< 詩篇 34 >
1 ダビデ、アビメレクのまへにて狂へる状をなし逐れていでさりしときに作れるうた われつねにヱホバを祝ひまつらんその頌詞はわが口にたえじ
Nitamsifu Yahwe wakati wote, siku zote sifa zake zitakuwa mdomoni mwangu.
2 わがたましひはヱホバによりて誇らん 謙だるものは之をききてよろこばん
Nitamsifu Yahwe! walio onewa wasikie na kufurahi.
3 われとともにヱホバを崇めよ われらともにその名をあげたたへん
Msifuni Yahwe pamoja nami, kwa pamoja tuliinue jina lake.
4 われヱホバを尋ねたればヱホバわれにこたへ我をもろもろの畏懼よりたすけいだしたまへり
Nilimuomba Yahwe msaada naye akanijibu, akanipa ushindi juu ya hofu yangu yote.
5 かれらヱホバを仰ぎのぞみて光をかうぶれり かれらの面ははぢあからむことなし
Wale wanao mtazama yeye wana furaha, na nyuso zao hazina aibu.
6 この苦しむもの叫びたればヱホバこれをきき そのすべての患難よりすくひいだしたまへり
Huyu mtu aliye onewa alilia na Yahwe akamsikia na kumuokoa kwenye matatizo yake yote.
7 ヱホバの使者はヱホバをおそるる者のまはりに営をつらねてこれを援く
Malaika wa Yahwe huweka kambi wakiwazunguka wale wanao muogopa yeye na kuwaokoa.
8 なんぢらヱホバの恩恵ふかきを嘗ひしれ ヱホバによりたのむ者はさいはひなり
Onjeni muone Yahwe ni mzuri. Amebarikiwa mtu yule ambaye Yahwe ni kimbilio lake.
9 ヱホバの聖徒よヱホバを畏れよヱホバをおそるるものには乏しきことなければなり
Muogopeni Yahwe, ninyi watu watakatifu wake. Hakuna kupungukikwa kwa wale wanao mhofu yeye.
10 わかき獅はともしくして饑ることあり されどヱホバをたづぬるものは嘉物にかくることあらじ
Simba wadogo wakati mwingine hukosa chakula na kuteseka kwa njaa, bali wale wamtafutao Yahwe hawatapungukiwa chochote kilicho kizuri.
11 子よきたりて我にきけ われヱホバを畏るべきことを汝等にをしへん
Njoni, wana, mnisikilize mimi. nitawafundisha ninyi hofu ya Yahwe.
12 福祉をみんがために生命をしたひ存へんことをこのむ者はたれぞや
Mtu nani aliyepo ambaye anatamani maisha na anapenda kuwa na siku nyingi, ili kwamba aweze kuona vizuri?
13 なんぢの舌をおさへて惡につかしめず なんぢの口唇をおさへて虚偽をいはざらしめよ
Hivyo uepushe ulimi wako na uovu na uilinde midomo yako kuongea uongo.
14 惡をはなれて善をおこなひ和睦をもとめて切にこのことを勉めよ
Uache uovu na utende mema. Uitafute amani na kuiendea amani.
15 ヱホバの目はただしきものをかへりみ その耳はかれらの号呼にかたぶく
Macho ya Yahwe yako kwenye haki na masikio yake huelekea kulia kwao.
16 ヱホバの聖顔はあくをなす者にむかひてその跡を地より断滅したまふ
Uso wa Yahwe uko kinyume na wale watendao uovu, kuikatilia mbali kumbukumbu yao duniani.
17 義者さけびたれぱヱホバ之をききてそのすべての患難よりたすけいだしたまへり
Wenye haki hulia na Yahwe husikia na kuwaokoa kwenye matatizo yao yote.
18 ヱホバは心のいたみかなしめる者にちかく在してたましひの悔頽れたるものをすくひたまふ
Yahwe yu karibu nao waliovunjika moyo, naye huwaokoa waliogandamizwa rohoni.
19 ただしきものは患難おほし されどヱホバはみなその中よりたすけいだしたまふ
Mateso ya wenye haki ni mengi, bali Yahwe huwaokoa nayo yote.
20 ヱホバはかれがすべての骨をまもりたまふ その一つだに折らるることなし
Yeye huitunza mifupa yake yote, hakuna hata mmoja wao utavunjika.
21 惡はあしきものをころさん 義人をにくむものは刑なはるべし
Uovu utawauwa waovu. Wale wachukiao haki watahukumiwa.
22 ヱホバはその僕等のたましひを贖ひたまふ ヱホバに依頼むものは一人だにつみなはるることなからん
Yahwe huokoa maisha ya watumishi wake. Hakuna atakaye hukumiwa hata mmoja atafutaye usalama katika yeye.