< 詩篇 149 >

1 ヱホバをほめたたへよ ヱホバに對ひてあたらしき歌をうたへ 聖徒のつどひにてヱホバの頌美をうたへ
Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
2 イスラエルはおのれを造りたまひしものをよろこび シオンの子輩は己が王のゆゑによりて樂しむべし
Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
3 かれらをどりつつその聖名をほめたたへ 琴鼓にてヱホバをほめうたべし
Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
4 ヱホバはおのが民をよろこび 救にて柔和なるものを美しくしたまへばなり
Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
5 聖徒はえいくわうの故によりてよろこび その寝牀にてよろこびうたふべし
Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
6 その口に神をほむるうたあり その手にもろはの劍あり
Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
7 こはもろもろの國に仇をかへし もろもろの民をつみなひ
ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
8 かれらの王たちを鏈にてかれらの貴人をくろかねの械にていましめ
wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
9 録したる審判をかれらに行ふべきためなり 斯るほまれはそのもろもろの聖徒にあり ヱホバをほめたたへよ
ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.

< 詩篇 149 >