< 詩篇 25 >
Zaburi ya Daudi. Kwako wewe, Ee Bwana, nainua nafsi yangu,
2 わが神よわれなんぢに依賴めり ねがはくはわれに愧をおはしめたまふなかれ わが仇のわれに勝誇ることなからしめたまへ
ni wewe ninayekutumainia, Ee Mungu wangu. Usiniache niaibike, wala usiache adui zangu wakanishinda.
3 實になんぢを俟望むものははぢしめられず 故なくして信をうしなふものは愧をうけん
Kamwe hakuna hata mmoja anayekutegemea atakayeaibishwa, bali wataaibishwa wafanyao hila bila sababu.
4 ヱホバよなんぢの大路をわれにしめし なんぢの徑をわれにをしへたまへ
Nionyeshe njia zako, Ee Bwana, nifundishe mapito yako,
5 我をなんぢの眞理にみちびき我ををしへたまへ 汝はわがすくひの神なり われ終日なんぢを俟望む
niongoze katika kweli yako na kunifundisha, kwa maana wewe ni Mungu Mwokozi wangu, nalo tumaini langu liko kwako wakati wote.
6 なんぢのあはれみと仁慈とはいにしへより絶ずあり ヱホバよこれを思ひいだしたまへ
Kumbuka, Ee Bwana, rehema zako kuu na upendo, kwa maana zimekuwepo tangu zamani.
7 わがわかきときの罪とわが愆とはおもひいでたまふなかれ ヱホバよ汝のめぐみの故になんぢの仁慈にしたがひて我をおもひいでたまへ
Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala njia zangu za uasi, sawasawa na upendo wako unikumbuke, kwa maana wewe ni mwema, Ee Bwana.
8 ヱホバはめぐみ深くして直くましませり 斯るがゆゑに道をつみびとにをしへ
Bwana ni mwema na mwenye adili, kwa hiyo huwafundisha wenye dhambi njia zake.
9 謙だるものを正義にみちびきたまはん その道をへりくだる者にしめしたまはん
Huwaongoza wanyenyekevu katika haki, naye huwafundisha njia yake.
10 ヱホバのもろもろの道はそのけいやくと證詞とをまもるものには仁慈なり眞理なり
Njia zote za Bwana ni za upendo na uaminifu kwa wale wanaoshika shuhuda za agano lake.
11 わが不義はおほいなり ヱホバよ名のために之をゆるしたまへ
Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, unisamehe uovu wangu, ijapokuwa ni mwingi.
12 ヱホバをおそるる者はたれなるか 之にそのえらぶべき道をしめしたまはん
Ni nani basi, mtu yule anayemcha Bwana? Atamfundisha katika njia atakayoichagua kwa ajili yake.
13 かかる人のたましひは平安にすまひ その裔はくにをつぐべし
Mtu huyo atafanikiwa maishani mwake, nao wazao wake watairithi nchi.
14 ヱホバの親愛はヱホバをおそるる者とともにあり ヱホバはその契約をかれらに示したまはん
Siri ya Bwana iko kwa wale wamchao, yeye huwajulisha agano lake.
15 わが目はつねにヱホバにむかふ ヱホバわがあしを網よりとりいだしたまふ可ればなり
Macho yangu humwelekea Bwana daima, kwa kuwa yeye peke yake ndiye ataitoa miguu yangu kutoka mtego.
16 ねがはくは歸りきたりて我をあはれみたまへ われ獨わびしくまた苦しみをるなり
Nigeukie na unihurumie, kwa maana mimi ni mpweke na mwenye kuteseka.
17 願くはわが心のうれへをゆるめ我をわざはひより脱かれしめたまへ
Shida za moyo wangu zimeongezeka, niokoe katika dhiki yangu.
18 わが患難わが辛苦をかへりみ わがすべての罪をゆるしたまへ
Uangalie mateso na shida zangu na uniondolee dhambi zangu zote.
19 わが仇をみたまへ かれらの數はおほし情なき憾をもてわれをにくめり
Tazama adui zangu walivyo wengi, pia uone jinsi wanavyonichukia vikali!
20 わがたましひをまもり我をたすけたまへ われに愧をおはしめたまふなかれ 我なんぢに依賴めばなり
Uyalinde maisha yangu na uniokoe, usiniache niaibike, kwa maana nimekukimbilia wewe.
21 われなんぢを挨望むねがはくは完全と正直とわれをまもれかし
Uadilifu na uaminifu vinilinde, kwa sababu tumaini langu ni kwako.
22 神よすべての憂よりイスラエルを贖ひいだしたまへ
Ee Mungu, wakomboe Israeli, katika shida zao zote!