< ヨブ 記 27 >

1 ヨブまた語を繼ぎていはく
Ndipo Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2 われに義しき審判を施したまはざる神 わが心魂をなやまし給ふ全能者此神は活く
“Hakika kama Mungu aishivyo, aliyeninyima haki yangu, Mwenyezi ambaye amenifanya nionje uchungu wa nafsi,
3 (わが生命なほ全くわれの衷にあり 神の氣息なほわが鼻にあり)
kwa muda wote nitakaokuwa na uhai ndani yangu, nayo pumzi ya Mungu ikiwa puani mwangu,
4 わが口は惡を言ず わが舌は謊言を語らじ
midomo yangu haitanena uovu, wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu.
5 我決めて汝等を是とせじ 我に死るまで我が罪なきを言ことを息じ
Sitakubaliana nanyi kabisa kuwa mko sahihi; hadi nife, sitakana uadilifu wangu.
6 われ堅くわが正義を持ちて之を棄じ 我は今まで一日も心に責られし事なし
Nitadumisha haki yangu wala sitaiacha; dhamiri yangu haitanisuta muda wote ninaoishi.
7 我に敵する者は惡き者と成り我を攻る者は義からざる者と成るべし
“Watesi wangu wawe kama waovu, nao adui zangu wawe kama wasio haki!
8 邪曲なる者もし神に絶れその魂神を脱とらるるに於ては何の望かあらん
Kwa maana mtu asiyemcha Mungu analo tegemeo gani anapokatiliwa mbali, Mungu anapouondoa uhai wake?
9 かれ艱難に罹る時に神その呼號を聽いれたまはんや
Je, Mungu husikiliza kilio chake, shida zimjiapo?
10 かれ全能者を喜こばんや 常に神を龥んや
Je, anaweza kumfurahia Mwenyezi? Je, atamwita Mungu nyakati zote?
11 われ神の御手を汝等に敎へん 全能者の道を汝等に隱さじ
“Nitawafundisha juu ya uweza wa Mungu; njia za Mwenyezi sitazificha.
12 視よ汝等もみな自らこれを觀たり 然るに何ぞ斯愚蒙をきはむるや
Ninyi nyote mmeona hili wenyewe. Ni ya nini basi mazungumzo haya yasiyo na maana?
13 惡き人の神に得る分 強暴の人の全能者より受る業は是なり
“Hili ndilo fungu ambalo Mungu humpa mtu mwovu, urithi ule mtu mdhalimu anapokea kutoka kwa Mwenyezi:
14 その子等蕃れば劍に殺さる その子孫は食物に飽ず
Hata kama watoto wake watakuwa wengi kiasi gani, fungu lao ni kuuawa kwa upanga; wazao wake hawatakuwa kamwe na chakula cha kuwatosha.
15 その遺れる者は疫病に斃れて埋められ その妻等は哀哭をなさず
Tauni itawazika wale watakaonusurika miongoni mwao, nao wajane wao hawatawaombolezea.
16 かれ銀を積こと塵のごとく衣服を備ふること土のごとくなるとも
Ajapokusanya fedha nyingi kama mavumbi, na mavazi kama malundo ya udongo wa mfinyanzi,
17 その備ふる者は義き人これを着ん またその銀は無辜者これを分ち取ん
yale yote mtu mwovu aliyojiwekea akiba, mwenye haki atayavaa, naye asiye na hatia ataigawanya fedha yake.
18 その建る家は蟲の巣のごとく また番人の造る茅家のごとし
Nyumba aijengayo ni kama utando wa buibui, kama kibanda alichotengeneza mlinzi.
19 彼は富る身にて寢臥し重ねて興ること無し また目を開けば即ちその身きえ亡す
Yeye hulala akiwa tajiri, lakini ndiyo mara ya mwisho; afunguapo macho yake, yote yametoweka.
20 懼ろしき事大水のごとく彼に追及き 夜の暴風かれを奪ひ去る
Vitisho humjia kama mafuriko; dhoruba humkumba ghafula usiku.
21 東風かれを颺げて去り 彼をその處より吹はらふ
Upepo mkali wa mashariki humchukua, naye hutoweka; humzoa kutoka mahali pake.
22 神かれを射て恤まず 彼その手より逃れんともがく
Humvurumisha bila huruma, huku akikimbia kasi kukwepa nguvu zake.
23 人かれに對ひて手を鳴し 嘲りわらひてその處をいでゆかしむ
Upepo humpigia makofi kwa dharau, na kumfukuza atoke mahali pake.

< ヨブ 記 27 >