< マタイの福音書 24 >
1 イエス宮を出でてゆき給ふとき、弟子たち宮の建造物を示さんとて御許に來りしに、
Yesu alitoka hekaluni na kwenda zake. Wanafunzi wake walimwendea na kumuonesha majengo ya hekalu.
2 答へて言ひ給ふ『なんぢら此の一切の物を見ぬか。誠に汝らに告ぐ、此處に一つの石も崩されずしては石の上に遺らじ』
Laikni aliwajibu na kuwaambia, “Je, hamuyaoni mambo haya yote? Kweli nawaambia, hakuna jiwe litalobaki juu ya lingine bila kubomolewa.”
3 オリブ山に坐し給ひしとき、弟子たち竊に御許に來りて言ふ『われらに告げ給へ、これらの事は何時あるか、又なんぢの來り給ふと世の終とには、何の兆あるか』 (aiōn )
Na alipokaa katika Mlima wa Mizeituni, wanafunzi wake walimwendea kwa faragha na kusema, “Tuambie, mambo haya yatatokea lini? Kitu gani kitakuwa dalili ya kuja kwako na mwisho wa ulimwengu?” (aiōn )
4 イエス答へて言ひ給ふ『なんぢら人に惑されぬやうに心せよ。
Yesu aliwajibu na kuwaambia, “Iweni makini kwamba asije mtu akawapotosha.
5 多くの者わが名を冒し來り「我はキリストなり」と言ひて多くの人を惑さん。
Kwa kuwa wengi watakuja kwa jina langu. Watasema, 'Mimi ndiye Kristo', na watawapotosha wengi.
6 又なんぢら戰爭と戰爭の噂とを聞かん、愼みて懼るな。かかる事はあるべきなり、されど未だ終にはあらず。
Mtasikia vita na taarifa za vita. Angalieni msije mkawa na wasiwasi, kwa kuwa mambo haya hayabudi kutokea; lakini ule mwisho utakuwa bado.
7 即ち「民は民に、國は國に逆ひて起たん」また處々に饑饉と地震とあらん、
Kwa kuwa taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na njaa na matetemeko ya ardhi katika sehemu mbalimbali.
Lakini mambo haya yote ni mwanzo tu wa uchungu wa kujifungua.
9 そのとき人々なんぢらを患難に付し、また殺さん、汝 等わが名の爲に、もろもろの國人に憎まれん。
Ndipo watawatoa kwa ajili ya mateso na kuwaua. Mtachukiwa na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.
10 その時おほくの人つまづき、且たがひに付し、互に憎まん。
Ndipo wengi watajikwaa na kusalitiana na watachukiana wenyewe kwa wenyewe.
11 多くの僞 預言者おこりて、多くの人を惑さん。
Manabii wengi wa uongo watatokea na kuwadanganya wengi.
12 また不法の増すによりて、多くの人の愛ひややかにならん。
Kwa sababu uovu utaongezeka, upendo wa wengi utapoa.
Lakini atakaye vumilia mpaka mwisho, ataokolewa.
14 御國のこの福音は、もろもろの國人に證をなさんため全世界に宣傅へられん、而してのち終は至るべし。
Hii Injili ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu mzima kama ushuhuda kwa mataifa yote. Na ndipo ule mwisho utafika.
15 なんぢら預言者ダニエルによりて言はれたる「荒す惡むべき者」の聖なる處に立つを見ば(讀む者さとれ)
Kwa hiyo, mtakapoona chukizo la uharibifu, lililosemwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu [asomaye na afahamu],
ndipo walioko Yuda wakimbilie milimani.
17 屋の上に居る者はその家の物を取り出さんとして下るな。
Na yule aliyeko juu ya paa la nyumba asiweze kuteremka chini kuchukua kitu chochote kutoka ndani ya nyumba yake,
naye aliyeko shambani asirudi kuchukua vazi lake.
19 その日には孕りたる者と乳を哺まする者とは禍害なるかな。
Lakini ole wao ambao wana mtoto na wale ambao wananyonyesha katika siku hizo!
20 汝らの遁ぐることの冬または安息 日に起らぬように祈れ。
Ombeni kwamba kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato.
21 そのとき大なる患難あらん、世の創より今に至るまでかかる患難はなく、また後にも無からん。
Kwa kuwa kutakuwa na dhiki kuu, ambayo haijawahi kuwapo tangu kuumbwa kwa ulimwengu hadi sasa, na wala haitakuwapo tena.
22 その日もし少くせられずば、一人だに救はるる者なからん、されど選民の爲にその日 少くせらるべし。
Kama siku hizo zisingefupishwa, hakuna ambaye angeokoka. Lakini kwa sababu ya wateule, siku hizo zitafupishwa.
23 その時あるひは「視よ、キリスト此處にあり」或は「此處にあり」と言ふ者ありとも信ずな。
Kisha ikiwa mtu yeyote atawaambia 'Tazama, Kristo yuko hapa! au, 'Kristo yuko kule' msiamini maneno hayo.
24 僞キリスト・僞 預言者おこりて、大なる徴と不思議とを現し、爲し得べくば選民をも惑さんとするなり。
Kwa kuwa Makristo wa uongo na manabii wa uongo watakuja na kuonesha ishara kubwa na maajabu, kwa kusudi la kupotosha, kama ingewezekana hata na wateule.
Tazameni, nimewatahadharisha kabla ya mambo hayo kutokea.
26 されば人もし汝らに「視よ、彼は荒野にあり」といふとも出で往くな「視よ、彼は部屋にあり」と言ふとも信ずな。
Kwa hiyo, ikiwa watawaambia, ''Kristo yuko jangwani,' msiende huko jangwani. Au, 'Tazameni, yuko ndani ya nyumba,' msiamini maneno hayo.
