< ヨブ 記 39 >

1 なんぢ岩間の山羊が子を産む時をしるや また麀鹿の産に臨むを見しや
“Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa? Je, watambua ni wakati gani kulungu jike azaapo mtoto wake?
2 なんぢ是等の在胎の月を數へうるや また是等が産む時を知るや
Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo? Je, unajua majira yao ya kuzaa?
3 これらは身を鞠めて子を産みその痛苦を出す
Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao; utungu wa kuzaa unakoma.
4 またその子は強くなりて野に育ち 出ゆきて再たびその親にかへらず
Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani; huenda zao wala hawarudi tena.
5 誰が野驢馬を放ちて自由にせしや 誰が野驢馬の繋繩を解しや
“Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru? Ni nani aliyezifungua kamba zake?
6 われ野をその家となし 荒野をその住所となせり
Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake, nchi ya chumvi kuwa makao yake.
7 是は邑の喧閙を賤しめ 馭者の號呼を聽いれず
Huzicheka ghasia za mji, wala hasikii kelele za mwendesha gari.
8 山を走まはりて草を食ひ 各種の青き物を尋ぬ
Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho na kutafuta kila kitu kibichi.
9 兕肯て汝に事へ なんぢの飼草槽の傍にとどまらんや
“Je, nyati atakubali kukutumikia? Atakaa karibu na hori lako usiku?
10 なんぢ兕に綱附て阡陌をあるかせ得んや 是あに汝にしたがひて谷に馬鈀を牽んや
Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba? Je, atalima mabonde nyuma yako?
11 その力おほいなればとて汝これに恃まんや またなんぢの工事をこれに任せんや
Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi? Utamwachia yeye kazi zako nzito?
12 なんぢこれにたよりて己が穀物を運びかへらせ之を打禾塲にあつめしめんや
Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani kutoka shambani na kuikusanya kwenye sakafu yako ya kupuria?
13 駝鳥は歡然にその翼を皷ふ 然どもその羽と毛とはあに鶴にしかんや
“Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha, lakini hayawezi kulinganishwa na mabawa na manyoya ya korongo.
14 是はその卵を土の中に棄おき これを砂の中にて暖たまらしめ
Huyataga mayai yake juu ya ardhi, na kuyaacha yapate joto mchangani,
15 足にてその潰さるべきと 野の獸のこれを踐むべきとを思はず
bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda, kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.
16 これはその子に情なくして宛然おのれの子ならざるが如くし その劬勞の空しくなるも繋念ところ無し
Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake; hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,
17 是は神これに智慧を授けず穎悟を與へざるが故なり
kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima, wala hakumpa fungu la akili njema.
18 その身をおこして走るにおいては馬をもその騎手をも嘲るべし
Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia, humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.
19 なんぢ馬に力を與へしや その頸に勇ましき鬣を粧ひしや
“Je, wewe humpa farasi nguvu au kuivika shingo yake manyoya marefu?
20 なんぢ之を蝗蟲のごとく飛しむるや その嘶なく聲の響は畏るべし
Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige, akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?
21 谷を踋爬て力に誇り 自ら進みて兵士に向ふ
Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake, husonga mbele kukabiliana na silaha.
22 懼るることを笑ひて驚ろくところ無く 劍にむかふとも退ぞかず
Huicheka hofu, haogopi chochote, wala haukimbii upanga.
23 矢筒その上に鳴り 鎗に矛あひきらめく
Podo hutoa sauti kando yake, pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.
24 猛りつ狂ひつ地を一呑にし 喇叭の聲鳴わたるも立どまる事なし
Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi, wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.
25 喇叭の鳴ごとにハーハーと言ひ遠方より戰鬪を嗅つけ 將帥の大聲および吶喊聲を聞しる
Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’ Hunusa harufu ya vita toka mbali, sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.
26 鷹の飛かけり その羽翼を舒て南に向ふは豈なんぢの智慧によるならんや
“Je, mwewe huruka kwa hekima yako na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?
27 鷲の翔のぼり 高き處に巣を營なむは豈なんぢの命令に依んや
Je, tai hupaa juu kwa amri yako na kujenga kiota chake mahali pa juu?
28 これは岩の上に住所を構へ 岩の尖所または峻險き所に居り
Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku; majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.
29 其處よりして攫むべき物をうかがふ その目のおよぶところ遠し
Kutoka huko hutafuta chakula chake; macho yake hukiona kutoka mbali.
30 その子等もまた血を吸ふ 凡そ殺されし者のあるところには是そこに在り
Makinda yake hujilisha damu, na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”

< ヨブ 記 39 >