< 創世記 10 >

1 ノアの子セム、ハム、ヤペテの系図は次のとおりである。洪水の後、彼らに子が生れた。
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya wana wa Nuhu, ambao ni, Shemu, Hamu, na Yafethi. Wana wa kiume walizaliwa kwao baada ya gharika.
2 ヤペテの子孫はゴメル、マゴグ、マダイ、ヤワン、トバル、メセク、テラスであった。
Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Masheki, na Tirasi.
3 ゴメルの子孫はアシケナズ、リパテ、トガルマ。
Na wana wa Gomeri walikuwa Ashikenazi, Rifathi na Togama.
4 ヤワンの子孫はエリシャ、タルシシ、キッテム、ドダニムであった。
Wana wa Yavani walikuwa Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Dodanimu.
5 これらから海沿いの地の国民が分れて、おのおのその土地におり、その言語にしたがい、その氏族にしたがって、その国々に住んだ。
Kutoka kwa hawa watu wa pwani waligawanyika na kwenda kwenye ardhi zao, kila mtu na lugha yake, kufuatana na koo zao, kwa mataifa yao.
6 ハムの子孫はクシ、ミツライム、プテ、カナンであった。
Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misraimu, Putu, na Kanaani.
7 クシの子孫はセバ、ハビラ、サブタ、ラアマ、サブテカであり、ラアマの子孫はシバとデダンであった。
Wana wa Kushi walikuwa Seba, Havila, Sabta, Raama, na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.
8 クシの子はニムロデであって、このニムロデは世の権力者となった最初の人である。
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikuwa hodari wa kwanza juu ya nchi.
9 彼は主の前に力ある狩猟者であった。これから「主の前に力ある狩猟者ニムロデのごとし」ということわざが起った。
Alikuwa mwindaji mkuu mbele ya Yahwe. Hii ndiyo sababu hunenwa, “Kama Nimrod mwindaji mkuu mbele za Yahwe.”
10 彼の国は最初シナルの地にあるバベル、エレク、アカデ、カルネであった。
Miji ya kwanza ya ufalme wake ilikuwa Babeli, Ereku, Akadi na Kalne, katika ichi ya Shinari.
11 彼はその地からアッスリヤに出て、ニネベ、レホボテイリ、カラ、
Kutoka katika nchi ile alikwenda Ashuru na akajenga Ninawi, Rehoboth- iri na Kala,
12 およびニネベとカラとの間にある大いなる町レセンを建てた。
na Raseni ambao ulikuwa kati ya Ninawi na Kala. Ulikuwa mji mkubwa.
13 ミツライムからルデ族、アナミ族、レハビ族、ナフト族、
Misraimu akazaa Waludi, Waanami, Walehabi, na Wanaftuhi,
14 パテロス族、カスル族、カフトリ族が出た。カフトリ族からペリシテ族が出た。
Wapathrusi na Wakasluhi ( ambao kwao Wafilisti walitokea), na Wakaftori.
15 カナンからその長子シドンが出て、またヘテが出た。
Kanaani akamzaa Sidono, mwanawe wa kwanza, na Hethi,
16 その他エブスびと、アモリびと、ギルガシびと、
pia na Myebusi, na Mwamori, Mgirgashi,
17 ヒビびと、アルキびと、セニびと、
Mhivi, Mwarki, Msini,
18 アルワデびと、ゼマリびと、ハマテびとが出た。後になってカナンびとの氏族がひろがった。
Mwarvadi, Msemari, na Mhamathi. Baadaye koo za wakanaani zikasambaa.
19 カナンびとの境はシドンからゲラルを経てガザに至り、ソドム、ゴモラ、アデマ、ゼボイムを経て、レシャに及んだ。
Mpaka wa Wakanaani ulianzia Sidoni, katika mwelekeo wa Gerari, hata Gaza, na kama kuelekea Sodoma, Gomora, Adma, na Seboimu hata Lasha.
20 これらはハムの子孫であって、その氏族とその言語とにしたがって、その土地と、その国々にいた。
Hawa walikuwa wana wa Ham, kwa koo zao, kwa lugha zao, katika ardhi zao na katika mataifa yao.
21 セムにも子が生れた。セムはエベルのすべての子孫の先祖であって、ヤペテの兄であった。
Pia walizaliwa wana kwa Shemu, ndugu yake mkubwa wa Yafethi. Shemu pia alikuwa baba yao na watu wote wa Eberi.
22 セムの子孫はエラム、アシュル、アルパクサデ、ルデ、アラムであった。
Wana wa Shemu walikuwa Elamu, Ashuru, Alfaksadi, Ludi, na Aramu.
23 アラムの子孫はウヅ、ホル、ゲテル、マシであった。
Wana wa Aramu walikuwa ni Usi, Huli, Getheri, na Mashi.
24 アルパクサデの子はシラ、シラの子はエベルである。
Arfaksadi akamzaa Sela, na Sela akamzaa Eber.
25 エベルにふたりの子が生れた。そのひとりの名をペレグといった。これは彼の代に地の民が分れたからである。その弟の名をヨクタンといった。
Eberi akazaa wana wawili wa kiume. Jina la mmoja aliitwa Pelegi maana katika siku zake nchi iligawanyika. Jina la ndugu yake aliitwa Yoktani.
26 ヨクタンにアルモダデ、シャレフ、ハザルマウテ、エラ、
Yoktani akamzaa Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 ハドラム、ウザル、デクラ、
Hadoram, Uzali, Dikla,
28 オバル、アビマエル、シバ、
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 オフル、ハビラ、ヨバブが生れた。これらは皆ヨクタンの子であった。
Ofiri, Havila, na Yobabi. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 彼らが住んだ所はメシャから東の山地セパルに及んだ。
Mpaka wao ulikuwa unaanzia Mesha, hadi Sefari, mlima wa mashariki.
31 これらはセムの子孫であって、その氏族とその言語とにしたがって、その土地と、その国々にいた。
Hawa walikuwa wana wa Shemu, kulingana na koo zao na lugha zao, katika ardhi zao kulingana na mataifa yao.
32 これらはノアの子らの氏族であって、血統にしたがって国々に住んでいたが、洪水の後、これらから地上の諸国民が分れたのである。
Hizi zilikuwa koo za wana wa Nuhu, kulingana na vizazi vyao, kwa mataifa yao. Kutokea kwa hawa mataifa yaligawanyika na kwenda juu ya nchi baada ya gharika.

< 創世記 10 >