< 箴言 知恵の泉 14 >

1 智慧ある婦はその家をたて 愚なる婦はおのれの手をもて之を毀つ
Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2 直くあゆむ者はヱホバを畏れ 曲りてあゆむ者はこれを侮る
Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
3 愚なる者の口にはその傲のために鞭笞あり 智者の口唇はおのれを守る
Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
4 牛なければ飼蒭倉むなし牛の力によりて生產る物おほし
Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
5 忠信の證人はいつはらず 虚偽のあかしびとは謊言を吐く
Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
6 嘲笑者は智慧を求むれどもえず 哲者は知識を得ること容易し
Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
7 汝おろかなる者の前を離れされ つひに知識の彼にあるを見ざるべし
Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
8 賢者の智慧はおのれの道を暁るにあり 愚なる者の痴は欺くにあり
Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
9 おろろかなる者は罪をかろんず されど義者の中には恩惠あり
Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
10 心の苦みは心みづから知る其よろこびには他人あづからず
Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
11 惡者の家は亡され 正直き者の幕屋はさかゆ
Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
12 人のみづから見て正しとする途にしてその終はつひに死にいたる途となるものあり
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
13 笑ふ時にも心に悲あり 歓樂の終に憂あり
Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
14 心の悖れる者はおのれの途に飽かん 善人もまた自己に飽かん
Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
15 拙者はすべての言を信ず 賢者はその行を愼む
Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
16 智慧ある者は怖れて惡をはなれ 愚なる者はたかぶりて怖れず
Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
17 怒り易き者は愚なることを行ひ 惡き謀計を設くる者は惡まる
Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
18 拙者は愚なる事を得て所有となし 賢者は知識をもて冠弁となす
Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
19 惡者は善者の前に俯伏し 罪ある者は義者の門に俯伏す
Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
20 貧者はその鄰にさへも惡まる されど富者を愛する者はおほし
Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
21 その鄰を藐むる者は罪あり 困苦者を憐むものは幸福あり
Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
22 惡を謀る者は自己をあやまるにあらずや 善を謀る者には憐憫と眞實とあり
Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
23 すべての勤勞には利益あり されど口唇のことばは貧乏をきたらするのみなり
Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
24 智慧ある者の財寳はその冠弁となる 愚なる者のおろかはただ痴なり
Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
25 眞實の證人は人のいのちを救ふ 謊言を吐く者は偽人なり
Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
26 ヱホバを畏るることは堅き依賴なり その兒輩は逃避場をうべし
Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
27 ヱホバを畏るることは生命の泉なり 人を死の罟より脱れしむ
Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
28 王の榮は民の多きにあり 牧伯の衰敗は民を失ふにあり
Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
29 怒を遅くする者は大なる知識あり 氣の短き者は愚なることを顯す
Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
30 心の安穩なるは身のいのちなり 娼嫉は骨の腐なり
Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
31 貧者を虐ぐる者はその造主を侮るなり 彼をうやまふ者は貧者をあはれむ
Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
32 惡者はその惡のうちにて亡され義者はその死ぬる時にも望あり
Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
33 智慧は哲者の心にとどまり 愚なる者の衷にある事はあらはる
Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
34 義は國を高くし罪は民を辱しむ
Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
35 さとき僕は王の恩を蒙ぶり 辱をきたらす者はその震怒にあふ
Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.

< 箴言 知恵の泉 14 >