< 箴言 知恵の泉 16 >
1 心にはかることは人に属し、舌の答は主から出る。
Mipango ya moyo ni ya mtu, bali Yehova hutoa jawabu kutoka kwenye ulimi wake.
2 人の道は自分の目にことごとく潔しと見える、しかし主は人の魂をはかられる。
Njia zote za mtu ni safi kwenye macho yake mwenyewe, bali Yehova huipima mioyo.
3 あなたのなすべき事を主にゆだねよ、そうすれば、あなたの計るところは必ず成る。
Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
4 主はすべての物をおのおのその用のために造り、悪しき人をも災の日のために造られた。
Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
5 すべて心に高ぶる者は主に憎まれる、確かに、彼は罰を免れない。
Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
6 いつくしみとまことによって、とがはあがなわれる、主を恐れることによって、人は悪を免れる。
Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
7 人の道が主を喜ばせる時、主はその人の敵をもその人と和らがせられる。
Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
8 正義によって得たわずかなものは、不義によって得た多くの宝にまさる。
Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
9 人は心に自分の道を考え計る、しかし、その歩みを導く者は主である。
Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
10 王のくちびるには神の決定がある、さばきをするとき、その口に誤りがない。
Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
11 正しいはかりと天びんとは主のものである、袋にあるふんどうもすべて彼の造られたものである。
Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.
12 悪を行うことは王の憎むところである、その位が正義によって堅く立っているからである。
Wafalme wanapofanya mambo maovu, hicho ni kitu cha kudharauliwa, kwa maana utawala huimarishwa kwa kutenda haki.
13 正しいくちびるは王に喜ばれる、彼は正しい事を言う者を愛する。
Mfalme hufurahia midomo ambayo husema haki na anampenda mwenye kusema waziwazi.
14 王の怒りは死の使者である、知恵ある人はこれをなだめる。
Hasira ya mfalme ni mjumbe wa mauti lakini mtu mwenye busara atajaribu kutuliza hasira yake.
15 王の顔の光には命がある、彼の恵みは春雨をもたらす雲のようだ。
Katika nuru ya uso wa mfalme ni uzima na fadhila yake ni kama wingu linaloleta mvua ya masika.
16 知恵を得るのは金を得るのにまさる、悟りを得るのは銀を得るよりも望ましい。
Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu. Kuchagua kupata ufahamu ni zaidi kuliko fedha.
17 悪を離れることは正しい人の道である、自分の道を守る者はその魂を守る。
Njia kuu ya watu waadilifu hujitenga na ubaya; mwenye kuyahifadhi maisha yake huilinda njia yake.
18 高ぶりは滅びにさきだち、誇る心は倒れにさきだつ。
Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
19 へりくだって貧しい人々と共におるのは、高ぶる者と共にいて、獲物を分けるにまさる。
Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
20 慎んで、み言葉をおこなう者は栄える、主に寄り頼む者はさいわいである。
Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
21 心に知恵ある者はさとき者ととなえられる、くちびるが甘ければ、その教に人を説きつける力を増す。
Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
22 知恵はこれを持つ者に命の泉となる、しかし、愚かさは愚かな者の受ける懲しめである。
Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
23 知恵ある者の心はその言うところを賢くし、またそのくちびるに人を説きつける力を増す。
Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
24 ここちよい言葉は蜂蜜のように、魂に甘く、からだを健やかにする。
Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
25 人が見て自分で正しいとする道があり、その終りはついに死にいたる道となるものがある。
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
26 ほねおる者は飲食のためにほねおる、その口が自分に迫るからである。
Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
27 よこしまな人は悪を企てる、そのくちびるには激しい火のようなものがある。
Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
28 偽る者は争いを起し、つげ口する者は親しい友を離れさせる。
Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
29 しえたげる者はその隣り人をいざない、これを良くない道に導く。
Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
30 めくばせする者は悪を計り、くちびるを縮める者は悪事をなし遂げる。
Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
31 しらがは栄えの冠である、正しく生きることによってそれが得られる。
Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
32 怒りをおそくする者は勇士にまさり、自分の心を治める者は城を攻め取る者にまさる。
Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
33 人はくじをひく、しかし事を定めるのは全く主のことである。
Kura hurushwa kwenye mkunjo, bali maamuzi hutoka kwa Yehova.