'hola mwovu ibhwesyalepi kumdhuru.
Tunajua ya kuwa yeye aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, bali aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hawezi kumdhuru.
19 Tumanyili kuj'ha tete ni bha K'yara na tumanyili kuj'ha bhulimwengu bhuoha bhuj'hele pasi pa bhutawala bhwa j'hola mwovu.
Sisi twajua kuwa tu watoto wa Mungu na ya kwamba ulimwengu wote uko chini ya utawala wa yule mwovu.
20 Lakini tumanyili kuj'ha mwana ghwa K'yara ahidili na atupelili bhujuzi, kuj'ha tummanyili muene j'haaj'hele ghwa bhukweli na kwamba tujhele mugati mwa muene j'haaj'hele ghwa bhukweli, hata kwa mwanabhe Yesu Kristu. Ni K'yara ghwa bhukweli ni bhusima bhwa milele. (aiōnios g166)
Nasi pia twajua ya kwamba Mwana wa Mungu amekuja, naye ametupa sisi ufahamu ili tupate kumjua yeye aliye Kweli. Nasi tumo ndani yake yeye aliye Kweli, yaani, ndani ya Yesu Kristo Mwanawe. Yeye ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele. (aiōnios g166)
21 Bhana bhapenzi, mkij'hepusiaghe ni lisanamu.
Watoto wapendwa, jilindeni nafsi zenu kutokana na sanamu. Amen.

< 1 Yohana 5 >