< ヨブ 記 31 >

1 我わが目と約を立たり 何ぞ小艾を慕はんや
Nimefanya patano na macho yangu; ni kwa namna gani tena napaswa kumtazama mwanamwali kwa tamaa?
2 然せば上より神の降し給ふ分は如何なるべきぞ 高處より全能者の與へ給ふ業は如何なるべきぞ
Ni sehemu gani kutoka kwa Mungu juu, na urithi gani kutoka kwake mwenye nguvu aliye juu?
3 惡き人には滅亡きたらざらんや 善らぬ事を爲す者には常ならぬ災禍あらざらんや
Nilikuwa nafikiri kwamba majanga ni kwa watu wasio na haki, na misiba ni kwa ajili ya watu watendao mabaya.
4 彼わが道を見そなはし わが歩履をことごとく數へたまはざらんや
Je Mungu hazioni njia zangu na kuzihesabu hatua zangu zote?
5 我虚誕とつれだちて歩みし事ありや わが足虚僞に奔從がひし事ありや
Kama nimetembea katika udanganyifu, kama mguu wangu umeharakisha katika uongo,
6 請ふ公平き權衡をもて我を稱れ 然ば神われの正しきを知たまはん
na nipimwe katika vipimo vilivyo sawa ili kwamba Mungu aujue uadilifu wangu.
7 わが歩履もし道を離れ わが心もしわが目に隨がひて歩み わが手にもし汚のつきてあらば
Kama hatua zangu zimegeuka kutoka katika njia sahihi, kama moyo wangu umetembea kwa kufuata macho yangu, na kama doa lolote la uchafu limeng'ang'ania katika mikono yangu,
8 我が播たるを人食ふも善し わが產物を根より拔るるも善し
na kisha mimi nipande na mtu mwingine na ale; mavuno na yang'olewe katika shamba langu.
9 われもし婦人のために心まよへる事あるか 又は我もしわが隣の門にありて伺ひし事あらば
Na kama moyo wangu umevutiwa na mwanamke mwingine, ikiwa nimelala na mke wa jirani yangu katika hali ya kusubiria katika mlango wake,
10 わが妻ほかの人のために臼磨き ほかの人々かれの上に寢るも善し
na ndipo mke wangu na asage nafaka kwa mwanaume mwingine, na wanaume wengine na walale naye.
11 其は是は重き罪にして裁判人に罰せらるべき惡事なればなり
Na kwa hilo litakuwa ni kosa kubwa; kwa kweli, utakuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi.
12 是はすなはち滅亡にまでも燬いたる火にしてわが一切の產をことごとく絶さん
Kwa kuwa ni moto ambao unateketeza kila kitu kwa uharibifu, na kwamba utaunguza mavuno yangu yote.
13 わが僕あるひは婢の我と辯爭ひし時に我もし之が權理を輕んぜし事あらば
Ikiwa nilikataa ombi la haki kutoka kwa watumishi wangu wa kiume na wa kike wakati walipohojiana nami,
14 神の起あがりたまふ時には如何せんや 神の臨みたまふ時には何と答へまつらんや
kisha nini basi ningefanya wakati Mungu anapoinuka ili kunishitaki mimi? Atakapokuja kunihukumu, nitamjibuje?
15 われを胎内に造りし者また彼をも造りたまひしならずや われらを腹の内に形造りたまひし者は唯一の者ならずや
Je yeye aliyenifanya mimi tumboni hakuwafanya wao pia? Je yeye si yeye yule aliyetuumba sisi wote katika tumbo?
16 我もし貧き者にその願ふところを獲しめず 寡婦をしてその目おとろへしめし事あるか
kama nimewanyima watu masikini matakwa yao, au kama nimesababisha macho ya wajane yafifie kwa kulia,
17 または我獨みづから食物を啖ひて孤子にこれを啖はしめざりしこと有るか
au ikiwa kama nimekula kipande changu na sijawaruhusu wale wasio na baba kukila pia -
18 (却つて彼らは我が若き時より我に育てられしこと父におけるが如し 我は胎内を出てより以來寡を導びく事をせり)
kwasababu tangu ujana wangu yatima walikua pamoja nami kama kuwa na baba, nami nimemwongoza mama yake, mjane, tangu katika tumbo la mama yangu mwenyewe.
19 われ衣服なくして死んとする者あるひは身を覆ふ物なくして居る人を見し時に
ikiwa nimemwona yeyote akiangamia kwa kwa kukosa mavazi, au kama nimemwona mtu mhitaji akiwa hana nguo;
20 その腰もし我を祝せず また彼もしわが羊の毛にて温まらざりし事あるか
ikiwa moyo wake haujanibariki kwasababu amekuwa hajatiwa joto na sufu ya kondoo zangu,
21 われを助くる者の門にをるを見て我みなしごに向ひて手を上し事あるか
ikiwa nimeinua juu mkono wangu kinyume na watu wasio na baba kwa kuwa niliona msaada wangu katika lango la mji, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu.
