< 2 Kroniku 22 >

1 Hanki Jerusalemi kumate'ma nemani'za vahe'mo'za Jehoramuna amite'na mofavre'a Ahasiana kinia azeri otizageno, nefa Jehoramu nona erino kinia mani'ne. Na'ankure Arabia vahe'mo'za ha'ma eme huzmante'za maka Ahasi afuhe'ina zamahe vagare'naze. E'ina higeno Jehoramu nemofo Ahasi'a Juda vahe kini manino kegava huzmante'ne.
Watu wa Yerusalemu wakamfanya Ahazia, mdogo wa wote wa wana wa Yerohamu, kuwa mfalme mahali pa baba yake, kwa sababu washambuliaji wa ghafula waliokuwa wameingia kambini pamoja na Waarabu, walikuwa wamewaua wana wakubwa wote wa Yehoramu. Kwa hiyo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
2 Hagi Ahasia'a 22tu'a kafu hu'neno kinia efore hu'neankino, magoke kafu Jerusalemi kumatera kinia mani'ne. Hagi nerera agi'a Ataliakino negeho'a Israeli kini ne' Omri'e.
Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri.
3 Hagi Ahapu nagamo'ma hu'naza avu'ava Ahasia'a avariri'ne. Na'ankure nerera'a antahintahi amigeno kefo avu'ava hu'ne.
Ahazia naye akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, kwa sababu mama yake alimshawishi katika kutenda maovu.
4 Ahasia'a Ahapu naga'mo'zama hu'nazaza huno Ra Anumzamofo avufina kefo avu'ava hu'ne. Na'ankure Ahasia'a nefa'ma fritegeno'a Ahapu nagapinti vahetmimo'za antahintahia ami'zageno havi avu'avara hu'ne.
Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana kama walivyokuwa wamefanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa baada ya kufa kwa baba yake nyumba ya Ahabu ndio waliokuwa washauri wake, kwa uangamivu wake.
5 Ahasia'a ana vahe'mokizmi ke antahino Israeli kini ne' Ahapu nemofo Jehoramu avaririno Siria vahe kini ne' Hazaeli ha' ome hunte'naku Ramot-Gileati kumate vigeno, ana hapi Siria vahe'mo'za Joramuna ahe kuzafa antazageno,
Pia akafuata shauri lao alipokwenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu.
6 ete rukrahe huno eno namuma'ama teganinogura Jezrili kumate emani'ne. Hagi Juda kini ne' Jehoramu nemofo Ahasia'a Ahapu nemofo Joramu kenaku Jezrili kumate urami'ne. Na'ankure Joramuna hapinti ahe kuzafa antazageno umase'negeno'e.
Hivyo akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa huko Ramothi alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu. Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.
7 Hianagi Anumzamo'a Ahasiana azeri haviza hunaku higeno, Joramuna ome kenakura vu'ne. Na'ankure anante'ma nevuno'a Jehoramu'ene vuno Ra Anumzamo'ma Ahapu nagama zamahe hana hinogu'ma Nimsi nemofo Jehu'ma masavema frente'nea ne' ome ke'naku vu'na'e.
Mungu alikuwa ameamuru kwamba kuanguka kwa Ahazia kungetokea atakapokwenda kumwona Yoramu. Ahazia alipowasili, wakatoka pamoja na Yoramu ili kwenda kukutana na Yehu mwana wa Nimshi, ambaye Bwana alikuwa amemtia mafuta kuangamiza nyumba ya Ahabu.
8 Hagi Jehu'ma Ahapu naga'ma zamazeri havizama nehireti'ma Juda kva vahetamine, Ahasia afuhe'ima ome tutagiha'ma hunezmanteno'a, ana maka zamahe fri'ne.
Yehu alipokuwa anatekeleza hukumu juu ya nyumba ya Ahabu, akawakuta wakuu wa Yuda na wana wa jamaa ya Ahazia waliokuwa wanamhudumia Ahazia, naye akawaua.
9 Ana nehuno Ahasianku nehakege'za, mago'a vahe'mo'za Sameria kumateti Ahasia'a frakinege'za ome ke'za avre'za Jehuna eme amizageno, ahe fri'ne. Ana hige'za Ahasiana kerifi asente'naze. Na'ankure negeho Jehosafati'a agu'areti huno Ra Anumzamofona amagera ante'ne. Ana hazageno Ahasia nagapina hanavetino mani'neno Ahasia noma erino kinima maniga vahera omani'ne.
Ndipo akaenda kumsaka Ahazia, nao watu wake wakamkamata alipokuwa amejificha huko Samaria. Akaletwa kwa Yehu, naye Yehu akamuua. Wakamzika kwani walisema, “Alikuwa mwana wa Yehoshafati, ambaye alimtafuta Bwana kwa moyo wake wote.” Hivyo hapakuwa na mtu mwenye uwezo katika nyumba ya Ahazia aliyeweza kushika ufalme.
10 Hagi Atalia'ama antahiama nemofo Ahasia'ma fria nanekema nentahino'a, maka Juda nagapinti'ma kinima maniga vahetamina zamahe hana hu'ne.
Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme ya nyumba ya Yuda.
11 Hagi Ahasia nemofo Joasina ahenaku neageno, kini ne'mofo mofa Jehosabeti'a ana mofavrea oku'a avreno nemasefinka ome frakino ante'negeno mago a'mo kegava hu'ne. Hagi Jehosabeti'a kini ne' Jehoramu mofakino pristi ne' Jehoaida nenaro'e. Hagi Jehosabeti'a Ahasiana nesarokino Atalia'ma Joasima ahe fri'zanku avreno ome frakinte'negeno Atali'a ana mofavrea ahe ofrine.
Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala. Kwa kuwa Yehosheba, aliyekuwa binti wa Mfalme Yehoramu, na pia alikuwa mke wa kuhani Yehoyada, alikuwa dada yake Ahazia, akamficha huyo mtoto ili Athalia asimuue.
12 Hagi Atalia'ma Juda mopama kegavama hu'negeno'a, 6si'a kafufi Ra Anumzamofo mono nompi Joasina avre frakine'za kegava hazageno mani'ne.
Alibaki amefichwa pamoja nao katika Hekalu la Mungu kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.

< 2 Kroniku 22 >