< 詩篇 73 >
1 アサフの歌 神は正しい者にむかい、心の清い者にむかって、まことに恵みふかい。
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 しかし、わたしは、わたしの足がつまずくばかり、わたしの歩みがすべるばかりであった。
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 これはわたしが、悪しき者の栄えるのを見て、その高ぶる者をねたんだからである。
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 彼らには苦しみがなく、その身はすこやかで、つやがあり、
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5 ほかの人々のように悩むことがなく、ほかの人々のように打たれることはない。
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 それゆえ高慢は彼らの首飾となり、暴力は衣のように彼らをおおっている。
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7 彼らは肥え太って、その目はとびいで、その心は愚かな思いに満ちあふれている。
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8 彼らはあざけり、悪意をもって語り、高ぶって、しえたげを語る。
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9 彼らはその口を天にさからって置き、その舌は地をあるきまわる。
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10 それゆえ民は心を変えて彼らをほめたたえ、彼らのうちにあやまちを認めない。
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11 彼らは言う、「神はどうして知り得ようか、いと高き者に知識があろうか」と。
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12 見よ、これらは悪しき者であるのに、常に安らかで、その富が増し加わる。
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
13 まことに、わたしはいたずらに心をきよめ、罪を犯すことなく手を洗った。
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14 わたしはひねもす打たれ、朝ごとに懲しめをうけた。
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15 もしわたしが「このような事を語ろう」と言ったなら、わたしはあなたの子らの代を誤らせたであろう。
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16 しかし、わたしがこれを知ろうと思いめぐらしたとき、これはわたしにめんどうな仕事のように思われた。
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17 わたしが神の聖所に行って、彼らの最後を悟り得たまではそうであった。
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18 まことにあなたは彼らをなめらかな所に置き、彼らを滅びに陥らせられる。
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19 なんと彼らはまたたくまに滅ぼされ、恐れをもって全く一掃されたことであろう。
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20 あなたが目をさまして彼らの影をかろしめられるとき、彼らは夢みた人の目をさました時のようである。
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
21 わたしの魂が痛み、わたしの心が刺されたとき、
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22 わたしは愚かで悟りがなく、あなたに対しては獣のようであった。
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23 けれどもわたしは常にあなたと共にあり、あなたはわたしの右の手を保たれる。
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24 あなたはさとしをもってわたしを導き、その後わたしを受けて栄光にあずからせられる。
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25 わたしはあなたのほかに、だれを天にもち得よう。地にはあなたのほかに慕うものはない。
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26 わが身とわが心とは衰える。しかし神はとこしえにわが心の力、わが嗣業である。
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27 見よ、あなたに遠い者は滅びる。あなたは、あなたにそむく者を滅ぼされる。
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 しかし神に近くあることはわたしに良いことである。わたしは主なる神をわが避け所として、あなたのもろもろのみわざを宣べ伝えるであろう。
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.