< 箴言 知恵の泉 20 >

1 酒は人をして嘲らせ 濃酒は人をして騒がしむ 之に迷はさるる者は無智なり
Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi; yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.
2 王の震怒は獅の吼るがごとし 彼を怒らする者は自己のいのちを害ふ
Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; yeye amkasirishaye hupoteza uhai wake.
3 穩かに居りて爭はざるは人の榮譽なりすべて愚なる者は怒り爭ふ
Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi, bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.
4 惰者は寒ければとて耕さず この故に収穫のときにおよびて求るとも得るところなし
Mvivu halimi kwa majira; kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama lakini hapati chochote.
5 人の心にある謀計は深き井の水のごとし 然れど哲人はこれを汲出す
Makusudi ya moyo wa mwanadamu ni maji yenye kina, lakini mtu mwenye ufahamu huyachota.
6 凡そ人は各自おのれの善を誇る されど誰か忠信なる者に遇しぞ
Watu wengi hujidai kuwa na upendo usiokoma, bali mtu mwaminifu ni nani awezaye kumpata?
7 身を正しくして歩履む義人はその後の子孫に福祉あるべし
Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama, wamebarikiwa watoto wake baada yake.
8 審判の位に坐する王はその目をもてすべての惡を散す
Wakati mfalme aketipo katika kiti chake cha enzi kuhukumu, hupepeta ubaya wote kwa macho yake.
9 たれか我わが心をきよめ わが罪を潔められたりといひ得るや
Ni nani awezaye kusema, “Nimeuweka moyo wangu safi; mimi ni safi na sina dhambi?”
10 二種の權衡二種の斗量は等しくヱホバに憎まる
Mawe ya kupimia yaliyo tofauti na vipimo tofauti, Bwana huchukia vyote viwili.
11 幼子といへどもその動作によりておのれの根性の清きか或は正しきかをあらはす
Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake, kama tabia yake ni safi na adili.
12 聽くところの耳と視るところの眼とはともにヱホバの造り給へるものなり
Masikio yasikiayo na macho yaonayo, Bwana ndiye alivifanya vyote viwili.
13 なんぢ睡眠を愛すること勿れ 恐くは貧窮にいたらん 汝の眼をひらけ 然らば糧に飽べし
Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.
14 買者はいふ惡し惡しと 然れど去りて後はみづから誇る
“Haifai, haifai!” asema mnunuzi, kisha huondoka akijisifia ununuzi wake.
15 金もあり眞珠も多くあれど貴き器は知識のくちびるなり
Dhahabu kunayo, na marijani kwa wingi, lakini midomo inenayo maarifa ni kito cha thamani kilicho adimu.
16 人の保證をなす者よりは先その衣をとれ 他人の保證をなす者をばかたくとらへよ
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
17 欺きとりし糧は人に甜し されど後にはその口に沙を充されん
Chakula kilichopatikana kwa hila ni kitamu kwa mwanadamu, bali huishia na kinywa kilichojaa changarawe.
18 謀計は相議るによりて成る 戰はんとせば先よく議るべし
Fanya mipango kwa kutafuta mashauri, ukipigana vita, tafuta maelekezo.
19 あるきめぐりて人の是非をいふ者は密事をもらす 口唇をひらきてあるくものと交ること勿れ
Maneno ya kusengenya husababisha kutokuaminika, kwa hiyo mwepuke mtu anayezungumza kupita kiasi.
20 おのれの父母を罵るものはその燈火くらやみの中に消ゆべし
Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itazimwa katika giza nene.
21 初に俄に得たる產業はその終さいはひならず
Urithi upatikanao haraka mwanzoni, hautabarikiwa mwishoni.
22 われ惡に報いんと言ふこと勿れ ヱホバを待て 彼なんぢを救はん
Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!” Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
23 二種の法馬はヱホバに憎まる 虚偽の權衡は善らず
Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu, nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.
24 人の歩履はヱホバによる 人いかで自らその道を明かにせんや
Hatua za mtu huongozwa na Bwana. Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?
25 漫に誓願をたつることは其人の罟となる誓願をたててのちに考ふることも亦然り
Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.
26 賢き王は箕をもて簸るごとく惡人を散し 車輪をもて碾すごとく之を罰す
Mfalme mwenye hekima hupepeta waovu, hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.
27 人の霊魂はヱホバの燈火にして人の心の奧を窺ふ
Taa ya Bwana huchunguza roho ya mwanadamu, huchunguza utu wake wa ndani.
28 王は仁慈と眞實をもて自らたもつ その位もまた恩惠のおこなひによりて堅くなる
Upendo na uaminifu humweka mfalme salama, kwa njia ya upendo, kiti chake cha enzi huwa salama.
29 少者の榮はその力 おいたる者の美しきは白髮なり
Utukufu wa vijana ni nguvu zao, mvi ni fahari ya uzee.
30 傷つくまでに打たば惡きところきよまり 打てる鞭は腹の底までもとほる
Mapigo na majeraha huusafisha ubaya, nayo michapo hutakasa utu wa ndani.

< 箴言 知恵の泉 20 >