< 詩篇 50 >

1 ぜんのうの神ヱホバ詔命して日のいづるところより日のいるところまであまねく地をよびたまへり
Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
2 かみは美麗の極なるシオンより光をはなちたまへり
Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
3 われらの神はきたりて默したまはじ火その前にものをやきつくし暴風その四周にふきあれん
Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
4 神はその民をさばかんとて上なる天および地をよびたまへり
Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
5 いはく祭物をもて我とけいやくをたてしわが聖徒をわがもとに集めよと
“Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
6 もろもろの天は神の義をあらはせり 神はみづから審士たればなり (セラ)
Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
7 わが民よきけ我ものいはんイスラエルよきけ我なんぢにむかひて證をなさん われは神なんぢの神なり
“Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
8 わがなんぢを責るは祭物のゆゑにあらず なんぢの燔祭はつねにわが前にあり
Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
9 我はなんぢの家より牡牛をとらず なんぢの牢より牡山羊をとらず
Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
10 林のもろもろのけもの山のうへの千々の牲畜はみなわが有なり
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
11 われは山のすべての鳥をしる 野のたけき獣はみなわがものなり
Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
12 世界とそのなかに充るものとはわが有なれば縦ひわれ饑るともなんぢに告じ
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
13 われいかで牡牛の肉をくらひ牡山羊の血をのまんや
Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
14 感謝のそなへものを神にささげよ なんぢのちかひを至上者につくのへ
Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
15 なやみの日にわれをよべ我なんぢを援けん而してなんぢ我をあがむべし
na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
16 然はあれど神あしきものに言給く なんぢは敎をにくみ わが言をその後にすつるものなるに何のかかはりありてわが律法をのべ わがけいやくを口にとりしや
Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
17 然はあれど神あしきものに言給く なんぢは敎をにくみ わが言をその後にすつるものなるに何のかかはりありてわが律法をのべ わがけいやくを口にとりしや
Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
18 なんぢ盗人をみれば之をよしとし姦淫をおこなふものの伴侶となれり
Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
19 なんぢその口を惡にわたす なんぢの舌は詭計をくみなせり
Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
20 なんぢ坐りて兄弟をそしり己がははの子を誣ののしれり
Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
21 汝これらの事をなししをわれ默しぬれば なんぢ我をおのれに恰にたるものとおもへり されど我なんぢを責めてその罪をなんぢの目前につらぬべし
Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
22 神をわするるものよ今このことを念へ おそらくは我なんぢを抓さかんとき助るものあらじ
“Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
23 感謝のそなへものを献るものは我をあがむ おのれの行爲をつつしむ者にはわれ神の救をあらはさん
Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”

< 詩篇 50 >