< ヨブ 記 22 >

1 そこでテマンびとエリパズは答えて言った、
Ndipo Elifazi Mtemani akajibu:
2 「人は神を益することができるであろうか。賢い人も、ただ自身を益するのみである。
“Je, mwanadamu aweza kuwa wa faida kwa Mungu? Je, hata mtu mwenye hekima aweza kumfaidi?
3 あなたが正しくても、全能者になんの喜びがあろう。あなたが自分の道を全うしても、彼になんの利益があろう。
Je, Mwenyezi angefurahia nini kama ungekuwa mwadilifu? Au je, yeye angepata faida gani kama njia zako zingekuwa kamilifu?
4 神はあなたが神を恐れることのゆえに、あなたを責め、あなたをさばかれるであろうか。
“Je, ni kwa ajili ya utaua wako ndiyo maana anakukemea na kuleta mashtaka dhidi yako?
5 あなたの悪は大きいではないか。あなたの罪は、はてしがない。
Je, uovu wako si mkuu? Dhambi zako si hazina mwisho?
6 あなたはゆえなく兄弟のものを質にとり、裸な者の着物をはぎ取り、
Umedai dhamana kwa ndugu zako bila sababu; umewavua watu nguo zao, ukawaacha uchi.
7 疲れた者に水を飲ませず、飢えた者に食物を与えなかった。
Hukumpa maji aliyechoka, nawe ulimnyima chakula mwenye njaa,
8 力ある人は土地を得、名ある人はそのうちに住んだ。
ingawa ulikuwa mtu mwenye uwezo ukimiliki nchi: mtu uliyeheshimiwa, ukiishi ndani yake.
9 あなたは、やもめをむなしく去らせた。みなしごの腕は折られた。
Umewafukuza wajane mikono mitupu na kuzivunja nguvu za yatima.
10 それゆえ、わなはあなたをめぐり、恐怖は、にわかにあなたを驚かす。
Ndiyo sababu mitego imekuzunguka pande zote, hatari ya ghafula inakutia hofu,
11 あなたの光は暗くされ、あなたは見ることができない。大水はあなたをおおうであろう。
ndiyo sababu ni giza sana huwezi kuona, tena ndiyo sababu mafuriko ya maji yamekufunika.
12 神は天に高くおられるではないか。見よ、いと高き星を。いかに高いことよ。
“Je, Mungu hayuko katika mbingu za juu? Juu kuliko nyota zilizo juu sana!
13 それであなたは言う、『神は何を知っておられるか。彼は黒雲を通して、さばくことができるのか。
Hivyo wewe wasema, ‘Mungu anajua nini?’ Je, yeye huhukumu katika giza kama hilo?
14 濃い雲が彼をおおい隠すと、彼は見ることができない。彼は天の大空を歩まれるのだ』と。
Mawingu mazito ni pazia lake, hivyo hatuoni sisi atembeapo juu ya anga la dunia.
15 あなたは悪しき人々が踏んだいにしえの道を守ろうとするのか。
Je, utaifuata njia ya zamani, ambayo watu waovu waliikanyaga?
16 彼らは時がこないうちに取り去られ、その基は川のように押し流された。
Waliondolewa kabla ya wakati wao, misingi yao ikachukuliwa na mafuriko.
17 彼らは神に言った、『われわれを離れてください』と、また『全能者はわれわれに何をなしえようか』と。
Walimwambia Mungu, ‘Tuache sisi! Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini?’
18 しかし神は彼らの家を良い物で満たされた。ただし悪人の計りごとはわたしのくみする所ではない。
Lakini ndiye alizijaza nyumba zao na vitu vizuri, hivyo ninajitenga mbali na mashauri ya waovu.
19 正しい者はこれを見て喜び、罪なき者は彼らをあざ笑って言う、
“Wenye haki wanaona maangamizi yao na kufurahi, nao wasio na hatia huwadhihaki, wakisema,
20 『まことにわれわれのあだは滅ぼされ、その残した物は火で焼き滅ぼされた』と。
‘Hakika adui zetu wameangamizwa, nao moto umeteketeza mali zao.’
21 あなたは神と和らいで、平安を得るがよい。そうすれば幸福があなたに来るでしょう。
“Mjue sana Mungu ili uwe na amani, ndipo mema yatakapokujia.
22 どうか、彼の口から教を受け、その言葉をあなたの心におさめるように。
Uyapokee mafundisho toka kinywani mwake, na maneno yake uyaweke moyoni mwako.
23 あなたがもし全能者に立ち返って、おのれを低くし、あなたの天幕から不義を除き去り、
Kama ukimrudia Mwenyezi, utarudishwa upya: Kama ukiuondoa uovu uwe mbali na hema lako,
24 こがねをちりの中に置き、オフルのこがねを谷川の石の中に置き、
kama dhahabu yako ukiihesabu kama mavumbi, dhahabu yako ya Ofiri kama miamba ya mabondeni,
25 全能者があなたのこがねとなり、あなたの貴重なしろがねとなるならば、
ndipo Mwenyezi atakuwa dhahabu yako, naye atakuwa fedha yako iliyo bora.
26 その時、あなたは全能者を喜び、神に向かって顔をあげることができる。
Hakika ndipo utakapojifurahisha kwa Mwenyezi, nawe utamwinulia Mungu uso wako.
27 あなたが彼に祈るならば、彼はあなたに聞かれる。そしてあなたは自分の誓いを果す。
Utamwomba yeye, naye atakusikia, nawe utazitimiza nadhiri zako.
28 あなたが事をなそうと定めるならば、あなたはその事を成就し、あなたの道には光が輝く。
Utakusudia jambo nalo litatendeka, nao mwanga utaangazia njia zako.
29 彼は高ぶる者を低くされるが、へりくだる者を救われるからだ。
Watu watakaposhushwa, nawe ukasema, ‘Wainue!’ ndipo atamwokoa aliyevunjika moyo.
30 彼は罪のない者を救われる。あなたはその手の潔いことによって、救われるであろう」。
Atamwokoa hata yule ambaye ana hatia, ataokolewa kwa sababu ya usafi wa mikono yako.”

< ヨブ 記 22 >