< Umatiyu 18 >

1 Uganiya uguno me anu tasa umeme wa eh ahira a yeso wa ikki me wagu, “Aveni ma teki unu gbadang anyimo ati gomo ta seseri?”
Wakati huo, wanafunzi wakamjia Yesu na kumuuliza, “Je, nani aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni?”
2 Ma titi vana ucin anyumo awe.
Yesu akamwita mtoto mdogo na kumsimamisha katikati yao.
3 Ma gu, kadundure inbo shi in daki ya kurzo ace ashi kasi ahana acicin ba ida ribe shi anyimo ati gomo ta seseri ba.
Naye akasema: “Amin, nawaambia, msipookoka na kuwa kama watoto wadogo, kamwe hamtaingia katika Ufalme wa Mbinguni.
4 Vat de sa daki ma zika nice anyo ire imum kasi vana ucin ugeme ba, mada ribe me ati gomo ta seseri ba.
Kwa hiyo mtu yeyote anyenyekeaye kama huyu mtoto, ndiye aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni.
5 Vat de sa makaba vana ucin kasi ugeme barki mi, i mani makaba.
“Yeyote amkaribishaye mtoto mdogo kama huyu kwa Jina langu, anikaribisha mimi.
6 Vat de sa ma wunā unu inde anyumo a hana ageme macara abangan sa wa hem in mi, idi teki a tirzi me unanzu udandang irir areki me anyumo uraba udandang uconcon.
Lakini kama mtu yeyote akimsababisha mmojawapo wa hawa wadogo wanaoniamini kutenda dhambi, ingekuwa bora kwake afungiwe jiwe kubwa la kusagia shingoni mwake, na kutoswa katika kilindi cha bahari.
7 Wa dee une barki ucara abangan ya cukuno gbass ucara ucara abanga u eh, de sa ma wuna una me ma dee.
“Ole kwa ulimwengu kwa sababu ya yale mambo yanayosababisha watu kutenda dhambi! Mambo hayo lazima yawepo, lakini ole wake mtu yule ambaye huyasababisha.
8 Nyoro ubuna nan tari tuwe me u vetten ingi ti wuza we ucara abangan iteki uriba ati gomo ta seseri inu buna u inde nan tari ti inde wanu guna areki we anyumo ura uzatu umara inti buna tuwe tire nan tari tire. (aiōnios g166)
Ikiwa mkono wako au mguu wako unakusababisha utende dhambi, ukate na uutupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa huna mkono mmoja au mguu mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili, na kutupwa katika moto wa milele. (aiōnios g166)
9 Ingi nije wuwe upilko kara nini uveten, iteki uribe ati gomo ta seseri in nije ni inde innu areki we anyumo ura in naje arere. (Geenna g1067)
Nalo jicho lako likikusababisha kutenda dhambi, lingʼoe, ulitupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili lakini ukatupwa katika moto wa jehanamu. (Geenna g1067)
10 Hirani kati i izi unu inde anyumo ahana acicin wa geme ba, in bo shi ibe ikadura ka Asere aweme aseseri wa hira muhenu maco um de sa mara anyumo aseseri.
“Angalia ili usimdharau mmojawapo wa hawa wadogo, kwa maana nawaambia, malaika wao mbinguni daima wanauona uso wa Baba yangu aliye mbinguni. [
11 I rusa vana unu ma aye barki ma buri an de sa wa hunne we.
Kwa maana Mwana wa Adamu alikuja kuokoa kile kilichopotea.]
12 I bassa ingi urunu mazin ini tam ini ni ino bi inde ba hunne me i hira mada ceki me ukasu me ma dusa unyara ubi inde me ba?
“Mwaonaje? Ikiwa mtu ana kondoo mia moja, na mmoja wao akapotea, je, hatawaacha wale tisini na tisa vilimani na kwenda kumtafuta huyo mmoja aliyepotea?
13 Ingi ma tinka bini, iruba ime me idi rume i teki unu ni, ino uzati ubi inde me.
Naye akishampata, amin, nawaambia, hufurahi zaidi kwa ajili ya huyo kondoo mmoja kuliko wale tisini na tisa ambao hawakupotea.
14 Ani me ani aco ushi me sa ma rani anyumo aseseri mada nyarā me unu inde anyumo a hana acincin wa geme mahunne ba.
Vivyo hivyo, Baba yenu wa mbinguni hapendi hata mmojawapo wa hawa wadogo apotee.
15 Ingi u hennu uwe me macara we abanga, hana uka buka me hu nan me, ingi makunna we wa bura me.
“Kama ndugu yako akikukosea, nenda ukamwonyeshe kosa lake, kati yenu ninyi wawili peke yenu. Kama akikusikiliza, utakuwa umempata tena ndugu yako.
16 Ingi daki makunna we ba nyara unu inde utizi anyo ana ware nan watara ikeki.
Lakini kama hatakusikiliza, nenda na mtu mwingine mmoja au wawili ili kila neno lithibitishwe kwa ushahidi wa mashahidi wawili au watatu.
17 Ingi daki makunna we ba, ubuki anu tarsa Asere ingi magame ukunna anu tarsa Asere uziki me de sa ma tame Asere nan unu cara abangan sa magame ubarka.
