< レビ記 18 >
2 イスラエルの子孫に告て之に言へ我は汝らの神ヱホバなり
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.
3 汝らその住をりしエジプトの國に行はるる所の事等を傚ひ行ふべからずまた我が汝等を導きいたるカナンの國におこなはるる所の事等を傚ひおこなふべからずまたその例に歩行べからず
Msifanye kama wafanyavyo huko Misri, mahali mlipokuwa mnaishi, wala msifanye kama wanavyofanya katika nchi ya Kanaani, mahali ninapowapeleka. Msifuate matendo yao.
4 汝等は我が法を行ひ我が例をまもりてその中にあゆむべし我は汝等の神ヱホバなり
Ni lazima mzitii sheria zangu, na mwe waangalifu kuzifuata amri zangu. Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.
5 汝等わが例とわが法をまもるべし人もし是を行はば之によりて生べし我はヱホバなり
Zishikeni amri zangu na sheria zangu, kwa maana mtu anayezitii ataishi kwa hizo. Mimi ndimi Bwana.
6 汝等凡てその骨肉の親に近づきて之と淫するなかれ我はヱホバなり
“‘Hakuna mtu awaye yote atakayemsogelea ndugu wa karibu ili kukutana naye kimwili. Mimi ndimi Bwana.
7 汝の母と淫するなかれ是汝の父を辱しむるなればなり彼は汝の母なれば汝これと淫するなかれ
“‘Usimvunjie heshima baba yako kwa kukutana kimwili na mama yako. Yeye ni mama yako; usiwe na mahusiano kama hayo naye.
8 汝の父の妻と淫するなかれ是汝の父を辱しむるなればなり
“‘Usikutane kimwili na mke wa baba yako; hiyo itamvunjia heshima baba yako.
9 汝の姉妹すなはち汝の父の女子と汝の母の女子は家に生れたると家外に生れたるとによらず凡てこれと淫するなかれ
“‘Usikutane kimwili na dada yako, wala binti wa baba yako, au binti wa mama yako, awe amezaliwa katika nyumba hiyo au mahali pengine.
10 汝の男子の女子または汝の女子の女子と淫する事なかれ是自己を辱しむるなればなり
“‘Usikutane kimwili na binti wa mwanao ama binti wa binti yako; utajivunjia heshima.
11 汝の父の妻が汝の父によりて產たる女子は汝の姉妹なれば之と淫する勿れ
“‘Usikutane kimwili na binti wa mke wa baba yako, aliyezaliwa na baba yako; huyo ni dada yako.
12 汝の父の姉妹と淫するなかれ是は汝の父の骨肉の親なればなり
“‘Usikutane kimwili na dada wa baba yako; ni ndugu wa karibu wa baba yako.
13 また汝の母の姉妹と淫する勿れ是は汝の母の骨肉の親なり
“‘Usikutane kimwili na dada wa mama yako, kwa sababu ni ndugu wa mama yako wa karibu.
14 汝の父の兄弟の妻に親づきて之と淫する勿れ是は汝の叔伯母なり
“‘Usimvunjie heshima ndugu wa baba yako, kwa kukutana kimwili na mke wake; yeye ni shangazi yako.
15 汝の媳と淫するなかれ是は汝の息子の妻なれば汝これと淫する勿れ
“‘Usikutane kimwili na mkwe wako, yeye ni mke wa mwanao; usiwe na mahusiano kama hayo naye.
16 汝の兄弟の妻と淫する勿れ是汝の兄弟を辱しむるなればなり
“‘Usikutane kimwili na mke wa kaka yako; utamvunjia heshima kaka yako.
17 汝婦人とその婦の女子とに淫する勿れまたその婦人の子息の女子またはその女子の女子を取て之に淫する勿れ是等は汝の骨肉の親なれば然するは惡し
“‘Usikutane kimwili na mwanamke kisha na binti yake. Usikutane kimwili na binti wa mwanawe au binti wa binti yake; hao ni ndugu zake wa karibu. Huo ni uovu.
18 汝妻の尚生る間に彼の姉妹を取て彼とおなじく妻となして之に淫する勿れ
“‘Usimchukue dada wa mke wako kuwa mke mwenza, na kukutana naye kimwili wakati bado mke wako anaishi.
19 婦のその行經の汚穢にある間はこれに近づきて淫するなかれ
“‘Usimsogelee mwanamke ili kukutana naye kimwili wakati wa unajisi wa siku zake za mwezi.
20 汝の鄰の妻と交合して彼によりて己が身を汚すなかれ
“‘Usikutane kimwili na mke wa jirani yako na kujitia naye unajisi.
21 汝その子女に火の中を通らしめてこれをモロクにささぐることを絶て爲ざれ亦汝の神ヱホバの名を汚すことなかれ我はヱホバなり
“‘Usimtoe mtoto wako yeyote awe kafara kwa mungu Moleki, kwani hutalinajisi kamwe jina la Mungu wako. Mimi ndimi Bwana.
22 汝女と寝るごとくに男と寝るなかれ是は憎むべき事なり
“‘Usikutane kimwili na mwanaume kama mtu akutanaye na mwanamke; hilo ni chukizo.
23 汝獣畜と交合して之によりて己が身を汚すこと勿れまた女たる者は獣畜の前に立て之と接ること勿れ是憎むべき事なり
“‘Usikutane kimwili na mnyama na kujitia unajisi kwake. Mwanamke asijipeleke kwa mnyama ili kukutana naye kimwili; huo ni upotovu.
24 汝等はこの諸の事をもて身を汚すなかれ我が汝等の前に逐はらふ國々の人はこの諸の事によりて汚れ
“‘Msijitie unajisi kwa njia yoyote katika hizi, kwa sababu hivi ndivyo mataifa nitakayoyafukuza mbele yenu yalivyojitia unajisi.
25 その地もまた汚る是をもて我その惡のために之を罰すその地も亦自らそこに住る民を吐いだすなり
Hata nchi ilitiwa unajisi, hivyo nikaiadhibu kwa dhambi zake, nayo nchi ikawatapika wakazi wake.
26 然ば汝等はわが例と法を守りこの諸の憎むべき事を一も爲べからず汝らの國の人も汝らの中間に寄寓る他國の人も然るべし
Lakini ni lazima uzitunze amri zangu na sheria zangu. Mzawa na wageni waishio miongoni mwenu kamwe wasifanye mambo yoyote ya machukizo haya,
27 汝等の先にありし此地の人々はこの諸の憎むべき事を行へりその地もまた汚る
kwa kuwa mambo haya yote yalifanywa na watu walioishi katika nchi hii kabla yenu, na nchi ikawa najisi.
28 汝等は是のごとくするなかれ恐くはこの地汝らの先にありし國人を吐いだす如くに汝らをも吐いださん
Kama mkiinajisi nchi, itawatapika kama ilivyowatapika mataifa yaliyowatangulia.
29 凡そこの憎むべき事等を一にても行ふ者あれば之を行ふ人はその民の中より絶るべし
“‘Kila mtu atakayefanya mojawapo ya machukizo haya, watu hao ni lazima wakatiliwe mbali na watu wao.
30 然ば汝等はわが例規を守り汝等の先におこなはれし是等の憎むべき習俗を一も行ふなかれまた之によりて汝等身を汚す勿れ我は汝等の神ヱホバなり
Shikeni maagizo yangu, wala msifuate desturi za machukizo yoyote yaliyofanywa kabla hamjafika katika nchi hii, na kujitia unajisi kwa hayo. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.’”