< 詩篇 107 >

1 「主に感謝せよ、主は恵みふかく、そのいつくしみはとこしえに絶えることがない」と、
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2 主にあがなわれた者は言え。主は彼らを悩みからあがない、
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3 もろもろの国から、東、西、北、南から彼らを集められた。
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 彼らは人なき荒野にさまよい、住むべき町にいたる道を見いださなかった。
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5 彼らは飢え、またかわき、その魂は彼らのうちに衰えた。
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6 彼らはその悩みのうちに主に呼ばわったので、主は彼らをその悩みから助け出し、
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7 住むべき町に行き着くまで、まっすぐな道に導かれた。
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8 どうか、彼らが主のいつくしみと、人の子らになされたくすしきみわざとのために、主に感謝するように。
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9 主はかわいた魂を満ち足らせ、飢えた魂を良き物で満たされるからである。
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
10 暗黒と深いやみの中にいる者、苦しみと、くろがねに縛られた者、
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11 彼らは神の言葉にそむき、いと高き者の勧めを軽んじたので、
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12 主は重い労働をもって彼らの心を低くされた。彼らはつまずき倒れても、助ける者がなかった。
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13 彼らはその悩みのうちに主に呼ばわったので、主は彼らをその悩みから救い、
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14 暗黒と深いやみから彼らを導き出して、そのかせをこわされた。
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15 どうか、彼らが主のいつくしみと、人の子らになされたくすしきみわざとのために、主に感謝するように。
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
16 主は青銅のとびらをこわし、鉄の貫の木を断ち切られたからである。
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 ある者はその罪に汚れた行いによって病み、その不義のゆえに悩んだ。
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
18 彼らはすべての食物をきらって、死の門に近づいた。
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
19 彼らはその悩みのうちに主に呼ばわったので、主は彼らをその悩みから救い、
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
20 そのみ言葉をつかわして、彼らをいやし、彼らを滅びから助け出された。
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
21 どうか、彼らが主のいつくしみと、人の子らになされたくすしきみわざとのために、主に感謝するように。
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
22 彼らが感謝のいけにえをささげ、喜びの歌をもって、そのみわざを言いあらわすように。
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
23 舟で海にくだり、大海で商売をする者は、
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
24 主のみわざを見、また深い所でそのくすしきみわざを見た。
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
25 主が命じられると暴風が起って、海の波をあげた。
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
26 彼らは天にのぼり、淵にくだり、悩みによってその勇気は溶け去り、
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
27 酔った人のようによろめき、よろめいて途方にくれる。
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
28 彼らはその悩みのうちに主に呼ばわったので、主は彼らをその悩みから救い出された。
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
29 主があらしを静められると、海の波は穏やかになった。
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
30 こうして彼らは波の静まったのを喜び、主は彼らをその望む港へ導かれた。
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
31 どうか、彼らが主のいつくしみと、人の子らになされたくすしきみわざとのために、主に感謝するように。
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
32 彼らが民の集会で主をあがめ、長老の会合で主をほめたたえるように。
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
33 主は川を野に変らせ、泉をかわいた地に変らせ、
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
34 肥えた地をそれに住む者の悪のゆえに塩地に変らせられる。
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
35 主は野を池に変らせ、かわいた地を泉に変らせ、
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36 飢えた者をそこに住まわせられる。こうして彼らはその住むべき町を建て、
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37 畑に種をまき、ぶどう畑を設けて多くの収穫を得た。
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38 主が彼らを祝福されたので彼らは大いにふえ、その家畜の減るのをゆるされなかった。
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
39 彼らがしえたげと、悩みと、悲しみとによって減り、かつ卑しめられたとき、
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40 主はもろもろの君に侮りをそそぎ、道なき荒れ地にさまよわせられた。
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41 しかし主は貧しい者を悩みのうちからあげて、その家族を羊の群れのようにされた。
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
42 正しい者はこれを見て喜び、もろもろの不義はその口を閉じた。
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
43 すべて賢い者はこれらの事に心をよせ、主のいつくしみをさとるようにせよ。
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.

< 詩篇 107 >