22 然ありしならば肩骨よりしてわが肩おち骨とはなれてわが腕折よ
Ndipo bega langu na lianguake kutoka katika sehemu yake, na mkono wangu uvunjike katika kiungo chake.
23 神より出る災禍は我これを懼る その威光の前には我 能力なし
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu; kwasababu ya mawazo ya ukuu wake, nisingeweza kufanya mambo hayo.
24 我もし金をわが望となし 精金にむかひて汝わが所賴なりと言しこと有か
Kama ningeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, na kama ningesema kwa dhahabu safi, 'wewe unanifanya kuwa na tumaini';
25 我もしわが富の大なるとわが手に物を多く獲たることを喜びしことあるか
na kama nimefurahi kwasababu ya utajiri wangu ulikuwa mkubwa, kwa kuwa mkono wangu umepata mali nyingi, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu!
26 われ日の輝くを見または月の輝わたりて歩むを見し時
Ikiwa nimeliona jua lilipowaka, au mwezi ukitembea katika mng'ao wake,
27 心竊にまよひて手を口に接しことあるか
na kama moyo wangu umevutwa kwa siri, ili kwamba mdomo wangu umeubusu mkono wangu katika ibada yao -
28 是もまた裁判人に罪せらるべき惡事なり 我もし斯なせし事あらば上なる神に背しなり
hili nalo pia lingekuwa ni ubaya wa kuadhibiwa na waamuzi, kwa kuwa ningekuwa nimemkana Mungu aliyejuu.
29 我もし我を惡む者の滅亡るを喜び 又は其災禍に罹るによりて自ら誇りし事あるか
Ikiwa nimefurahia uharibifu wa yeyote ambaye ananichukia mimi, au kuwapa hongera wakati majanga yanapowapata, ndipo ulete mashitaka dhidi yangu!
30 (我は之が生命を呪ひ索めて我口に罪を犯さしめし如き事あらず)
Kwa kweli sijauruhusu hata mdomo wangu kutenda dhambi kwa kuuomba uhai wake kwa laana.
31 わが天幕の人は言ずや彼の肉に飽ざる者いづこにか在んと
Ikiwa watu wa hema yangu hawajasema,' Nani aweza kumpata mtu ambaye hayashibishwa na chakula cha Ayubu?
32 旅人は外に宿らず わが門を我は街衢にむけて啓けり
(hata mgeni hajawahi kukaa katika pembe ya mji, kwa kuwa siku zote nimefungua milango yangu kwa ajili ya wasafiri), na kama haiko hivyo, ndipo mlete mashitaka kinyume nami!
33 我もしアダムのごとくわが罪を蔽ひ わが惡事を胸に隱せしことあるか
Ikiwa, kama binadamu nimezificha dhambi zangu kwa kuficha hatia ndani ya kanzu yangu -
34 すなはち大衆を懼れ宗族の輕蔑に怖ぢて口を閉ぢ門を出ざりしごとき事あるか
kwa kuwa niliogopa kusanyiko kubwa, kwasababu ya matwezo ya familia yaliniogopesha, hivyo basi nilinyamaza kimya na sikuweza kwenda nje, basi nileteni mashitaka dhidi yangu!
35 嗚呼われの言ところを聽わくる者あらまほし(我が花押ここに在り 願くは全能者われに答へたまへ)我を訴ふる者みづから訴訟状を書け
Ee, kama nilikuwa na mtu wa kunisikiliza! Ona, hii ni saini yangu; na Mwenye nguvu na anijibu! Ikiwa nilikuwa na shitaka rasmi ambalo adui yangu ameliandika!
36 われ必らず之を肩に負ひ冠冕のごとくこれを首に結ばん
Hakika ningelibeba hadharani juu ya bega langu; ningeliweka juu kama taji.
37 我わが歩履の數を彼に述ん 君王たる者のごとくして彼に近づかん
Ningemweleza hesabu ya hatua zangu; na kama mwana wa mfalme mwenye kujiamini ningepanda kwenda kwake.
38 わが田圃號呼りて我を攻め その阡陌ことごとく泣さけぶあるか
Kama nchi yangu ingelia dhidi yangu, na matuta yake yaomboleza pamoja,
39 若われ金を出さずしてその產物を食ひ またはその所有主をして生命を失はしめし事あらば
ikiwa nimekula mavuno yake bila kulipia au kama nimesababisha wamiliki wake kupoteza maisha yao,
40 小麥の代に蒺藜生いで 大麥のかはりに雜草おひ出るとも善し ヨブの詞をはりぬ
ndipo miiba na iote badala ya ngano na magugu badala ya shayiri.” Maneno ya Ayubu yamemalizika.

< ヨブ 記 31 >