< 箴言 知恵の泉 9 >

1 知恵は自分の家を建て、その七つの柱を立て、
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
2 獣をほふり、酒を混ぜ合わせて、ふるまいを備え、
Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
3 はしためをつかわして、町の高い所で呼ばわり言わせた、
Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
4 「思慮のない者よ、ここに来れ」と。また、知恵のない者に言う、
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
5 「来て、わたしのパンを食べ、わたしの混ぜ合わせた酒をのみ、
Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
6 思慮のないわざを捨てて命を得、悟りの道を歩め」と。
Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 あざける者を戒める者は、自ら恥を得、悪しき者を責める者は自ら傷を受ける。
“Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
8 あざける者を責めるな、おそらく彼はあなたを憎むであろう。知恵ある者を責めよ、彼はあなたを愛する。
Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
9 知恵ある者に教訓を授けよ、彼はますます知恵を得る。正しい者を教えよ、彼は学に進む。
Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
10 主を恐れることは知恵のもとである、聖なる者を知ることは、悟りである。
“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
11 わたしによって、あなたの日は多くなり、あなたの命の年は増す。
Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
12 もしあなたに知恵があるならば、あなた自身のために知恵があるのである。もしあなたがあざけるならば、あなたひとりがその責めを負うことになる。
Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
13 愚かな女は、騒がしく、みだらで、恥を知らない。
Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
14 彼女はその家の戸口に座し、町の高い所にある座にすわり、
Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
15 道を急ぐ行き来の人を招いて言う、
akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
16 「思慮のない者よ、ここに来れ」と。また知恵のない人に向かってこれに言う、
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
17 「盗んだ水は甘く、ひそかに食べるパンはうまい」と。
“Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
18 しかしその人は、死の影がそこにあることを知らず、彼女の客は陰府の深みにおることを知らない。 (Sheol h7585)
Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)

< 箴言 知恵の泉 9 >