< ヨブ 記 35 >
2 「あなたはこれを正しいと思うのか、あなたは『神の前に自分は正しい』と言うのか。
“Je, unadhani hili ni haki? Wewe unasema, ‘Nina haki mbele za Mungu.’
3 あなたは言う、『これはわたしになんの益があるか、罪を犯したのとくらべてなんのまさるところがあるか』と。
Bado unamuuliza, ‘Ni faida gani nimepata, na imenifaidi nini kwa kutokutenda dhambi?’
4 わたしはあなたおよび、あなたと共にいるあなたの友人たちに答えよう。
“Ningependa nikujibu wewe pamoja na marafiki zako walio pamoja nawe.
5 天を仰ぎ見よ、あなたの上なる高き空を望み見よ。
Tazama juu mbinguni ukaone; yaangalie mawingu yaliyo juu sana juu yako.
6 あなたが罪を犯しても、彼になんのさしさわりがあるか。あなたのとがが多くても、彼に何をなし得ようか。
Je, ukitenda dhambi, inamdhuruje Mungu? Kama dhambi zako zikiwa nyingi, hilo linamfanyia nini Mungu?
7 またあなたは正しくても、彼に何を与え得ようか。彼はあなたの手から何を受けられるであろうか。
Kama wewe ni mwadilifu, unampa nini, au yeye anapokea nini mkononi kwako?
8 あなたの悪はただあなたのような人にかかわり、あなたの義はただ人の子にかかわるのみだ。
Uovu wako unamdhuru tu mtu mwingine kama wewe, nayo haki yako inawafaa wanadamu tu.
9 しえたげの多いために叫び、力ある者の腕のゆえに呼ばわる人々がある。
“Wanadamu hulia kwa kulemewa na mateso; huomba msaada kutoka mkono wenye nguvu.
10 しかし、ひとりとして言う者はない、『わが造り主なる神はどこにおられるか、彼は夜の間に歌を与え、
Lakini hakuna asemaye, ‘Yuko wapi Mungu Muumba wangu, yeye anifanyaye niimbe usiku,
11 地の獣よりも多く、われわれを教え、空の鳥よりも、われわれを賢くされる方である』と。
yeye atufundishaye sisi zaidi kuliko wanyama wa dunia, na kutufanya wenye hekima kuliko ndege wa angani?’
12 彼らが叫んでも答えられないのは、悪しき者の高ぶりによる。
Yeye hajibu wakati watu waliapo kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.
13 まことに神はむなしい叫びを聞かれない。また全能者はこれを顧みられない。
Naam, Mungu hasikilizi maombi yao ya ubatili; Mwenyezi hayazingatii.
14 あなたが彼を見ないと言う時はなおさらだ。さばきは神の前にある。あなたは彼を待つべきである。
Si zaidi sana kwamba hatakusikiliza wewe usemapo humwoni, tena ya kwamba shauri lako liko mbele zake na wewe lazima umngojee,
15 今彼が怒りをもって罰せず、罪とがを深く心にとめられないゆえに
pia zaidi, kwamba hasira yake kamwe haiadhibu wala haangalii uovu hata kidogo?
16 ヨブは口を開いてむなしい事を述べ、無知の言葉をしげくする」。
Hivyo Ayubu hufumbua kinywa chake kwa maneno yasiyo na maana; anaongea maneno mengi bila maarifa.”