< Umarkus 1 >
1 U tuba uka dura kurunta ka Yesu vana Asere.
Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2 Kasi unu kurzo tize ta sere Ishaya ma nyetike “ira, “indi tuburko we una kadura a hira awe me, meh mani madi barka we uname.”
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako”:
3 “Akunna nimyera nu uye ani jaa, 'unu tisa, cukuno unu rusa anu nan Ugomo Asere, hakani una umeme dert'”.
“sauti ya mtu aliaye nyikani. ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’”
4 Yohana ma eh ma zorso anu anyimo anijaa makuri ma beziwe una uzorso me nannu guna wa ceki a cara abanga a zenzen barki akabiwe usuro abanga aburume.
Yohana alikuja, akibatiza huko nyikani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
5 Vat nipin nu Judiya nan anu Urushalima, wasuri wa ha ahira ameme manno ma zorowe uraba u Juda. sawabuki uguna wa ceki a banga a buru aweme.
Watu kutoka Uyahudi wote na sehemu zote za Yerusalemu walikuwa wakimwendea. Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
6 Yohana ma soki u dibi utiwui unu subu urakumi ma kuri ma tirzi utinome ini wa imimare imeme yazi matu mishii ini jaa.
Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
7 Maboo tize ti Ugomo Asere maguwe uye ma eze sa ma tekum ini kara mi indaki mabari uguna in tunguno in sopi be nyumo ba kpatak ameme.
Naye alihubiri akisema, “Baada yangu atakuja yeye aliye na uwezo kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kuinama na kulegeza kamba za viatu vyake.
8 Mima zoroshi imgwei me madi zorsoshi inbibe beriri.
Mimi nawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
9 Anyimo atiye tigonome tine Yesu ma suri Unazarat anyimo Ugalili Yohana mani ma zoro me uraba Ujorda.
Wakati huo Yesu akaja kutoka Nazareti ya Galilaya, naye akabatizwa na Yohana katika Mto Yordani.
10 Sa Yesu ma suro agwei me, Asesere a pokino bibe biriri ba Asere bi tu anipum nimeme gusi bihurge
Yesu alipokuwa akitoka ndani ya maji, aliona mbingu zikifunguka na Roho akishuka juu yake kama hua.
11 Sa nimyrang na suro Asesere. Hu, vana um mani sa inteki unu nyara me. in kunna urunta uweme.
Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
12 Abinime bibe biziki me bi hamme ani jaa.
Wakati huo huo, Roho akamwongoza Yesu kwenda nyikani,
13 Ma cukuno ani jaa me tiye tina akura nazi, una bi be bizenzen ma eh ma mansame, maciki ni gome nan ni nama ini jaa una katuma ka Asere ma nyinzi me imum besa manyara.
naye akawa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikaa na wanyama wa mwituni, nao malaika wakamhudumia.
14 Uganiya sa a meki Yohana Yesu ma ennu boo anu tize ka Asere.
Baada ya Yohana kukamatwa na kutiwa gerezani, Yesu aliingia Galilaya akaanza kuhubiri habari njema ya Mungu,
15 Magu ana uganiya wa aye ma saa mu Ugomo Asere ma aye mamu. hem mi ikabi tize tum.
akisema, “Wakati umewadia, Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema.”
16 Madusa ani kira nu raba udan Ugalili, ma iri Siman nan Andrawus uhenu u Siman wazi ma hurba uraba me. wazi numensi icere.
Yesu alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
17 Yesu ma guwe aye tarsan nimi indi wushi anu mensi anabu.
Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
18 Wa ba ceki ma hurba me wa tarsi me.
Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.
19 Mara anyimo a tanu ma iri Yakubu vana u Zabadi nan Yohana uhenume. wah ra anyimo ujirgi umgwei unu urezi umakoma.
Alipokwenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20 Matiti we, wa dusa waba ceki acho awe me Zabadi anyimo ujirgi umgwei me wa tarsi me.
Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Yesu.
21 Ma haki a nyimo Ukaparnahum Asabar adusa a ribe, me ma ka ribe a nyimo udenge unigura ma boo tize ta Asere. Wa kunna biyau inni mumbe sa ba we wa
Wakaenda mpaka Kapernaumu. Ilipofika siku ya Sabato, mara Yesu akaingia sinagogi, akaanza kufundisha.
22 ziki me debe sa mazin nikara azoh gusi debe sa ma bezizi abanga.
Watu wakashangaa sana kwa mafundisho yake, kwa maana aliwafundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wa sheria.
23 A nyimo udenge unigura me uye mara ni in bibe bizenzeng. Maha ma wu uhunu gangang.
Wakati huo huo katika sinagogi lao palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu,
24 Nyanini tidi wuzi in hu Yeso una nu nazareth? Wa aye uhuzin duru? Marusa we hu bibe ba Asere bini.
naye akapiga kelele akisema, “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
25 Yeso ma busurka ugbergene me magu, ingara u suri abini me.
Lakini Yesu akamkemea, akamwambia, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!”
