< 詩篇 36 >
1 あしきものの愆はわが心のうちにかたりて その目のまへに神をおそるるの畏あることなしといふ
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
2 かれはおのが邪曲のあらはるることなく憎まるることなからんとて自からその目にて謟る
Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
3 その口のことばは邪曲と虚偽となり智をこばみ善をおこなふことを息たり
Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
4 かつその寝床にてよこしまなる事をはかり よからぬ途にたちとまりて惡をきらはず
Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
5 ヱホバよなんぢの仁慈は天にあり なんぢの眞實は雲にまでおよぶ
Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
6 汝のただしきは神の山のごとく なんぢの審判はおほいなる淵なり ヱホバよなんぢは人とけものとを護りたまふ
Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
7 神よなんぢの仁慈はたふときかな 人の子はなんぢの翼の蔭にさけどころを得
Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
8 なんぢの屋のゆたかなるによりてことごとく飽ことをえん なんぢはその歓樂のかはの水をかれらに飮しめたまはん
Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
9 そはいのちの泉はなんぢに在り われらはなんぢの光によりて光をみん
Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
10 ねがはくはなんぢを知るものにたえず憐憫をほどこし心なほき者にたえず正義をほどこしたまへ
Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
11 たかぶるものの足われをふみ惡きものの手われを逐去ふをゆるし給ふなかれ
Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
12 邪曲をおこなふ者はかしこに仆れたり かれら打伏られてまた起ことあたはざるべし
Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!