< 詩篇 102 >

1 苦しむ者が思いくずおれてその嘆きを主のみ前に注ぎ出すときの祈 主よ、わたしの祈をお聞きください。わたしの叫びをみ前に至らせてください。
Maombi ya mtu aliyechoka. Anapoteseka na kumimina malalamiko yake kwa Bwana. Ee Bwana, usikie maombi yangu, kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.
2 わたしの悩みの日にみ顔を隠すことなく、あなたの耳をわたしに傾け、わが呼ばわる日に、すみやかにお答えください。
Usinifiche uso wako ninapokuwa katika shida. Unitegee sikio lako, ninapoita, unijibu kwa upesi.
3 わたしの日は煙のように消え、わたしの骨は炉のように燃えるからです。
Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi, mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.
4 わたしの心は草のように撃たれて、しおれました。わたしはパンを食べることを忘れました。
Moyo wangu umefifia na kunyauka kama jani, ninasahau kula chakula changu.
5 わが嘆きの声によってわたしの骨はわたしの肉に着きます。
Kwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu, nimebakia ngozi na mifupa.
6 わたしは荒野のはげたかのごとく、荒れた跡のふくろうのようです。
Nimekuwa kama bundi wa jangwani, kama bundi kwenye magofu.
7 わたしは眠らずに屋根にひとりいるすずめのようです。
Nilalapo sipati usingizi, nimekuwa kama ndege mpweke kwenye paa la nyumba.
8 わたしの敵はひねもす、わたしをそしり、わたしをあざける者はわが名によってのろいます。
Mchana kutwa adui zangu hunidhihaki, wale wanaonizunguka hutumia jina langu kama laana.
9 わたしは灰をパンのように食べ、わたしの飲み物に涙を交えました。
Ninakula majivu kama chakula changu na nimechanganya kinywaji changu na machozi
10 これはあなたの憤りと怒りのゆえです。あなたはわたしをもたげて投げすてられました。
kwa sababu ya ghadhabu yako kuu, kwa maana umeniinua na kunitupa kando.
11 わたしのよわいは夕暮の日影のようです。わたしは草のようにしおれました。
Siku zangu ni kama kivuli cha jioni, ninanyauka kama jani.
12 しかし主よ、あなたはとこしえにみくらに座し、そのみ名はよろず代に及びます。
Lakini wewe, Ee Bwana, umeketi katika kiti chako cha enzi milele, sifa zako za ukuu zaendelea vizazi vyote.
13 あなたは立ってシオンをあわれまれるでしょう。これはシオンを恵まれる時であり、定まった時が来たからです。
Utainuka na kuihurumia Sayuni, kwa maana ni wakati wa kumwonyesha wema; wakati uliokubalika umewadia.
14 あなたのしもべはシオンの石をも喜び、そのちりをさえあわれむのです。
Kwa maana mawe yake ni ya thamani kwa watumishi wako, vumbi lake lenyewe hulionea huruma.
15 もろもろの国民は主のみ名を恐れ、地のもろもろの王はあなたの栄光を恐れるでしょう。
Mataifa wataogopa jina la Bwana, wafalme wote wa dunia watauheshimu utukufu wako.
16 主はシオンを築き、その栄光をもって現れ、
Kwa maana Bwana ataijenga tena Sayuni na kutokea katika utukufu wake.
17 乏しい者の祈をかえりみ、彼らの願いをかろしめられないからです。
Ataitikia maombi ya mtu mkiwa, wala hatadharau hoja yao.
18 きたるべき代のために、この事を書きしるしましょう。そうすれば新しく造られる民は、主をほめたたえるでしょう。
Hili na liandikwe kwa ajili ya kizazi kijacho, ili taifa litakaloumbwa baadaye waweze kumsifu Bwana:
19 主はその聖なる高き所から見おろし、天から地を見られた。
“Bwana alitazama chini kutoka patakatifu pake palipo juu, kutoka mbinguni alitazama dunia,
20 これは捕われ人の嘆きを聞き、死に定められた者を解き放ち、
kusikiliza vilio vya uchungu vya wafungwa na kuwaweka huru wale waliohukumiwa kufa.”
21 人々がシオンで主のみ名をあらわし、エルサレムでその誉をあらわすためです。
Kwa hiyo jina la Bwana latangazwa huko Sayuni na sifa zake katika Yerusalemu,
22 その時もろもろの民、もろもろの国はともに集まって、主に仕えるでしょう。
wakati mataifa na falme zitakapokusanyika ili kumwabudu Bwana.
23 主はわたしの力を中途でくじき、わたしのよわいを短くされました。
Katika kuishi kwangu alivunja nguvu zangu, akafupisha siku zangu.
24 わたしは言いました、「わが神よ、どうか、わたしのよわいの半ばでわたしを取り去らないでください。あなたのよわいはよろず代に及びます」と。
Ndipo niliposema: “Ee Mungu wangu, usinichukue katikati ya siku zangu; miaka yako inaendelea vizazi vyote.
25 あなたはいにしえ、地の基をすえられました。天もまたあなたのみ手のわざです。
Hapo mwanzo uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
26 これらは滅びるでしょう。しかしあなたは長らえられます。これらはみな衣のように古びるでしょう。あなたがこれらを上着のように替えられると、これらは過ぎ去ります。
Hizi zitatoweka, lakini wewe utadumu, zote zitachakaa kama vazi. Utazibadilisha kama nguo nazo zitaondoshwa.
27 しかしあなたは変ることなく、あなたのよわいは終ることがありません。
Lakini wewe, U yeye yule, nayo miaka yako haikomi kamwe.
28 あなたのしもべの子らは安らかに住み、その子孫はあなたの前に堅く立てられるでしょう。
Watoto wa watumishi wako wataishi mbele zako; wazao wao wataimarishwa mbele zako.”

< 詩篇 102 >