< 詩篇 89 >
1 われヱホバの憐憫をとこしへにうたはん われ口もてヱホバの眞實をよろづ代につげしらせん
Utenzi wa Ethani Mwezrahi. Nitaimba juu ya upendo mkuu wa Bwana milele; kwa kinywa changu nitajulisha uaminifu wako ujulikane kwa vizazi vyote.
2 われいふ あはれみは永遠にたてらる 汝はその眞實をかたく天にさだめたまはんと
Nitatangaza kuwa upendo wako unasimama imara milele na uaminifu wako umeuthibitisha mbinguni.
3 われわが撰びたるものと契約をむすびわが僕ダビデにちかひたり
Ulisema, “Nimefanya agano na mteule wangu, nimemwapia mtumishi wangu Daudi,
4 われなんぢの裔をとこしへに固うしなんぢの座位をたてて代々におよばしめん (セラ)
‘Nitaimarisha uzao wako milele na kudumisha ufalme wako kwa vizazi vyote.’”
5 ヱホバよもろもろの天はなんぢの奇しき事跡をほめん なんぢの眞實もまた潔きものの會にてほめらるべし
Ee Bwana, mbingu zinayasifu maajabu yako, uaminifu wako pia katika kusanyiko la watakatifu.
6 蒼天にてたれかヱホバに類ふものあらんや 神の子のなかに誰かヱホバのごとき者あらんや
Kwa kuwa ni nani katika mbingu anayeweza kulinganishwa na Bwana? Ni nani miongoni mwa viumbe vya mbinguni aliye kama Bwana?
7 神はきよきものの公會のなかにて畏むべきものなり その四周にあるすべての者にまさりて懼るべきものなり
Katika kusanyiko la watakatifu, Mungu huogopwa sana, anahofiwa kuliko wote wanaomzunguka.
8 萬軍の神ヱホバよヤハよ汝のごとく大能あるものは誰ぞや なんぢの眞實はなんぢをめぐりたり
Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, ni nani aliye kama wewe? Ee Bwana, wewe ni mwenye nguvu, na uaminifu wako unakuzunguka.
9 なんぢ海のあるるををさめ その浪のたちあがらんときは之をしづめたまふなり
Wewe unatawala bahari yenye msukosuko; wakati mawimbi yake yanapoinuka, wewe unayatuliza.
10 なんぢラハブを殺されしもののごとく撃碎きおのれの仇どもを力ある腕をもて打散したまへり
Wewe ulimponda Rahabu kama mmojawapo wa waliochinjwa; kwa mkono wako wenye nguvu, uliwatawanya adui zako.
11 もろもろの天はなんぢのもの地もまた汝のものなり世界とその中にみつるものとはなんぢの基したまへるなり
Mbingu ni zako, nayo nchi pia ni yako, uliuwekea ulimwengu msingi pamoja na vyote vilivyomo.
12 北と南はなんぢ造りたまへり タボル、ヘルモンはなんぢの名によりて歓びよばふ
Uliumba kaskazini na kusini; Tabori na Hermoni wanaliimbia jina lako kwa furaha.
13 なんぢは大能のみうでをもちたまふ なんぢの手はつよく汝のみぎの手はたかし
Mkono wako umejaa uwezo; mkono wako una nguvu, mkono wako wa kuume umetukuzwa.
14 義と公平はなんぢの寳座のもとゐなり あはれみと眞實とは聖顔のまへにあらはれゆく
Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako cha enzi; upendo na uaminifu vinakutangulia.
15 よろこびの音をしる民はさいはひなり ヱホバよかれらはみかほの光のなかをあゆめり
Heri ni wale ambao wamejifunza kukusifu kwa shangwe, wanaotembea katika mwanga wa uwepo wako, Ee Bwana.
16 かれらは名によりて終日よろこび 汝の義によりて高くあげられたり
Wanashangilia katika jina lako mchana kutwa, wanafurahi katika haki yako.
17 かれらの力の榮光はなんぢなり 汝の惠によりてわれらの角はたかくあげられん
Kwa kuwa wewe ni utukufu na nguvu yao, kwa wema wako unatukuza pembe yetu.
18 そはわれらの盾はヱホバに屬われらの王はイスラエルの聖者につけり
Naam, ngao yetu ni mali ya Bwana, na mfalme wetu mali ya Aliye Mtakatifu wa Israeli.
19 そのとき異象をもてなんぢの聖徒につげたまはく われ佑助をちからあるものに委ねたり わが民のなかより一人をえらびて高くあげたり
Ulizungumza wakati fulani katika maono, kwa watu wako waaminifu, ukasema: “Nimeweka nguvu kwa shujaa, nimemwinua kijana miongoni mwa watu.
20 われわが僕ダビデをえて之にわが聖膏をそそげり
Nimemwona Daudi, mtumishi wangu, na nimemtia mafuta yangu matakatifu.
21 わが手はかれとともに堅くわが臂はかれを強くせん
Kitanga changu kitamtegemeza, hakika mkono wangu utamtia nguvu.
22 仇かれをしへたぐることなし惡の子かれを苦しむることなからん
Hakuna adui atakayemtoza ushuru, hakuna mtu mwovu atakayemwonea.
23 われかれの前にそのもろもろの敵をたふし彼をにくめるものを撃ん
Nitawaponda adui zake mbele zake na kuwaangamiza watesi wake.
24 されどわが眞實とわが憐憫とはダビデとともに居り わが名によりてその角はたかくあげられん
Upendo wangu mkamilifu utakuwa pamoja naye, kwa Jina langu pembe yake itatukuzwa.
