< ヨブ 記 19 >

1 そこでヨブは答えて言った、
Ndipo Ayubu akajibu:
2 「あなたがたはいつまでわたしを悩まし、言葉をもってわたしを打ち砕くのか。
“Je, mtaendelea kunitesa mpaka lini, na kuniponda kwa maneno yenu?
3 あなたがたはすでに十度もわたしをはずかしめ、わたしを悪くあしらってもなお恥じないのか。
Mara kumi hizi mmenishutumu; bila aibu mnanishambulia.
4 たといわたしが、まことにあやまったとしても、そのあやまちは、わたし自身にとどまる。
Kama ni kweli nimepotoka, kosa langu ninabaki kuhusika nalo mwenyewe.
5 もしあなたがたが、まことにわたしに向かって高ぶり、わたしの恥を論じるならば、
Kama kweli mngejitukuza wenyewe juu yangu, na kutumia unyonge wangu dhidi yangu,
6 『神がわたしをしえたげ、その網でわたしを囲まれたのだ』と知るべきだ。
basi jueni kuwa Mungu amenitendea yaliyo mabaya, naye amekokota wavu wake kunizunguka.
7 見よ、わたしが『暴虐』と叫んでも答えられず、助けを呼び求めても、さばきはない。
“Ingawa ninalia, ‘Nimetendewa mabaya!’ sipati jibu; ingawa ninaomba msaada, hakuna haki.
8 彼はわたしの道にかきをめぐらして、越えることのできないようにし、わたしの行く道に暗やみを置かれた。
Yeye ameizuia njia yangu hivyo siwezi kupita; ameyafunika mapito yangu na giza.
9 彼はわたしの栄えをわたしからはぎ取り、わたしのこうべから冠を奪い、
Amenivua heshima yangu, na kuniondolea taji kichwani pangu.
10 四方からわたしを取りこわして、うせさせ、わたしの望みを木のように抜き去り、
Amenibomoa kila upande hadi nimeisha; amelingʼoa tegemeo langu kama mti.
11 わたしに向かって怒りを燃やし、わたしを敵のひとりのように思われた。
Hasira yake imewaka juu yangu; amenihesabu kuwa miongoni mwa adui zake.
12 その軍勢がいっせいに来て、塁を築いて攻め寄せ、わたしの天幕のまわりに陣を張った。
Majeshi yake yananisogelea kwa nguvu; yamenizingira, yamepiga kambi kulizunguka hema langu.
13 彼はわたしの兄弟たちをわたしから遠く離れさせられた。わたしを知る人々は全くわたしに疎遠になった。
“Amewatenga ndugu zangu mbali nami; wale tunaojuana nao wamefarakana nami kabisa.
14 わたしの親類および親しい友はわたしを見捨て、
Watu wa jamaa yangu wamekwenda mbali; rafiki zangu wamenisahau.
15 わたしの家に宿る者はわたしを忘れ、わたしのはしためらはわたしを他人のように思い、わたしは彼らの目に他国人となった。
Wageni wangu na watumishi wangu wa kike wananiona kama mgeni; wananitazama kama mgeni.
16 わたしがしもべを呼んでも、彼は答えず、わたしは口をもって彼に請わなければならない。
Namwita mtumishi wangu, wala haitiki, ingawa namwomba kwa kinywa changu mwenyewe.
17 わたしの息はわが妻にいとわれ、わたしは同じ腹の子たちにきらわれる。
Pumzi ya kinywa changu ni kinyaa kwa mke wangu; nimekuwa chukizo mno kwa ndugu zangu mwenyewe.
18 わらべたちさえもわたしを侮り、わたしが起き上がれば、わたしをあざける。
Hata watoto wadogo hunidhihaki; ninapojitokeza, hunifanyia mzaha.
19 親しい人々は皆わたしをいみきらい、わたしの愛した人々はわたしにそむいた。
Rafiki zangu wa moyoni wote wananichukia kabisa; wale niwapendao wamekuwa kinyume nami.
20 わたしの骨は皮と肉につき、わたしはわずかに歯の皮をもってのがれた。
Mimi nimebaki mifupa na ngozi tu; nimeponea nikiwa karibu kufa.
21 わが友よ、わたしをあわれめ、わたしをあわれめ、神のみ手がわたしを打ったからである。
“Nihurumieni, rafiki zangu, kuweni na huruma, kwa kuwa mkono wa Mungu umenipiga.
22 あなたがたは、なにゆえ神のようにわたしを責め、わたしの肉をもって満足しないのか。
Kwa nini mnanifuatia kama Mungu afanyavyo? Hamtosheki kamwe na mwili wangu?
23 どうか、わたしの言葉が、書きとめられるように。どうか、わたしの言葉が、書物にしるされるように。
“Laiti maneno yangu yangewekwa kwenye kumbukumbu, laiti kwamba yangeandikwa kwenye kitabu,
24 鉄の筆と鉛とをもって、ながく岩に刻みつけられるように。
kwamba yangechorwa kwenye risasi kwa kifaa cha chuma, au kuyachonga juu ya mwamba milele!
25 わたしは知る、わたしをあがなう者は生きておられる、後の日に彼は必ず地の上に立たれる。
Ninajua kwamba Mkombozi wangu yu hai, naye kwamba mwishoni atasimama juu ya nchi.
26 わたしの皮がこのように滅ぼされたのち、わたしは肉を離れて神を見るであろう。
Nami baada ya ngozi yangu kuharibiwa, bado nikiwa na mwili huu nitamwona Mungu;
27 しかもわたしの味方として見るであろう。わたしの見る者はこれ以外のものではない。わたしの心はこれを望んでこがれる。
mimi nitamwona kwa macho yangu mwenyewe: mimi, wala si mwingine. Tazama jinsi moyo wangu unavyomtamani sana!
28 あなたがたがもし『われわれはどうして彼を責めようか』と言い、また『事の根源は彼のうちに見いだされる』と言うならば、
“Kama mkisema, ‘Tazama tutakavyomwinda, maadamu mzizi wa tatizo uko ndani yake,’
29 つるぎを恐れよ、怒りはつるぎの罰をきたらすからだ。これによって、あなたがたは、さばきのあることを知るであろう」。
ninyi wenyewe uogopeni upanga, kwa kuwa ghadhabu italeta adhabu kwa upanga, nanyi ndipo mtakapojua kwamba kuna hukumu.”

< ヨブ 記 19 >