Kama akikataa kuwasikiliza hao, liambie kanisa. Naye kama akikataa hata kulisikiliza kanisa, basi awe kwenu kama mtu asiyeamini au mtoza ushuru.
18 Kadundura inbo shivatti imum me sa ya tira une izin nutira aseseri imum be sa ya sopo aseseri.
“Amin, nawaambia, lolote mtakalolifunga duniani litakuwa limefungwa mbinguni, na lolote mtakalolifungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.
19 In kuri inbu shi, ingi anu ware anyumo ashi me une wa hem wa iko ire imum, aco um sa marani anyumo aseseri madi nya we.
“Tena nawaambia, ikiwa wawili wenu watakubaliana duniani kuhusu jambo lolote watakaloomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.
20 Barki vat ahira me sa ana ware nani wataru gurnan izi na we.
Kwa kuwa wanapokusanyika pamoja watu wawili au watatu kwa Jina langu, mimi niko papo hapo pamoja nao.”
21 Ara anyumo anime Bitrus ma eh ma gun yeso, ugomo Asere kani ka hono kani uhenu um madi carrum iruban in vette? kanu sunare?
Ndipo Petro akamjia Yesu na kumuuliza, “Bwana, ndugu yangu anikosee mara ngapi nami nimsamehe? Je, hata mara saba?”
22 Yeso ma gun inzo kanu sunare ba akuru sunare kanu sunare.
Yesu akamjibu, “Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.
23 Barki ani me adi bati tigomo ta seseri nan urugomo sa ma nyara ma bassa ucira ume me atari tarere ame me.
“Kwa hiyo Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme aliyetaka kufanya hesabu zake za fedha na watumishi wake.
24 Sa ugomo me mara anyumo ubassa me a eh mu reme wazurta sa matarsa me uge sa mada ke makurzo ba vat uciki ume une.
Alipoanza kufanya hesabu zake, mtu mmoja aliyekuwa anadaiwa talanta10,000, aliletwa kwake.
25 Sa madira ukurzo men, ugono magu azizi me nan une me wanna hana me vat nan imum me sa mazin akurzo ikirfi men.
Kwa kuwa alikuwa hawezi kulipa deni hilo, bwana wake akaamuru kwamba auzwe, yeye, mkewe, watoto wake na vyote alivyokuwa navyo, ili lile deni lipate kulipwa.
26 Urere matunguno ma gun me nata iruba indi kurzo we kondi nyanin.
“Yule mtumishi akampigia magoti, akamsihi yule bwana akisema, ‘Naomba univumilie, nami nitakulipa deni lako lote.’
27 Ugomo me makunna ugogoni urere me maceki me ma ceki ureme me.
Yule bwana wa huyo mtumishi akamwonea huruma, akafuta deni lake lote, akamwacha aende zake.
28 Sa ma suro magurna nan ure uroni me sa matarsa me ureme ikiirfi cin ma tappi me iriri ma gu nyam imumme sa in tarsa we.
“Lakini yule mtumishi alipokuwa anatoka nje, akakutana na mtumishi mwenzake aliyekuwa amemkopesha dinarimia moja. Akamkamata, akamkaba koo akimwambia, ‘Nilipe kile ninachokudai!’
29 Uroni me matunguno ma gun me nata iruba indi kurzo wen.
“Yule mtumishi mwenzake akapiga magoti akamsihi akisema, ‘Naomba univumilie, nami nitakulipa deni lako lote.’
30 Urere me ma ga me mahan unu rani me akura ani rere, agi makurzo men.
“Lakini akakataa. Badala yake, alienda akamtupa gerezani hata atakapolipa hilo deni.
31 Sa aroni akatuma wakunna imum me icari we muruban wa kurzo ugomo imum nan.
Watumishi wenzake walipoona haya yaliyotukia wakaudhika sana, nao wakaenda na kumwambia bwana wao kila kitu kilichokuwa kimetukia.
32 Ugomo matiti me ma gun me gu unu ubur mani, ma ceki vat imum me sa imtarsa sa wa tizom.
“Yule bwana akamwita yule mtumishi akamwambia, ‘Wewe mtumishi mwovu! Mimi nilikusamehe deni lako lote uliponisihi.
33 Daki ya wuna inu ukunna ugogoni uroni akatuma kawe ba?
Je, haikukupasa kumhurumia mtumishi mwenzako kama mimi nilivyokuhurumia wewe?’
34 Ugomo makunna iruba kang ma gu anyame titere makurzo vat ureme sa matarsa me.
Kwa hasira, yule bwana wake akamtia yule mtumishi mikononi mwa askari wa gereza ili ateswe mpaka atakapolipa yote aliyokuwa anadaiwa.
35 Ani me ani aco um sa marani anyuno aseseri madi wuzi vat de sa ma nyari me uceki uhenu umeme ini ruba ka inde.
“Hivi ndivyo Baba yangu wa mbinguni atakavyomfanyia kila mmoja wenu ikiwa hatamsamehe ndugu yake kutoka moyoni mwake.”

< Umatiyu 18 >