< ヨシュア記 19 >

1 次にシメオンのため即ちシメオン子孫の支派のためにその宗族にしたがひて籤を掣りその產業ばユダの子孫の產業の中にあり
Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
2 その有る產業はベエルシバ即ちシバ、モラダ
Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
3 ハザルシユアル、バラ、エゼム
Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
4 エルトラデ、ベトル、ホルマ
Eltoladi, Bethuli, Horma,
5 チクラグ、ベテマルカボテ、ハザルスサ
Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
6 ベテレバオテ、シヤルヘンの十三邑並びに之につける村々
Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.
7 およびアイン、リンモン、エテル、アシヤンの四邑ならびに之につける村々
Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
8 および此邑々の周圍にありてバアラテベエルすなはち南のラマまでに至るところの一切の村々等なりシメオンの子孫の支派がその宗族にしたがひて獲たる產業は是のごとし
pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.
9 シメオンの子孫の產業はユダの子孫の分の中より出づ是ユダの子孫の分自分のためには多かりしに因てシメオンの子孫のおのれの產業を彼らの產業の中に獲たるなり
Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
10 第三にゼブルンの子孫のために其宗族にしたがひて籤を掣り其產業の境界はサリデに及び
Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
11 また西に上りてマララに至りダバセテに達しヨグネアムの前なる河に達し
Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.
12 サリデよりして東の方日のいづる方にまがりてキスロテタボルの境界にいたりタベラに出でヤピアに上り
Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
13 彼處より東の方ガテヘペルにわたりてイツタカジンにいたりネアまで廣がるところのリンモンに至りて盡き
Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
14 また北にまはりてハンナトンにいたりイフタエルの谷にいたりて盡く
Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
15 カツタテ、ナハラル、シムロン、イダラ、ベテレヘムなどの十二邑ならびに之につける村々あり
Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
16 ゼブルンの子孫がその宗族にしたがひて獲たる產業およびその邑と村とは是のごとし
Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.
17 第四にイツサカルすなはちイツサカルの子孫のためにその宗族にしたがひて籤を掣り
Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.
18 その境界の包括る處はヱズレル、ケスロテ、シユネム
Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
19 ハパライム、シオン、アナハラテ
Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
20 ラビテ、キシン、エベツ
Rabithi, Kishioni, Ebesi,
21 レメテ、エンガンニム、エンハダ、ベテパツゼズなどなり
Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
22 その境界タボル、シヤハヂマおよびベテシメシに達しその境界ヨルダンにいたりて盡く其邑あはせて十六また之につける村々あり
Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
23 イツサカルの子孫の支派が其宗族にしたがひて獲たる產業および其邑々村々は是の如し
Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.
24 第五にアセルの子孫の支派のために其宗族にしたがひて籤を掣り
Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
25 其境界の内はヘルカテ、ハリ、ベテン、アクサフ
Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,
26 アランメレク、アマデ、ミシヤルなり其境界西の方カルメルに達しまたシホルリブナテに達し
Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
27 日の出る方に折てベテダゴンにいたりゼブルンに達し北の方イフタヱルの谷のベテエメク及びネイエルに達し左してカブルに出で
Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
28 エプロン、レホブ、ハンモン、カナにわたりて大シドンにまでいたり
Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
29 ラマに旋りツロの城に及びまたホサに旋りアクジブの邊にて海にいたりて盡く
Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
30 またウンマ、アベクおよびレホブありその邑あはせて二十二また之につける村々あり
Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
31 アセルの子孫の支派がその宗族にしたがひて獲たる產業およびその邑々村々は是のごとし
Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
32 第六にナフタリの子孫のためにナフタリの子孫の宗族にしたがひて籤を掣り
Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
33 その境界はヘレフより即ちザアナイムの樫の樹より起りアダミネケブおよびヤブニエルを經てラクムにいたりヨルダンにいたりて盡く
Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
34 而して其境界西に旋りてアズノテタボルにいたり彼處よりホツコクに出で南はゼブルンに達し西はアセルに達し日の出る方はヨルダンの邊にてユダに達す
Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
35 その堅固たる邑々はヂデム、ゼル、ハンマテ、ラツカテ、キンネレテ
Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
36 アダマ、ラマ、ハゾル
Adama, Rama, Hazori,
37 ケデシ、エデレイ、エンハゾル
Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
38 イロン、ミグダルエル、ホレム、ベテアナテ、ベテシメシなど合せて十九邑亦これにつける村々あり
Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
39 ナフタリの子孫の支派がその宗族にしたがひて獲たる產業およびその邑々村々は是のごとし
Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
40 第七にダンの子孫の支派のためにその宗族にしたがひて籤を掣り
Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
41 その產業の境界の内はゾラ、エシタオル、イルシメシ
Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
42 シヤラビム、アヤロン、イテラ
Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
43 エロン、テムナ、エクロン
Eloni, Timna, Ekroni,
44 エルテケ、ギベトン、バアラテ
Elteke, Gibethoni, Baalathi,
45 ヱホデ、ベネベラク、ガテリンモン
Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
46 メヤルコン、ラツコン、ヨツパと相對ふ地などなり
Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
47 但しダンの子孫の境界は初よりは廣くなれり其はダンの子孫上りゆきてライシを攻取り刃をもちてこれを撃ほろぼし之を獲て其處に住たればなり而してその先祖ダンの名にしたがびてライシをダンと名けたり
(Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
48 ダンの子孫の支派がその宗族にしたがひて獲たる產業およびその邑々村々は是のごとし
Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
49 かく境界を畫りて產業の地を與ふることを終ぬ而してイスラエルの子孫おのれの中にてヌンの子ヨシユアに產業を與へたり
Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,
50 すなはちヱホバの命にしたがひて彼にその求むる邑を與ふエフライムの山地なるテムナテセラ是なり彼その邑を建なほして其處に住む
kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
51 祭司エレアザル、ヌンの子ヨシユアおよびイスラエルの子孫の支派の族長等がシロにおいて集會の幕屋の門にてヱホバの前に籤をもて分與へし產業は是のごとし斯地を分つことを終たり
Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.

< ヨシュア記 19 >