< Uyuhana 3 >
1 Urunu marane neza numeme nikodimo memani unaje wa yahudawa.
Kulikuwa na kiongozi mmoja Myahudi, wa kikundi cha Mafarisayo, jina lake Nikodemo.
2 Unu uginome ma e ahira a yeso in niye magunmme hu una jetirusa hu unu rusamani sa wa e ahire asere, barki unu rusa wuza katuma kawe ma maraneba, de be sa mazi nigo nan na Asere memani madi uiuzi kani.”
Siku moja alimwendea Yesu usiku, akamwambia, “Rabi, tunajua kwamba wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, maana hakuna mtu awezaye kufanya ishara unazozifanya Mungu asipokuwa pamoja naye.”
3 Yeso makabirka me magu aneni inzinu bezi uwe in kadaki akuri ayo unububa mada irame akura asere be.
Yesu akamwambia, “Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa upya hataweza kuuona ufalme wa Mungu.”
4 Nikodimo magun me adi wo aneni ayo unubu sama uiuna ucokoro? ani madi kuri maribe aburu aino meme makuri mayome?”
Nikodemo akamwuliza, “Mtu mzima awezaje kuzaliwa tena? Hawezi kuingia tumboni mwa mama yake na kuzaliwa mara ya pili!”
5 Yeso makabirka me magu, “Inkadaki ayo unubu usuro ugmei nan bibe ba asere ba mada ribeneme akura asere ba.
Yesu akamjibu, “Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa kwa maji na Roho, hawezi kamwe kuingia katika ufalme wa Mungu.
6 Immum be sa unubu mayo unubu mani, imum be sa bibe ba yo bibe bini.
Mtu huzaliwa kimwili kwa baba na mama, lakini huzaliwa kiroho kwa Roho.
7 Kati icukuno we imum itize barki sa ma guna ya cukuno gbas akuri ayo we.
Usistaajabu kwamba nimekwambia kuwa ni lazima kuzaliwa upya.
8 Ueebu usuma uhama ahira iriba u uni uduki u kunna tanu tu uni utame ahira sa wasuroni uyami ahira me sa uhazani, anima izi ahira ade be sa bibe ba yo me.”
Upepo huvuma kuelekea upendako; waisikia sauti yake, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda. Ndivyo ilivyo kwa mtu aliyezaliwa kwa Roho.”
9 Nikodimo ma kabirka me magu, “Aneni idi cukuno?”
Nikodemo akamwuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”
10 Yeso ma kabirka me magu hume sa uzi unu bezi ihori anyimo isra'ila daki wa rusa ani me ba?
Yesu akamjibu, “Je, wewe ni mwalimu katika Israel na huyajui mambo haya?
11 Ine ini inzin nu gusan hu, imumbe sa tirusa ine ini ta buka we tizin nu kuri ubizi imumbe sata ira yagashi uhem inni mumbe sata bezi.
Kweli nakwambia, sisi twasema tunayoyajua na kushuhudia tuliyoyaona, lakini ninyi hamkubali ujumbe wetu.
12 Izi nu uboo ushi abanga uneh da hem ni ba, indi wa aneni i hem in na banga atize ta zezzere?
Ikiwa nimewaambieni mambo ya kidunia nanyi hamniamini, mtawezaje kuamini nikiwaambieni mambo ya mbinguni?
13 Avene mamu nyene azesere in daki memani de be sa matuu usuro azezze abanname me mani vana unu be sa marani azezzere me.
Hakuna mtu aliyepata kwenda juu mbinguni isipokuwa Mwana wa Mtu ambaye ameshuka kutoka mbinguni.
14 Kasi musa sama yeze biwa, biginome ani ja'a, ane ani adi yeze vana unubu.
“Kama vile Mose alivyomwinua juu nyoka wa shaba kule jangwani, naye Mwana wa Mtu atainuliwa juu vivyo hivyo,
15 Barki vat desa ma hem in me madi kem uvenke uzatu umara. (aiōnios )
ili kila anayemwamini awe na uzima wa milele. (aiōnios )
16 Barki uhemme sa ugomo asere mawu uneh men madusa ma nya vana uinde ugino me, barki vat debe sama kaba me kati macorno me, idi cukono me madi kem venke uzatu umarsa. (aiōnios )
Maana Mungu aliupenda ulimwengu hivi hata akamtoa Mwana wake wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (aiōnios )
17 Ugomo asere matubarka vana umeme uneh ugeme barki agi ma weki tize tini ba manyari uneh ukem ukaba ahira amame.
Maana Mungu hakumtuma Mwanae ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali aukomboe ulimwengu.
18 Vat debe sama hem me, ada weke me tize ba vat debe sa ma nyari me uhem in niza nu vana u inde ugino ugomo asere.
“Anayemwamini Mwana hahukumiwi; asiyemwamini amekwisha hukumiwa kwa sababu hakumwamini Mwana wa pekee wa Mungu.