26 Abini me bibe bi zenzeng me bi vete me adizi bi yeze nigmirang gangang bi ku sura me.
Yule pepo mchafu akamtikisatikisa huyo mtu kwa nguvu, kisha akamtoka akipiga kelele kwa sauti kubwa.
27 vat anu wa kunna biya, wa ikki nya nini izigeme, uboo abanga asoh nan ni kara! Mayenne anu ibe zenzeng wa yenne wa kunna me.
Watu wote wakashangaa, hata wakaulizana wao kwa wao, “Haya ni mambo gani? Ni mafundisho mapya, tena yenye mamlaka! Anaamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
28 Abini me abanga adusa a ribize vat a nyimo nan matara mu Galili.
Sifa zake zikaanza kuenea haraka katika eneo lote la karibu na Galilaya.
29 A hira me sa wa ceki udenge unigura me, wa ribe anyimo a kura Simon wan Andarawus an Yakubu nan Yohana.
Mara walipotoka katika sinagogi, walikwenda pamoja na Yakobo na Yohana hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea.
30 Ugiri u Simon marari innipum ba wa buki me abanga ameme.
Mama mkwe wa Simoni alikuwa kitandani, ana homa, nao wakamweleza Yesu habari zake.
31 Ba amini me ma meki tari ma hirza me. ma ba huma. ma ziki imumare ma nyawe.
Hivyo Yesu akamwendea, akamshika mkono na kumwinua. Kisha homa ikamwacha, naye akaanza kuwahudumia.
32 Unnu wunjoro, wa ezime inna na tikoni nan bibe sa agbergene wa ribe we.
Jioni ile baada ya jua kutua, watu wakamletea Yesu wagonjwa wote na waliopagawa na pepo wachafu.
33 ni pin me ni gurna vat ana tukum.
Mji wote ukakusanyika mbele ya nyumba hiyo.
34 ma humza vat ana tikoni sassas ma kuri ma suzo agbergene wa buki tize barki wa rusi me.
Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa ya aina mbalimbali. Akawatoa pepo wachafu wengi, lakini hakuwaacha hao pepo wachafu waseme, kwa sababu walimjua yeye ni nani.
35 Ma suri nisssizo maka wuna biringara in sissimme.
Alfajiri na mapema sana kulipokuwa bado kuna giza, Yesu akaamka, akaondoka, akaenda mahali pa faragha ili kuomba.
36 Siman nan bibe sa wa zi nigome wa nyarime.
Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta,
37 Wa dusa wa iri me a hira sa ma rani. sa wa ira me, wa gu imme, anabu wa zin innu nyara uwe.
nao walipomwona, wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta!”
38 Ma guna taru ni, arahira a ninjo a nipin imbuki we tize abini me cangi. Imumbe sa ya en me ya zigino me.
Yesu akawajibu, “Twendeni mahali pengine kwenye vijiji jirani, ili niweze kuhubiri huko pia, kwa sababu hicho ndicho nilichokuja kukifanya.”
39 Ma dusa vat a nyimo uGalili, ma boo tize ta Asere a nyimo a tidenge ti nigura, ma suzo a gbergene.
Kwa hiyo akazunguka Galilaya kote, akihubiri katika masinagogi yao na kutoa pepo wachafu.
40 Uku taru maka aye ma tun guno inna ruu, magu imme ana inki wa hem uhuman.
Mtu mmoja mwenye ukoma alimjia Yesu, akamwomba akipiga magoti, akamwambia, “Ukitaka, waweza kunitakasa.”
41 Ma ngwimca innu gogoni, Yeso ma yeze tari timeme ma dari me, magu inn zinnu su me, magu, huma.
Yesu, akiwa amejawa na huruma, akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Nataka. Takasika!”
Mara ukoma ukamtoka, naye akatakasika.
43 Yeso ma gu imme innki wa buka uye abanga agino adi huwe, dusa ana me. Yeso ma gu imme hana kati ubuki uye iri mum.
Baada ya Yesu kumwonya vikali, akamruhusu aende zake
44 Ka nya una katuma ka Asere udanga me, umm be sa Musa mabuki we unnu guna wuzi ini.
akimwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote habari hizi, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
45 Ba unu me ma tunguno ubo anabu imum me vat. Abini ani Yeso ma diri ace usuro a nipin. Ma dusa maka cukuno a manyanga ma huu im bikki cas barki anu wa nyarai me.
Lakini yule mtu akaenda akaanza kutangaza habari za kuponywa kwake waziwazi. Kwa hiyo, Yesu hakuweza tena kuingia katika miji waziwazi lakini alikaa sehemu zisizo na watu. Hata hivyo watu wakamfuata huko kutoka kila upande.