< ヨブ 記 3 >
Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
3 我が生れし日亡びうせよ 男子胎にやどれりと言し夜も亦然あれ
“Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
4 その日は暗くなれ 神上よりこれを顧みたまはざれ 光これを照す勿れ
Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
5 暗闇および死蔭これを取りもどせ 雲これが上をおほえ 日を暗くする者これを懼しめよ
Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
6 その夜は黒暗の執ふる所となれ 年の日の中に加はらざれ 月の數に入ざれ
Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
7 その夜は孕むこと有ざれ 歡喜の聲その中に興らざれ
Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
8 日を詛ふ者レビヤタンを激發すに巧なる者これを詛へ
Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
9 その夜の晨星は暗かれ その夜には光明を望むも得ざらしめ 又東雲の眼蓋を見ざらしめよ
Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
10 是は我母の胎の戸を闔ずまた我目に憂を見ること無らしめざりしによる
kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
11 何とて我は胎より死て出ざりしや 何とて胎より出し時に氣息たえざりしや
Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
12 如何なれば膝ありてわれを接しや 如何なれば乳房ありてわれを養ひしや
kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
13 否らずば今は我偃して安んじかつ眠らん 然ばこの身やすらひをり
Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
14 かの荒墟を自己のために築きたりし世の君等臣等と偕にあり
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
15 かの黄金を有ち白銀を家に充したりし牧伯等と偕にあらん
Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
16 又人しれず墮る胎兒のごとくにして世を出ず また光を見ざる赤子のごとくならん
Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
17 彼處にては惡き者 虐遇を息め倦憊たる者安息を得
Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
18 彼處にては俘囚人みな共に安然に居りて驅使者の聲を聞ず
Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
19 小き者も大なる者も同じく彼處にあり僕も主の手を離る
Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
20 如何なれば艱難にをる者に光を賜ひ 心苦しむ者に生命をたまひしや
Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
21 斯る者は死を望むなれどもきたらず これをもとむるは藏れたる寳を掘るよりも甚だし
ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
23 その道かくれ神に取籠られをる人に如何なれば光明を賜ふや
Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
24 わが歎息はわが食物に代り我呻吟は水の流れそそぐに似たり
Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
25 我が戰慄き懼れし者我に臨み我が怖懼れたる者この身に及べり
Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
26 我は安然ならず穩ならず安息を得ず唯艱難のみきたる
Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”