19 U weki utize teki u yenne masa'a mariba uneh anabu wa taki unu nyara u mareu nan kani.
Na hukumu yenyewe ndiyo hii: Mwanga umekuja ulimwenguni lakini watu wakapenda giza kuliko mwanga, kwani matendo yao ni maovu.
20 Vat de sa ma wuza imum izenzen ma nyar si me masa'a me nyani agu ma hanaa hira anmasa'a me barki kati a iri katuma ka zenze ka meme.
Kila mtu atendaye maovu anauchukia mwanga, wala haji kwenye mwanga, maana hapendi matendo yake maovu yamulikwe.
21 Unu uwuza ukadura me mani madike ma-e ahira a masaa me, barki masuso tize timeme, unuguna, ugomo asere mani mawuna ini.
Lakini mwenye kuuzingatia ukweli huja kwenye mwanga, ili matendo yake yaonekane yametendwa kwa kumtii Mungu.”
22 Yeso nan nahana akatuma kameme wa dusa amanyanga mu yahudiya abinime madii nan we mazi nu zarso anabu.
Baada ya hayo, Yesu alifika mkoani Yudea pamoja na wanafunzi wake. Alikaa huko pamoja nao kwa muda, akibatiza watu.
23 Yahaya mazin nu zorso anabu uainon mamamun nan nu salima barki gmei marani gbardan ahira me anabu wa ezi azorsowe.
Yohane pia alikuwa akibatiza watu huko Ainoni, karibu na Salemu, maana huko kulikuwa na maji mengi. Watu walimwendea, naye akawabatiza.
24 Barki anime da amu hanan yahaya udenge uni rereba.
(Wakati huo Yohane alikuwa bado hajafungwa gerezani.)
25 Abineme ana katuma ka yahaya wa meki matara nan ure u yahude ahira a tize tumeki unicce.
Ubishi ulitokea kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohane na Myahudi mmoja kuhusu desturi za kutawadha.
26 Wakuri wa eh ahira a yahaya, wagunmme desa dati wazi wazi nanme, urusa u urdun me, desa hu necce nu we wabezi urusa ume, manno mazin nu zorso anabu ine ini anabu wazin nu haza ahira ameme.
Basi, wanafunzi hao wakamwendea Yohane na kumwambia, “Mwalimu, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ng'ambo ya Yordani na ambaye wewe ulimshuhudia, sasa naye anabatiza, na watu wote wanamwendea.”
27 Yahaya ma kabirka magu in daki anya unu imum ahira a sere unu ukem ini mazoni.
Yohane akawaambia, “Mtu hawezi kuwa na kitu asipopewa na Mungu.
28 Shi acce ashime irusa uguna ana azo mimani asere me, mi a tuburkon ini a je ameme.
Nanyi wenyewe mwaweza kushuhudia kuwa nilisema: Mimi siye Kristo, lakini nimetumwa ili nimtangulie!
29 Una anya memani unu unee uso uroni unu nee sa ma turi, magunna tize timeme, ma wuza apuru arom kgan innu kunna uni gmirang ni manyani manya me, barki ani me iriba iram in ya gminca.
Bibiarusi ni wake bwanaarusi, lakini rafiki yake bwana arusi, anayesimama na kusikiliza, hufurahi sana anapomsikia bwana arusi akisema. Ndivyo furaha yangu ilivyokamilishwa.
30 Me madingi ukingizi mi, indii unu kaza unupum.
Ni lazima yeye azidi kuwa maarufu, na mimi nipungue.
31 Unu aye usuro azesere marani azesere nan na nabu desa marani adizii me una dizzii mani tize ta dizii tini mawuza, unu uayye azezere mara azezere a ko de avi.
“Anayekuja kutoka juu ni mkuu kuliko wote; atokaye duniani ni wa dunia, na huongea mambo ya kidunia. Lakini anayekuja kutoka mbinguni ni mkuu kuliko wote.
32 Imum be sama kunna ma kuri ma ira, ine ini mazin nukurzo men, vat anime anu wa game imum be sa mazi nu boo me.
Yeye husema yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna mtu anayekubali ujumbe wake.
33 Vat desa mahem ini mum be sa maboo makuri, matunno azezzere ani uguna ugomo Asere una kadura mani.
Lakini mtu yeyote anayekubali ujumbe wake anathibitisha kwamba Mungu ni kweli.
34 Barki desa ugomo asere matu mime, abanga ugomo asere ani maboo, ugomo asere ma nyinza bibe bizatu ubinani.
Yule aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, maana Mungu humjalia mtu huyo Roho wake bila kipimo.
35 Acome ma hem invana me makuri mawu vat imum atari ti meme.
Baba anampenda Mwana na amemkabidhi vitu vyote.
36 Desa ma hem invaname mazin nu venke uzatu ubinani. De be sa ma game vana me, mada kem me uvenke ugino me, madi ribe anyimo iriba ugomo Asere. (aiōnios )
Anayemwamini Mwana anao uzima wa milele; asiyemtii Mwana hatakuwa na uzima wa milele, bali ghadhabu ya Mungu hubaki juu yake.” (aiōnios )