< 箴言 知恵の泉 1 >

1 ダビデの子イスラエルの王ソロモンの箴言
Mithali za Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:
2 こは人に智慧と訓誨とをしらしめ哲言を暁らせ
Kwa kupata hekima na nidhamu; kwa kufahamu maneno ya busara;
3 さとき訓と公義と公平と正直とをえしめ
kwa kujipatia nidhamu na busara, kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;
4 拙者にさとりを與へ少者に知識と謹愼とを得させん爲なり
huwapa busara wajinga, maarifa na akili kwa vijana;
5 智慧ある者は之を聞て學にすすみ 哲者は智略をうべし
wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao, wenye kupambanua na wapate mwongozo;
6 人これによりて箴言と譬喩と智慧ある者の言とその隠語とを悟らん
kwa kufahamu mithali na mifano, misemo na vitendawili vya wenye hekima.
7 ヱホバを畏るるは知識の本なり 愚なる者は智慧と訓誨とを軽んず
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha maarifa, lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.
8 我が子よ汝の父の教をきけ 汝の母の法を棄ることなかれ
Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
9 これ汝の首の美しき冠となり 汝の項の妝飾とならん
Hayo yatakuwa taji la maua la neema kichwani pako, na mkufu wa kuipamba shingo yako.
10 わが子よ惡者なんぢ誘ふとも從ふことなかれ
Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi, usikubaliane nao.
11 彼等なんぢにむかひて請ふ われらと偕にきたれ 我儕まちぶせして人の血を流し 無辜ものを故なきに伏てねらひ
Kama wakisema, “Twende tufuatane; tukamvizie mtu na kumwaga damu, njoo tukavizie nafsi isiyo na hatia;
12 陰府のごとく彼等を活たるままにて呑み 壮健なる者を墳に下る者のごとくになさん (Sheol h7585)
tuwameze wakiwa hai kama kaburi, wakiwa wazima kama wale wanaotumbukia shimoni. (Sheol h7585)
13 われら各様のたふとき財貨をえ 奪ひ取たる物をもて我儕の家に盈さん
Tutapata aina zote za vitu vya thamani na kujaza nyumba zetu kwa nyara.
14 汝われらと偕に籤をひけ 我儕とともに一の金嚢を持べしと云とも
Njoo ushirikiane nasi, vitu vyote tutakavyopata tutagawana.”
15 我が子よ彼等とともに途を歩むことなかれ 汝の足を禁めてその路にゆくこと勿れ
Mwanangu, usiandamane nao. Usiweke mguu wako katika njia zao,
16 そは彼らの足は惡に趨り 血を流さんとて急げばなり
kwa kuwa miguu yao hukimbilia kwenye dhambi, ni wepesi kumwaga damu.
17 (すべて鳥の目の前にて羅を張は徒労なり)
Tazama ni jinsi gani ilivyo kazi bure kutandaza wavu wakati ndege wote wanakuona!
18 彼等はおのれの血のために埋伏し おのれの命をふしてねらふ
Watu hawa huvizia kumwaga damu yao wenyewe; hujivizia tu wenyewe!
19 凡て利を貧る者の途はかくの如し 是その持主をして生命をうしなはしむるなり
Huu ndio mwisho wa wote ambao wanajipatia mali kwa hila; huuondoa uhai wa wale wenye mali.
20 智慧外に呼はり衝に其聲をあげ
Hekima huita kwa sauti kuu barabarani, hupaza sauti yake kwenye viwanja vikubwa;
21 熱閙しき所にさけび 城市の門の口邑の中にその言をのぺていふ
kwenye makutano ya barabara za mji zenye makelele mengi hupaza sauti, kwenye malango ya mji hutoa hotuba yake:
22 なんぢら拙者のつたなきを愛し 嘲笑者のあざけりを樂しみ 愚なる者の知識を惡むは何時までぞや
“Enyi wajinga, mtangʼangʼania ujinga wenu hadi lini? Mpaka lini wenye mizaha watafurahia mizaha, na wapumbavu kuchukia maarifa?
23 わが督斥にしたがひて心を改めよ 視よわれ我が霊を汝らにそそぎ 我が言をなんぢらに示さん
Kama mngekuwa mmeitikia karipio langu, ningekuwa nimemimina roho yangu kwenu na kuwafahamisha maneno yangu.
24 われ呼たれども汝らこたへず 手を伸たれども顧る者なく
Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita na hakuna yeyote aliyekubali niliponyoosha mkono wangu,
25 かへつて我がすべての勧告をすて我が督斥を受ざりしに由り
kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote na hamkukubali karipio langu,
26 われ汝らが禍災にあふとき之を笑ひ 汝らの恐懼きたらんとき嘲るべし
mimi nami nitawacheka katika maafa yenu, nitawadhihaki wakati janga litawapata:
27 これは汝らのおそれ颶風の如くきたり 汝らのほろび颺風の如くきたり 艱難とかなしみと汝らにきたらん時なり
wakati janga litawapata kama tufani, wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli, wakati dhiki na taabu zitawalemea.
28 そのとき彼等われを呼ばん 然れどわれ應へじ 只管に我を求めん されど我に遇じ
“Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu; watanitafuta lakini hawatanipata.
29 かれら知識を憎み又ヱホバを畏るることを悦ばず
Kwa kuwa walichukia maarifa, wala hawakuchagua kumcha Bwana,
30 わが勤に從はず凡て我督斥をいやしめたるによりて
kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu, na kukataa maonyo yangu,
31 己の途の果を食ひおのれの策略に飽べし
watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa matunda ya hila zao.
32 拙者の違逆はおのれを殺し 愚なる者の幸福はおのれを滅さん
Kwa kuwa ukaidi wa wajinga utawaua, nako kuridhika kwa wajinga kutawaangamiza.
33 されど我に聞ものは平穏に住ひかつ禍害にあふ恐怖なくして安然ならん
Lakini yeyote anisikilizaye ataishi kwa usalama, atatulia, bila kuwa na hofu ya madhara.”

< 箴言 知恵の泉 1 >