< ヨブ 記 33 >

1 然ばヨブよ請ふ我が言ふ事を聽け わが一切の言語に耳を傾むけよ
Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
2 視よ我口を啓き 舌を口の中に動かす
Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
3 わが言ふ所は正義き心より出づ わが唇あきらかにその知識を陳ん
Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
4 神の靈われを造り 全能者の氣息われを活しむ
Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
5 汝もし能せば我に答へよ わが前に言をいひつらねて立て
Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
6 我も汝とおなじく神の者なり 我もまた土より取てつくられしなり
Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
7 わが威嚴はなんぢを懼れしめず わが勢はなんぢを壓せず
Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
8 汝わが聽くところにて言談り 我なんぢの言語の聲を聞けり云く
Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
9 われは潔淨くして愆なし 我は辜なく惡き事わが身にあらず
'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
10 視よ彼われを攻る釁隙を尋ね われを己の敵と算へ
Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
11 わが脚を桎に夾めわが一切の擧動に目を着たまふと
Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
12 視よ我なんぢに答へん なんぢ此事において正義からず 神は人よりも大なる者にいませり
Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
13 彼その凡て行なふところの理由を示したまはずとて汝かれにむかひて辯爭そふは何ぞや
Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
14 まことに神は一度二度と告示したまふなれど人これを曉らざるなり
Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
15 人熟睡する時または床に睡る時に夢あるひは夜の間の異象の中にて
Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
16 かれ人の耳をひらき その敎ふるところを印して堅うし
basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
17 斯して人にその惡き業を離れしめ 傲慢を人の中より除き
kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
18 人の魂靈を護りて墓に至らしめず 人の生命を護りて劍にほろびざらしめたまふ
Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
19 人床にありて疼痛に攻られ その骨の中に絶ず戰鬪のあるあり
Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
20 その氣食物を厭ひ その魂靈うまき物をも嫌ふ
ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
21 その肉は痩おちて見えず その骨は見えざりし者までも顯露になり
Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
22 その魂靈は墓に近より その生命は滅ぼす者に近づく
Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
23 しかる時にもし彼とともに一箇の使者あり 千の中の一箇にして中保となり 正しき道を人に示さば
Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
24 神かれを憫れみて言給はん彼を救ひて墓にくだること無らしめよ 我すでに收贖の物を得たりと
na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
25 その肉は小兒の肉よりも瑞々しくなり その若き時の形状に歸らん
kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
26 かれ若し神に祷らば神かれを顧りみ 彼をしてその御面を喜こび見ることを得せしめたまはん 神は人の正義に報をなしたまふべし
Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
27 かれ人の前に歌ひて言ふ 我は罪を犯し正しきを抂たり 然ど報を蒙らず
Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
28 神わが魂靈を贖ひて墓に下らしめず わが生命光明を見ん
Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
29 そもそも神は是等のもろもろの事をしばしば人におこなひ
Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
30 その魂靈を墓より牽かへし生命の光明をもて彼を照したまふ
kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
31 ヨブよ耳を傾むけて我に聽け 請ふ默せよ 我かたらん
Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
32 なんぢもし言ふべきことあらば我にこたへよ 請ふ語れ 我なんぢを義とせんと慾すればなり
Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
33 もし無ば我に聽け 請ふ默せよ 我なんぢに智慧を敎へん
Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”

< ヨブ 記 33 >