< Revelation 17 >

1 Sama tunno anyimo ibeu inu sanare andesa wa inta muso monu sunare mo ē magun “Aye inbezewe uweki utize udandang tuka dura uginome sama ciki azesere ma ē gbardang.
Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli saba akaja akaniambia, “Njoo, nitakuonyesha adhabu ya yule kahaba mkuu, aketiye juu ya maji mengi.
2 Ahira me ani agomo unee wa wuzi timumu ti madini nan ma nyimo utarsa umeme umadini mani wa wuna ti cukum tu nee wa humza”
Yule ambaye wafalme wa dunia walizini naye na watu wakaao duniani walilewa kwa mvinyo wa uzinzi wake.”
3 Ine ini bibeu bi kadura ka Asere bizikum anyimo abibeu bidusani ani ja, manno ma iri vannu eh ma ciki azesere abi nama ba'iro bivo mazin tize timadini. bina ma ba'iro me bazin tiye tinu sunare nan na hure anu kirau.
Kisha yule malaika akanichukua katika Roho akanipeleka jangwani. Huko nikamwona mwanamke mmoja ameketi juu ya mnyama mwekundu aliyejaa majina ya kumkufuru Mungu mwili mzima. Mnyama huyo alikuwa na vichwa saba na pembe kumi.
4 Uneme ma soki uzo wapo awalwalnan napo ina ma yaironan na azuma awal-wal. ma inta. iso yapo iwalwal atari tumeme nan timumu tizenzen gbardang nan tige sa anyara me tiniba nan madini mutarsa aneh.
Huyo mwanamke alikuwa amevaa mavazi ya rangi ya zambarau na nyekundu, akimetameta kwa dhahabu, vito vya thamani na lulu. Mkononi mwake alikuwa ameshika kikombe cha dhahabu kilichojaa mambo ya machukizo na uchafu wa uzinzi wake.
5 Abi timime anitiki nire niza anyimo ani hunzi “Ubabila nanu, a'ino amakaruwa nan nimum izenzen unēe.
Kwenye kipaji chake cha uso palikuwa pameandikwa jina: “Siri, Babeli Mkuu, Mama wa makahaba na wa machukizo ya dunia.”
6 Ma ira vana u ehme anyimo amaye ma desa wa nyara kadure nan maye mandesa a huza we a nyimo aniza ni Yeso, sa ma iri me, innu kunna biyau kang.
Nikaona kuwa huyo mwanamke alikuwa amelewa kwa damu ya watakatifu, yaani, damu ya wale watu waliouawa kwa ushuhuda wa Yesu. Nilipomwona huyo mwanamke, nilistaajabu sana.
7 Ine ini bibeume bagunmi, “Barki nyanizi ukunna biyau? inde bukiwe nigburang nu neh ugenome sa ma zen tiye usunare nan na hare anu kiraume.
Ndipo yule malaika akaniambia, “Kwa nini unastaajabu? Nitakufafanulia siri ya huyo mwanamke na huyo mnyama aliyempanda, mwenye vichwa saba na pembe kumi.
8 Biname be iro sawa hiri datti, aname biraniba, aname birani upuru aniwa nige sa nizome nubinani ba. Madi kunna iwano. Yan desa wa rani uneē, an desa a nyetike tiza tuwe me anyimo utakarda uvengize ba dati innu tuba unē-wade kunna biyau barki, uzetu ira ubi nama ba iro sawa rani datti ineni aname birani aname ba, aname ba aye ma mu aye. (Abyssos g12)
Huyo mnyama ambaye ulimwona, wakati fulani alikuwepo, lakini sasa hayupo, naye atapanda kutoka lile Shimo na kwenda kwenye maangamizo yake. Watu waishio duniani ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima tangu kuumbwa kwa ulimwengu watastaajabu kumwona huyo mnyama, kwa maana alikuwepo wakati fulani, na sasa hayupo, lakini atakuwepo. (Abyssos g12)
9 Imum iginome i nyara urusa, tiye sunare, tihira ti kon koron tinu sunare tini vanu eh me ma chikin.
“Hapa ndipo penye wito wa akili pamoja na hekima. Vile vichwa saba ni vilima saba ambavyo huyo mwanamke amevikalia.
10 We agomo anu sunare wani, agomo ucibi warezi, unu inde marani unu inde mamu aye ba, inka ma aye madi wuzi tichukum tu ganiya uhem.
Pia hivyo vichwa saba ni wafalme saba ambao miongoni mwao watano wamekwisha kuanguka, yupo mwingine hajaja bado, lakini atakapokuja, atalazimika kukaa kwa muda mfupi.
11 Iname ya iro sa ya rani datti, ine ini aname iraniba, mema ugomo mani unitutari me ugomo mani anyimo agomo sunare, madi dusa ma ka huza we.
Yule mnyama aliyekuwepo wakati fulani na ambaye sasa hayupo, yeye ni mfalme wa nane. Ni miongoni mwa wale saba, naye anakwenda kwenye maangamizi yake.
12 Ahure anu kirau sawa ira ahira agomo kirau wani andesa daki amu nyawe ba, wadi kabi ubari kasi agomo uganiya uginome anni nama ya iro.
“Zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme kumi ambao bado hawajapokea ufalme, lakini watapokea mamlaka kuwa wafalme kwa saa moja pamoja na yule mnyama.
13 Iriba iwe inde ini, wadi nya tigomo tuweme innu bezi iname yairo me.
Hawa wana nia moja, nao watamwachia yule mnyama nguvu zao na mamlaka yao.
14 Wadi wuzi nikono nan vana ubitam ba Asere vana ubitam ba Asere madi reje ahira awe me barki me Ugomo Asere anko co wani ugomo agomo nan desa atitame, nannu zauka”.
Watafanya vita na Mwana-Kondoo, lakini Mwana-Kondoo atawashinda kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme. Yeye atakuwa pamoja na watu wake walioitwa ambao ni wateule wake na wafuasi wake waaminifu.”
15 Bibeu me ba gunme, “Me sawa ira, ahira me sa ukaruwa me sama cikin me, anabu wani, nanni gura nigbardang, nan na nabu ati tem sasas.
Kisha yule malaika akaniambia, “Yale maji uliyoyaona yule kahaba akiwa ameketi juu yake ni jamaa, makutano, mataifa na lugha.
16 Ahure aginome sawa ira we nan ni nama yairome wadi nyari me ukaruwame, wadi samirka me wa ceki me nyenperen, wadi lenbika inama imeme, wadi punsime vat innura.
Zile pembe kumi ulizoziona, pamoja na huyo mnyama, watamchukia huyo kahaba, watamfilisi na kumwacha uchi, watamla nyama yake na kumteketeza kwa moto.
17 Ugomo Asere ma wuu amu ruba muweme wa wuzi ivai usuro uhem umeme, waweki urusa umeme wa wuzi uti gomo anicce nibi nama ba iro uhana uganiyame sa Ugomo Asere madi buki tize.
Kwa maana Mungu ameweka mioyoni mwao kutimiza kusudi lake kwa kukubali kumpa yule mnyama mamlaka yao ya utawala mpaka maneno ya Mungu yatakapotimia.
18 Uneme sa wa ira memani nipin nidandang me sama zin tigomo acce agomo unēe.
Yule mwanamke uliyemwona ni ule mji mkubwa unaotawala juu ya wafalme wa dunia.”

< Revelation 17 >