< 箴言 知恵の泉 24 >
1 悪を行う人をうらやんではならない、また彼らと共におることを願ってはならない。
Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
2 彼らはその心に強奪を計り、そのくちびるに人をそこなうことを語るからである。
kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
3 家は知恵によって建てられ、悟りによって堅くせられ、
Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
4 また、へやは知識によってさまざまの尊く、麗しい宝で満たされる。
kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
5 知恵ある者は強い人よりも強く、知識ある人は力ある人よりも強い。
Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
6 良い指揮によって戦いをすることができ、勝利は多くの議する者がいるからである。
kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
7 知恵は高くて愚かな者の及ぶところではない、愚かな者は門で口を開くことができない。
Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
8 悪を行うことを計る者を人はいたずら者ととなえる。
Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
9 愚かな者の計るところは罪であり、あざける者は人に憎まれる。
Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
10 もしあなたが悩みの日に気をくじくならば、あなたの力は弱い。
Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
11 死地にひかれゆく者を助け出せ、滅びによろめきゆく者を救え。
Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
12 あなたが、われわれはこれを知らなかったといっても、心をはかる者はそれを悟らないであろうか。あなたの魂を守る者はそれを知らないであろうか。彼はおのおのの行いにより、人に報いないであろうか。
Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
13 わが子よ、蜜を食べよ、これは良いものである、また、蜂の巣のしたたりはあなたの口に甘い。
Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
14 知恵もあなたの魂にはそのようであることを知れ。それを得るならば、かならず報いがあって、あなたの望みは、すたらない。
Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
15 悪しき者がするように、正しい者の家をうかがってはならない、その住む所に乱暴をしてはならない。
Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
16 正しい者は七たび倒れても、また起きあがる、しかし、悪しき者は災によって滅びる。
Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
17 あなたのあだが倒れるとき楽しんではならない、彼のつまずくとき心に喜んではならない。
Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
18 主はそれを見て悪いこととし、その怒りを彼から転じられる。
Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
19 悪を行う者のゆえに心を悩ましてはならない、よこしまな者をうらやんではならない。
Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
20 悪しき者には後の良い報いはない、よこしまな者のともしびは消される。
kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
21 わが子よ、主と王とを恐れよ、そのいずれにも不従順であってはならない。
Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
22 その災はたちまち起るからである。この二つの者からくる滅びをだれが知り得ようか。
kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
23 これらもまた知恵ある者の箴言である。片寄ったさばきをするのは、よくない。
Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
24 悪しき者に向かって、「あなたは正しい」という者を、人々はのろい、諸民は憎む。
Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
25 悪しき者をせめる者は恵みを得る、また幸福が与えられる。
Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
26 正しい答をする者は、くちびるに、口づけするのである。
Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
27 外で、あなたの仕事を整え、畑で、すべての物をおのれのために備え、その後あなたの家を建てるがよい。
Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
28 ゆえなく隣り人に敵して、証言をしてはならない、くちびるをもって欺いてはならない。
Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
29 「彼がわたしにしたように、わたしも彼にしよう、わたしは人がしたところにしたがって、その人に報いよう」と言ってはならない。
Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
30 わたしはなまけ者の畑のそばと、知恵のない人のぶどう畑のそばを通ってみたが、
Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
31 いばらが一面に生え、あざみがその地面をおおい、その石がきはくずれていた。
miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
32 わたしはこれをみて心をとどめ、これを見て教訓を得た。
Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
33 「しばらく眠り、しばらくまどろみ、手をこまぬいて、またしばらく休む」。
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
34 それゆえ、貧しさは盗びとのように、あなたに来、乏しさは、つわもののように、あなたに来る。
hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.