27 電光の東より出でて西にまで閃きわたる如く、人の子の來るも亦 然らん。
Kama vile radi inavyomulika kutokea mashariki na kuangaza hadi magharibi, ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.
Popote ulipo mzoga, huko ndiko tai wakusanyikapo.
29 これらの日の患難ののち直ちに日は暗く、月は光を發たず、星は空より隕ち、天の萬象ふるひ動かん。
Lakini mara baada ya dhiki kuu ya siku zile, Jua litatiwa giza, mwezi hautatoa mwanga wake, nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbinguni zitatikisika.
30 そのとき人の子の兆、天に現れん。そのとき地上の諸族みな嘆き、かつ人の子の能力と大なる榮光とをもて、天の雲に乘り來るを見ん。
Ndipo ishara ya Mwana wa Adamu itaonekana angani, na makabila yote ya dunia wataomboleza. Watamwona Mwana wa Adamu akija katika mawingu ya angani kwa nguvu na utukufu mkuu.
31 また彼は使たちを大なるラッパの聲とともに遣さん。使たちは天の此の極より彼の極まで、四方より選民を集めん。
Atawatuma malaika wake kwa sauti kuu ya tarumbeta, nao watawakusanya pamoja wateule wake kutoka pande nne za dunia, kutoka mwisho mmoja wa mbingu hadi mwingine.
32 無花果の樹よりの譬をまなべ、その枝すでに柔かくなりて葉 芽ぐめば、夏の近きを知る。
Jifunzeni somo kutokana na mti mtini. Mara tu tawi linapochipuka na kutoa majani, mnajua kwamba kiangazi kinakaribia.
33 かくのごとく汝らも此 等のすべての事を見ば、人の子すでに近づきて門邊に到るを知れ。
Hivyo pia, mtakapoona mambo haya yote, mnapaswa kujua kwamba amekaribia, karibu na malango.
34 誠に汝らに告ぐ、これらの事ことごとく成るまで、今の代は過ぎ往くまじ。
Kweli nawaambia, kizazi hiki hakitapita, hadi mambo yote haya yatakuwa yametokea.
35 天 地は過ぎゆかん、されど我が言は過ぎ往くことなし。
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
36 その日その時を知る者なし、天の使たちも知らず、子も知らず、ただ父のみ知り給ふ。
Lakini kuhusu siku ile na saa hakuna mtu ajuaye, hata malaika wa mbinguni, wala Mwana, bali Baba peke yake.
Kama vile ilivyokuwa katika siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.
38 曾て洪水の前ノア方舟に入る日までは、人々 飮み食ひ、娶り嫁がせなどし、
Kwa kuwa katika siku hizo kabla ya gharika watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa hadi siku ile ambayo Nuhu aliingia katika safina,
39 洪水の來りて悉とく滅すまでは知らざりき、人の子の來るも然あるべし。
na hawakujua kitu chochote hadi gharika ilipokuja na kuwasomba wote - ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.
40 そのとき二人の男 畑にをらんに、一人は取られ一人は遺されん。
Ndipo watu wawili watakuwa shambani- mmoja atachukuliwa, na mmoja ataachwa nyuma.
41 二人の女 磨ひき居らんに、一人は取られ一人は遺されん。
Wanawake wawili watakuwa wanasaga pamoja - mmoja atachukuliwa, na mmoja atabaki.
42 されば目を覺しをれ、汝らの主のきたるは、何れの日なるかを知らざればなり。
Kwa hiyo, kuweni macho kwa sababu hamjui ni siku gani ambayo atakuja Bwana wenu.
43 汝 等これを知れ、家主もし盜人いづれの時きたるかを知らば、目をさまし居て、その家を穿たすまじ。
Lakini mjue kwamba, ikiwa bwana mwenye nyumba angejua ni saa ipi ambayo mwizi angekuja, angekesha na asingeruhusu nyumba yake kuvamiwa.
44 この故に汝らも備へをれ、人の子は思はぬ時に來ればなり。
Kwa hiyo, pia mnapaswa kuwa tayari, kwa kuwa Mwana wa Adamu atakuja katika saa msiyoitarajia.
45 主人が時に及びて食物を與へさする爲に、家の者のうへに立てたる忠實にして慧き僕は誰なるか。
Hivyo ni nani aliye mwaminifu, mtumwa mwenye akili, ambaye bwana wake amempa madaraka juu ya walio katika nyumba yake, ili awape chakula kwa wakati unaofaa?
46 主人のきたる時、かく爲し居るを見らるる僕は幸福なり。
Amebarikiwa mtumishi huyo, ambaye bwana wake atamkuta akifanya hivyo wakati ajapo.
47 まことに汝らに告ぐ、主人すべての所有を彼に掌どらすべし。
Kweli nawaambia kwamba bwana atamweka juu ya kila kitu kilicho chake.
48 もしその僕 惡しくして、心のうちに主人は遲しと思ひて、
Lakini kama mtumwa mwovu akisema moyoni mwake, 'Bwana wangu amekawia,'
49 その同輩を扑きはじめ、酒徒らと飮食を共にせば、
na akaanza kuwapiga watumishi wake, na akala na kulewa vileo,
Bwana wa mtumwa huyo atakuja katika siku ambayo haitarajii, na katika saa ambayo haijui.
51 之を烈しく笞うち、その報を僞善者と同じうせん。其處にて哀哭・切齒することあらん。
Bwana wake atamkata vipande viwili na kumweka katika nafasi moja sawa na wanafiki, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.