< 詩篇 118 >
1 ヱホバに感謝せよヱホバは恩惠ふかくその憐憫とこしへに絶ることなし
Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 イスラエルは率いふべし その憐憫はとこしへにたゆることなしと
Israeli na aseme, “Uaminifu wa agano lake wadumu milele.”
3 アロンの家はいざ言ふべし そのあはれみは永遠にたゆることなしと
Nyumba ya Haruni na iseme, “Uaminifu wa agano lake wadumu milele.”
4 ヱホバを畏るるものは率いふべし その憐憫はとこしへにたゆることなしと
Wafuasi waaminifu wa Yahwe na waseme, “Uaminifu wa agano lake wadumu milele.”
5 われ患難のなかよりヱホバをよべば ヱホバこたへて我をひろき處におきたまへり
Katika dhiki yangu nilimuita Yahwe; Yahwe alinijibu na kuniweka huru.
6 ヱホバわが方にいませばわれにおそれなし 人われに何をなしえんや
Yahwe yuko pamoja nami; sitaogopa; mwanadamu atanifanya nini? Yahwe yuko upande wangu kama msaidizi;
7 ヱホバはわれを助くるものとともに我がかたに坐す この故にわれを憎むものにつきての願望をわれ見ることをえん
nitawatazama kwa ushindi wale walio nichukia.
Ni bora kuwa na makazi katika Yahwe kuliko kumtumainia mwanadamu.
9 ヱホバによりたのむはもろもろの侯にたよるよりも勝りてよし
Ni bora kukimbilia katika Yahwe kuliko kuamini katika wakuu.
10 もろもろの國はわれを圍めり われヱホバの名によりて彼等をほろぼさん
Mataifa yote walinizunguka; kwa jina la Yahwe niliwakatilia mbali.
11 かれらは我をかこめり我をかこめりヱホバの名によりて彼等をほろぼさん
Walinizunguka; naam, walinizunguka; kwa jina la Yahwe niliwakatilia mbali.
12 かれらは蜂のごとく我をかこめり かれらは荊の火のごとく消たり われはヱホバの名によりてかれらを滅さん
Walinizunguka kama nyuki; walitoweka haraka kama moto kati ya miiba; kwa jina la Yahwe niliwakatilia mbali.
13 汝われを倒さんとしていたく剌つれど ヱホバわれを助けたまへり
Walinishambulia ili waniangushe, lakini Yahwe alinisaidia.
14 ヱホバはわが力わが歌にしてわが救となりたまへり
Yahwe ni nguvu yangu na furaha yangu, na ndiye anaye niokoa.
15 歓喜とすくひとの聲はただしきものの幕屋にあり ヱホバのみぎの手はいさましき動作をなしたまふ
Kelele za ushindi zimesikika katika maskani ya wenye haki; mkono wa kuume wa Mungu umeshinda.
16 ヱホバのみぎの手はたかくあがりヱホバの右の手はいさましき動作をなしたまふ
Mkono wa kuume wa Mungu umetukuka; mkono wa kuume wa Yahwe umeshinda.
17 われは死ることなからん 存へてヤハの事跡をいひあらはさん
Sitakufa, bali nitaishi na kuyatangaza matendo ya Yahwe.
18 ヤハはいたく我をこらしたまひしかど死には付したまはざりき
Yahwe ameniadhibu vikali; lakini hajaruhusu nife.
19 わがために義の門をひらけ 我そのうちにいりてヤハに感謝せん
Unifungulie milango ya haki; nitaingia na nitamshukuru Yahwe.
20 こはヱホバの門なりただしきものはその内にいるべし
Hili ni lango la Yahwe; wenye haki hupitia kwalo.
21 われ汝に感謝せん なんぢ我にこたへてわが救となりたまへばなり
Nitakushukuru wewe, kwa kuwa ulinijibu, na umekuwa wokovu wangu.
Jiwe ambalo wajenzi walilikataa wajenzi limekuwa msingi.
23 これヱホバの成たまへる事にしてわれらの目にあやしとする所なり
Yahwe ndiye afanyaye hili; ni la ajabu machoni petu.
24 これヱホバの設けたまへる日なり われらはこの日によろこびたのしまん
Hii ni siku ambayo Yahwe ametenda; tutaifurahia na kuishangilia.
25 ヱホバよねがはくはわれらを今すくひたまへ ヱホバよねがはくは我儕をいま榮えしめたまヘ
Tafadhali, Yahwe, utupe ushindi! Tafadhali, Yahwe, utupe mafanikio!
26 ヱホバの名によりて來るものは福ひなり われらヱホバの家よりなんぢらを祝せり
Amebarikiwa yule ajaye katika jina la Yahwe; tunakubariki kutoka katika nyumba ya Yahwe.
27 ヱホバは神なり われらに光をあたへたまへり 繩をもて祭壇の角にいけにへをつなげ
Yahwe ni Mungu, na ametupa sisi nuru; ifungeni dhabihu kwa kamba pembeni mwa madhabahu.
28 なんぢはわが神なり我なんぢに感謝せん なんぢはわが神なり我なんぢを崇めまつらん
Wewe ni Mungu wangu, nami nitakushukuru; wewe ni Mungu wangu; nitakutukuza wewe.
29 ヱホバにかんしやせよ ヱホバは恩惠ふかくその憐憫とこしへに絶ることなし
Oh, mshukuruni Yahwe; kwa kuwa ni mwema; kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.