< 箴言 知恵の泉 26 >

1 榮譽の愚なる者に適はざるは夏の時に雪ふり 穡收の時に雨ふるがごとし
Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
2 故なき詛は雀の翔り燕の飛ぶが如くにきたるものにあらず
Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
3 馬の爲には策あり 驢馬の爲には銜あり 愚なる者の背のために杖あり
Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
4 愚なる者の痴にしたがひて答ふること勿れ 恐くはおのれも是と同じからん
Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
5 愚なる者の痴にしたがひて之に答へよ 恐くは彼おのれの目に自らを智者と見ん
Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
6 愚なる者に托して事を言おくる者はおのれの足をきり身に害をうく
Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
7 跛者の足は用なし 愚なる者の口の箴もかくのごとし
Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
8 榮譽を愚なる者に與ふるは石を投石索に繋ぐが如し
Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
9 愚なる者の口にたもつ箴言は酔へるものの刺ある杖を手にて擧ぐるがごとし
Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
10 愚なる者を傭ひ流浪者を傭ふ者は すべての人を傷くる射手の如し
Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
11 狗のかへり來りてその吐たる物を食ふがごとく 愚なる者は重ねてその痴なる事をおこなふ
Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
12 汝おのれの目に自らを智慧ある者とする人を見るか 彼よりも却て愚なる人に望あり
Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
13 惰者は途に獅あり 衢に獅ありといふ
Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
14 戸の蝶鉸によりて轉るごとく惰者はその牀に輾轉す
Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
15 惰者はその手を盤にいるるも之をその口に擧ることを厭ふ
Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
16 惰者はおのれの目に自らを善く答ふる七人の者よりも智慧ありとなす
Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
17 路をよぎり自己に關りなき爭擾にたづさはる者は狗の耳をとらふる者のごとし
Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
18 旣にその鄰を欺くことをなして我はただ戯れしのみといふ者は 火箭または鎗または死を擲つ狂人のごとし
Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
19 旣にその鄰を欺くことをなして我はただ戯れしのみといふ者は 火箭または鎗または死を擲つ狂人のごとし
ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
20 薪なければ火はきえ 人の是非をいふ者なければ爭端はやむ
Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
21 煨火に炭をつぎ火に薪をくぶるがごとく爭論を好む人は爭論を起す
Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
22 人の是非をいふものの言はたはぶれのごとしと雖もかへつて腹の奧に入る
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
23 温かき口唇をもちて惡き心あるは銀の滓をきせたる瓦片のごとし
Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
24 恨むる者は口唇をもて自ら飾れども 心の衷には虚偽をいだく
Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
25 彼その聲を和らかにするとも之を信ずるなかれ その心に七の憎むべき者あればなり
Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
26 たとひ虚偽をもてその恨をかくすとも その惡は會集の中に顯はる
Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
27 坑を掘るものは自ら之に陷らん 石を轉ばしあぐる者の上にはその石まろびかへらん
Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
28 虚偽の舌はおのれの害す者を憎み 諂ふ口は滅亡をきたらす
Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.

< 箴言 知恵の泉 26 >