< 詩篇 73 >
1 神はイスラエルにむかひ心のきよきものに對ひてまことに惠あり
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 然はあれどわれはわが足つまづくばかりわが歩すべるばかりにてありき
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 こはわれ惡きものの榮ゆるを見てその誇れる者をねたみしによる
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 かれらは死るに苦しみなくそのちからは反てかたし
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5 かれらは人のごとく憂にをらず人のごとく患難にあふことなし
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 このゆゑに傲慢は妝飾のごとくその頸をめぐり強暴はころものごとく彼等をおほへり
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7 かれら肥ふとりてその目とびいで心の欲にまさりて物をうるなり
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8 また嘲笑をなし惡をもて暴虐のことばをいだし高ぶりてものいふ
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10 このゆゑにかれの民はここにかへり水のみちたる杯をしぼりいだして
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11 いへらく神いかで知たまはんや至上者に知識あらんやと
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12 視よかれらは惡きものなるに常にやすらかにしてその富ましくははれり
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
13 誠に我はいたづらに心をきよめ罪ををかさずして手をあらひたり
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14 そはわれ終日なやみにあひ朝ごとに責をうけしなり
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15 われもし斯ることを述んといひしならば我なんぢが子輩の代をあやまらせしならん
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16 われこれらの道理をしらんとして思ひめぐらししにわが眼いたく痛たり
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17 われ神の聖所にゆきてかれらの結局をふかく思へるまでは然りき
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18 誠になんぢはかれらを滑かなるところにおきかれらを滅亡におとしいれ給ふ
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19 かれらは瞬間にやぶれたるかな彼等は恐怖をもてことごとく滅びたり
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20 主よなんぢ目をさましてかれらが像をかろしめたまはんときは夢みし人の目さめたるがごとし
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22 われおろかにして知覺なし聖前にありて獣にひとしかりき
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23 されど我つねになんぢとともにあり汝わが右手をたもちたまへり
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24 なんぢその訓諭をもて我をみちびき後またわれをうけて榮光のうちに入たまはん
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25 汝のほかに我たれをか天にもたん地にはなんぢの他にわが慕ふものなし
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26 わが身とわが心とはおとろふ されど神はわがこころの磐わがとこしへの嗣業なり
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27 視よなんぢに遠きものは滅びん 汝をはなれて姦淫をおこなふ者はみななんぢ之をほろぼしたまひたり
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 神にちかづき奉るは我によきことなり われは主ヱホバを避所としてそのもろもろの事跡をのべつたへん
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.