25 われ亦かれの手を海のうへにおき そのみぎの手を河のうへにおかん
Nitauweka mkono wake juu ya bahari, mkono wake wa kuume juu ya mito.
26 ダビデ我にむかひて汝はわが父わが神わがすくひの岩なりとよばん
Naye ataniita kwa sauti, ‘Wewe ni Baba yangu, Mungu wangu, Mwamba na Mwokozi wangu.’
27 われまた彼をわが初子となし地の王たちのうち最もたかき者となさん
Nitamteua pia awe mzaliwa wangu wa kwanza, aliyetukuka kuliko wafalme wote wa dunia.
28 われとこしへに憐憫をかれがためにたもち 之とたてし契約はかはることなかるべし
Nitadumisha upendo wangu kwake milele, na agano langu naye litakuwa imara.
29 われまたその裔をとこしへに存へ そのくらゐを天の日數のごとくながらへしめん
Nitaudumisha uzao wake milele, kiti chake cha enzi kama mbingu zinavyodumu.
30 もしその子わが法をはなれ わが審判にしたがひて歩まず
“Kama wanae wataacha amri yangu na wasifuate sheria zangu,
kama wakihalifu maagizo yangu na kutoshika amri zangu,
32 われ杖をもてかれらの愆をただし鞭をもてその邪曲をただすべし
nitaadhibu dhambi yao kwa fimbo, uovu wao kwa kuwapiga,
33 されど彼よりわが憐憫をことごとくはとりさらず わが眞實をおとろへしむることなからん
lakini sitauondoa upendo wangu kwake, wala sitausaliti uaminifu wangu kamwe.
34 われおのれの契約をやぶらず己のくちびるより出しことをかへじ
Mimi sitavunja agano langu wala sitabadili lile ambalo midomo yangu imelitamka.
35 われ曩にわが聖をさして誓へり われダビデに虚偽をいはじ
Mara moja na kwa milele, nimeapa kwa utakatifu wangu, nami sitamdanganya Daudi:
36 その裔はとこしへにつづきその座位は日のごとく恒にわが前にあらん
kwamba uzao wake utaendelea milele, na kiti chake cha enzi kitadumu mbele zangu kama jua;
37 また月のごとく永遠にたてられん空にある證人はまことなり (セラ)
kitaimarishwa milele kama mwezi, shahidi mwaminifu angani.”
38 されどその受膏者をとほざけて棄たまへり なんぢ之をいきどほりたまへり
Lakini wewe umemkataa, umemdharau, umemkasirikia sana mpakwa mafuta wako.
39 なんぢ己がしもべの契約をいみ 其かんむりをけがして地にまでおとし給へり
Umelikana agano lako na mtumishi wako, na umeinajisi taji yake mavumbini.
40 またその垣をことごとく倒し その保砦をあれすたれしめたまへり
Umebomoa kuta zake zote, na ngome zake zote umezifanya kuwa magofu.
41 その道をすぐるすべての者にかすめられ隣人にののしらる
Wote wapitao karibu wamemnyangʼanya mali zake; amekuwa dharau kwa jirani zake.
42 なんぢかれが敵のみぎの手をたかく擧そのもろもろの仇をよろこばしめたまへり
Umeutukuza mkono wa kuume wa adui zake, umewafanya watesi wake wote washangilie.
43 なんぢかれの劍の刃をふりかへして戰闘にたつに堪へざらしめたまひき
Umegeuza makali ya upanga wake, na hukumpa msaada katika vita.
Umeikomesha fahari yake, na kukiangusha kiti chake cha enzi.
45 その年若き日をちぢめ恥をそのうへに覆たまへり (セラ)
Umezifupisha siku za ujana wake, umemfunika kwa vazi la aibu.
46 ヱホバよかくて幾何時をへたまふや自己をとこしへに隠したまふや忿怒は火のもゆるごとくなるべきか
Hata lini, Ee Bwana? Utajificha milele? Ghadhabu yako itawaka kama moto hata lini?
47 ねがはくはわが時のいかに短かきかを思ひたまへ 汝いたづらにすべての人の子をつくりたまはんや
Kumbuka jinsi maisha yangu yanavyopita haraka. Ni kwa ubatili kiasi gani umemuumba mwanadamu!
48 誰かいきて死をみず又おのがたましひを陰府より救ひうるものあらんや (セラ) (Sheol )
Ni mtu gani awezaye kuishi na asione kifo, au kujiokoa mwenyewe kutoka nguvu za kaburi? (Sheol )
49 主よなんぢが眞實をもてダビデに誓ひたまへる昔日のあはれみはいづこにありや
Ee Bwana, uko wapi upendo wako mkuu wa mwanzoni, ambao katika uaminifu wako ulimwapia Daudi?
50 主よねがはくはなんぢの僕のうくる謗をみこころにとめたまへ ヱホバよ汝のもろもろの仇はわれをそしりなんぢの受膏者のあしあとをそしれり 我もろもろの民のそしりをわが懐中にいだく
Bwana kumbuka jinsi mtumishi wako amesimangwa, jinsi ninavyovumilia moyoni mwangu dhihaka za mataifa yote,
51 主よねがはくはなんぢの僕のうくる謗をみこころにとめたまへ ヱホバよ汝のもろもろの仇はわれをそしりなんぢの受膏者のあしあとをそしれり 我もろもろの民のそしりをわが懐中にいだく
dhihaka ambazo kwazo adui zako wamenisimanga, Ee Bwana, ambazo kwazo wamesimanga kila hatua ya mpakwa mafuta wako.
52 ヱホバは永遠にほむべきかな アーメン アーメン
Msifuni Bwana milele!