< ヨブ 記 20 >

1 ナアマ人ゾパルこたへて曰く
Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu:
2 これに因てわれ答をなすの思念を起し心しきりに之がために急る
“Mawazo yanayonisumbua yananisukuma kujibu, kwa sababu nimehangaika sana.
3 我を辱しむる警語を我聞ざるを得ず 然しながらわが了知の性われをして答ふることを得せしむ
Ninasikia makaripio ambayo yananivunjia heshima, nao ufahamu wangu unanisukuma kujibu.
4 なんぢ知ずや古昔より地に人の置れしより以來
“Hakika unajua jinsi ilivyokuwa tangu zamani, tangu zamani mwanadamu alipowekwa duniani,
5 惡き人の勝誇は暫時にして邪曲なる者の歡樂は時の間のみ
macheko ya mtu mwovu ni ya muda mfupi, nayo furaha ya wasiomcha Mungu hudumu kwa kitambo tu.
6 その高天に逹しその首雲に及ぶとも
Ingawa kujikweza kwake hufikia mbinguni na kichwa chake hugusa mawingu,
7 終には己の糞のごとくに永く亡絶べし 彼を見識る者は言ん彼は何處にありやと
ataangamia milele kama mavi yake mwenyewe. Wale waliomwona watauliza, ‘Yuko wapi?’
8 彼は夢の如く過さりて復見るべからず 夜の幻のごとく追はらはれん
Kama ndoto hutoweka, wala hapatikani tena, amefukuziwa mbali kama maono ya usiku.
9 彼を見たる目かさねてかれを見ることあらず 彼の住たる處も再びかれを見ること無らん
Jicho lililomwona halitamwona tena; mahali pake hapatamwona tena.
10 その子等は貧しき者に寛待を求めん 彼もまたその取し貨財を手づから償さん
Watoto wake watalipa yote baba yao aliyowadhulumu maskini, nayo mikono yake itarudisha mali yote aliyonyangʼanya watu.
11 その骨に少壯氣勢充り 然れどもその氣勢もまた塵の中に彼とおなじく臥ん
Nguvu za ujana zilizoijaza mifupa yake, zitalala naye mavumbini.
12 かれ惡を口に甘しとして舌の底に藏め
“Ingawa uovu ni mtamu kinywani mwake naye huuficha chini ya ulimi wake,
13 愛みて捨ず 之を口の中に含みをる
ingawa hawezi kukubali kuuachia uende, lakini huuweka kinywani mwake.
14 然どその食物膓の中にて變り 腹の内にて蝮の毒とならん
Hata hivyo chakula chake kitakuwa kichungu tumboni mwake, nacho kitakuwa sumu kali ya nyoka ndani yake.
15 かれ貨財を呑たれども復之を吐いださん 神これを彼の腹より推いだしたまふべし
Atatema mali alizozimeza; Mungu atalifanya tumbo lake kuzitapika.
16 かれは蝮の毒を吸ひ 虺の舌に殺されん
Atanyonya sumu za majoka; meno ya nyoka mwenye sumu kali yatamuua.
17 かれは蜂蜜と牛酪の湧て流るる河川を視ざらん
Hatafurahia vijito, mito inayotiririsha asali na siagi.
18 その勞苦て獲たる物は之を償して自ら食はず 又それを求めたる所有よりは快樂を得じ
Vile alivyovitaabikia atavirudisha bila kuvila; hatafurahia faida itokanayo na biashara yake.
19 是は彼貧しき者を虐遇げて之を棄たればなり 假令家を奪ひとるとも之を改め作ることを得ざらん
Kwa kuwa aliwaonea maskini na kuwaacha pasipo kitu; amenyangʼanya kwa nguvu nyumba asizozijenga.
20 かれはその腹に飽ことを知ざるが故に自己の深く喜ぶ物をも保つこと能はじ
“Hakika hatakuwa na raha katika kutamani kwake sana; hawezi kujiokoa mwenyewe kwa hazina zake.
21 かれが遺して食はざる物とては一も無し 是によりてその福祉は永く保たじ
Hakuna chochote kitakachosalia kwa ajili yake ili ale; kufanikiwa kwake hakutadumu.
22 その繁榮の眞盛において彼は艱難に迫られ 乏しき者すべて手をこれが上に置ん
Katikati ya wingi wa ustawi wake, dhiki itampata; taabu itamjia kwa nguvu zote.
23 かれ腹を充さんとすれば神烈しき震怒をその上に下し その食する時にこれをその上に降したまふ
Atakapokuwa amelijaza tumbo lake, Mungu ataionyesha ghadhabu kali dhidi yake, na kumnyeshea mapigo juu yake.
24 かれ鐡の器を避れば銅の弓これを射透す
Ijapokuwa aikimbia silaha ya chuma, mshale wa shaba utamchoma.
25 是に於て之をその身より拔ば閃く鏃その膽より出きたりて畏懼これに臨む
Atauchomoa katika mgongo wake, ncha ingʼaayo kutoka ini lake. Vitisho vitakuja juu yake;
26 各種の黑暗これが寳物ををほろぼすために蓄へらる 又人の吹おこせしに非る火かれを焚き その天幕に遺りをる者をも焚ん
giza nene linavizia hazina zake. Moto usiopepewa na mtu utamteketeza, na kuangamiza yaliyosalia nyumbani mwake.
27 天かれの罪を顯はし 地興りて彼を攻ん
Mbingu zitaweka wazi hatia yake, nayo nchi itainuka kinyume chake.
28 その家の儲蓄は亡て神の震怒の日に流れ去ん
Mafuriko yataichukua nyumba yake, maji yaendayo kasi katika siku ya ghadhabu ya Mungu.
29 是すなはち惡き人が神より受る分 神のこれに定めたまへる數なり
Hili ndilo fungu Mungu alilowagawia waovu, urithi uliowekwa kwa ajili yao na Mungu.”

< ヨブ 記 20 >