< 詩篇 48 >

1 ヱホバは大なり われらの神の都そのきよき山のうへにて甚くほめたたへられたまふべし
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
2 シオンの山はきたの端たかくしてうるはしく喜悦を地にあまねくあたふ ここは大なる王のみやこなり
Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
3 そのもろもろの殿のうちに神はおのれをたかき櫓としてあらはしたまへり
Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
4 みよ王等はつどひあつまりて偕にすぎゆきぬ
Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
5 かれらは都をみてあやしみ且おそれて忽ちのがれされり
walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
6 戰慄はかれらにのぞみ その苦痛は子をうまんとする婦のごとし
Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
7 なんぢは東風をおこしてタルシシの舟をやぶりたまふ
Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
8 曩にわれらが聞しごとく今われらは萬軍のヱホバの都われらの神のみやこにて之をみることをえたり 神はこの都をとこしへまで固くしたまはん (セラ)
Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
9 神よ我らはなんぢの宮のうちにて仁慈をおもへり
Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
10 神よなんぢの譽はその名のごとく地の極にまでおよべり なんぢの右手はただしきにて充り
Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
11 なんぢのもろもろの審判によりてシオンの山はよろこびユダの女輩はたのしむべし
Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
12 シオンの周圍をありき徧くめぐりてその櫓をかぞへよ
Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
13 その石垣に目をとめよ そのもろもろの殿をみよ なんぢらこれを後代にかたりつたへんが爲なり
yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
14 そはこの神はいや遠長にわれらの神にましましてわれらを死るまでみちびきたまはん
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.

< 詩篇 48 >