< 箴言 知恵の泉 12 >
1 訓誨を愛する者は知識を愛す 懲戒を惡むものは畜のごとし
Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
2 善人はヱホバの恩寵をうけ 惡き謀略を設くる人はヱホバに罰せらる
Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
3 人は惡をもて堅く立ことあたはず 義人の根は動くことなし
Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
4 賢き婦はその夫の冠弁なり 辱をきたらする婦は夫をしてその骨に腐あるが如くならしむ
Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
5 義者のおもひは直し 惡者の計るところは虚偽なり
Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
6 惡者の言は人の血を流さんとて伺ふ されど直者の口は人を救ふなり
Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
7 惡者はたふされて無ものとならん されど義者の家は立べし
Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
8 人はその聰明にしたがひて譽られ 心の悖れる者は藐めらる
Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
9 卑賤してしもべある者は自らたかぶりて食に乏き者に愈る
Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
10 義者はその畜の生命を顧みる されど惡者は殘忍をもてその憐憫とす
Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
11 おのれの田地を耕すものは食にあく 放蕩なる人にしたがふ者は智慧なし
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
12 惡者はあしき人の獲たる物をうらやみ 義者の根は芽をいだす
Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
13 惡者はくちびるの愆によりて罟に陷る されど義者は患難の中よりまぬかれいでん
Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
14 人はその口の徳によりて福祉に飽ん 人の手の行爲はその人の身にかへるべし
Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
15 愚なる者はみづからその道を見て正しとす されど智慧ある者はすすめを容る
Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
16 愚なる者はただちに怒をあらはし 智きものは恥をつつむ
Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
17 眞實をいふものは正義を述べ いつはりの證人は虚偽をいふ
Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
18 妄りに言をいだし劍をもて刺がごとくする者あり されど智慧ある者の舌は人をいやす
Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
19 眞理をいふ口唇は何時までも存つ されど虚偽をいふ舌はただ瞬息のあひだのみなり
Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
20 惡事をはかる者の心には欺詐あり 和平を謀る者には歓喜あり
Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
21 義者には何の禍害も來らず 惡者はわざはひをもて充さる
Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
22 いつはりの口唇はヱホバに憎まれ 眞實をおこなふ者は彼に悦ばる
Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
23 賢人は知識をかくす されど愚なる者のこころは愚なる事を述ぶ
Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
24 勤めはたらく者の手は人ををさむるにいたり惰者は人に服ふるにいたる
Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
25 うれひ人の心にあれば之を屈ます されど善言はこれを樂します
Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
26 義者はその友に道を示す されど惡者は自ら途にまよふ
Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
27 惰者はおのれの猟獲たる物をも燔ず 勉めはたらくことは人の貴とき寳なり
Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.