< 詩篇 71 >
1 ヱホバよ我なんぢに依賴む ねがはくは何の日までも恥うくることなからしめ給へ
Katika wewe, Yahwe, napatakimbilio salama; usiniache niaibishwe.
2 なんぢの義をもて我をたすけ我をまぬかれしめたまへ なんぢの耳をわれに傾けて我をすくひたまへ
Uniokoe na kunifanya salama katika haki yako; geuzia sikio lako kwangu.
3 ねがはくは汝わがすまひの磐となりたまへ われ恒にそのところに往ことを得ん なんぢ我をすくはんとて勅命をいだしたまへり そは汝はわが磐わが城なり
Uwe kwagu mwamba kwa ajili ya kimbilio salama ambako naweza kwenda siku zote; wewe umeamuru kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
4 わが神よあしきものの手より不義殘忍なる人のてより 我をまぬかれしめたまへ
Uniokoe mimi, Mungu wangu, kutoka katika mkono wa asiye haki na katili.
5 主ヱホバよなんぢはわが望なり わが幼少よりの恃なり
Maana wewe ni tumaini langu, Bwana Yahwe. Nimekuamini wewe siku zote tangu nilipokuwa mtoto.
6 われ胎をはなるるより汝にまもられ母の腹にありしときより汝にめぐまれたり 我つねに汝をほめたたへん
Nimekuwa nikisaidiwa na wewe tangu tumboni; wewe ndiye yule uliyenitoa tumboni mwa mama yangu; sifa zangu zitakuhusu wewe siku zote.
7 我おほくの人にあやしまるるごとき者となれり 然どなんぢはわが堅固なる避所なり
Mimi ni mfano bora kwa watu wangu; wewe ni kimbilio langu lenye nguvu.
8 なんぢの頌辭となんぢの頌美とは終日わが口にみちん
Mama yangu atajawa na sifa zako, siku zote akikuheshimu.
9 わが年老ぬるとき我をすてたまふなかれ わが力おとろふるとき我をはなれたまなかれ
Usinitupe katika siku za miaka ya uzee wangu; usiniache wakati nguvu zangu zitakapoisha.
10 わが仇はわがことを論ひ ひわが霊魂をうかがふ者はたがひに議ていふ
Maana adui zangu wanazungumza kuhusu mimi; wale wanao fatilia uhai wangu wanapanga njama pamoja.
11 神かれを離れたり彼をたすくる者なし かれを追てとらへよと
Wao husema, “Mungu amemuacha; mfuateni na mumchukue, maana hakuna yeyote awezaye kumuokoa yeye.”
12 神よわれに遠ざかりたまふなかれ わが神よとく來りて我をたすけたまへ
Mungu, usiwe mbali nami; Mungu wangu, harakisha kunisaidia mimi.
13 わがたましひの敵ははぢ且おとろへ我をそこなはんとするものは謗と辱とにおほはれよ
Waaibishwe na kuharibiwa, wale walio adui wa uhai wangu; wavishwe laumu na kudharauliwa, wale watafutao kuniumiza.
14 されど我はたえず望をいだきていやますます汝をほめたたへん
Lakini nitakutumainia wewe siku zote na nitakusifu wewe zaidi na zaidi.
15 わが口はひねもす汝の義となんぢの救とをかたらん われその數をしらざればなり
Kinywa changu kitaongea kuhusu haki yako na wokovu wako mchana kutwa, ingawa ziwezi kuzielewa maana ni nyingi mno.
16 われは主ヱホバの大能の事跡をたづさへゆかん われは只なんぢの義のみをかたらん
Nitakuja na matendo yenye nguvu ya Bwana Yahwe; nitataja haki yako, yako pekee.
17 神よなんぢわれを幼少より敎へたまへり われ今にいたるまで汝のくすしき事跡をのべつたへたり
Mungu, tangu ujana wangu wewe umenifundisha; hata sasa ninatangaza matendo yako ya ajabu.
18 神よねがはくはわれ老て頭髮しろくなるとも我がなんぢの力を次代にのべつたへ なんぢの大能を世にうまれいづる凡のものに宣傳ふるまで我をはなれ給ふなかれ
Hakika, hata niwapo mzee na mvi kichwani, Mungu, usiniache mimi, kama ambavyo nimekuwa nikitanga nguvu yako kwa vizazi vijavyo, na uweza wako kwa yeyote ajaye.
19 神よなんぢの義もまた甚たかし なんぢは大なることをなしたまへり 神よたれか汝にひとしき者あらんや
Pia haki yako, Mungu, iko juu sana; wewe ambaye umefanya mambo makuu, Mungu, ni nani aliye kama wewe?
20 汝われらを多のおもき苦難にあはせたまへり なんぢ再びわれらを活しわれらを地の深所よりあげたまはん
Wewe ambaye umetuonesha sisi mateso mengi utatuhuisha tena na utatupandisha tena juu kutoka kwenye kina cha nchi.
21 ねがはくは我をいよいよ大ならしめ歸りきたりて我をなぐさめ給へ
Uiongeze heshima yangu; rudi tena na unifariji.
22 わが神よさらばわれ筝をもて汝をほめ なんぢの眞實をほめたたへん イスラエルの聖者よわれ琴をもてなんぢを讃うたはん
Nami pia nitakushukuru kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako, Mungu wangu; kwako nitaimba sifa kwa kinubi, Mtakatifu wa Israel.
23 われ聖前にうたときわが口唇よろこびなんぢの贖ひたまへるわが霊魂おほいに喜ばん
Midomo yangu itapiga kelele kwa sababu ya furaha wakati nikikuimbia sifa, hata kwa roho yangu, ambayo wewe umeikomboa.
24 わが舌もまた終日なんぢの義をかたらん われを害はんとするもの愧惶つればなり
Ulimi wangu pia utaongea kuhusu haki yangu mchana kutwa; maana wameaibishwa na kuvurugwa, wale waliotafuta kuniumiza.