< 1 Ukorontiyawa 7 >
1 Barki timumu sa anyetike, “Ya wuna uree unubu kati ma dari uneh ba.”
Basi kuhusu mambo yale mliyoyaandika: Ni vyema mwanaume asimguse mwanamke.
2 Barki timumu ti madini sa ta wuna gbardang, ya wuna uri kondi uya yana uruma macukono nan uneh ume kondi uya uneh macukuno nan uruma ume.
Lakini ili kuepuka zinaa, kila mwanaume na awe na mke wake mwenyewe na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe.
3 Kondi uya unakuru ma nya uneh umeme Imum be sa ma nyara, kondi uya uneh ma nya uruma, umeme Imum inyra inipum.
Mume atimize wajibu wake wa ndoa kwa mkewe, naye vivyo hivyo mke kwa mumewe.
4 Uneh mazo inu bezi ini pum nume ba urama mani inipum nu neh um, ane ani, uruma mazo unu bezi ini pum nume ba uneh me mani.
Mwanamke hana mamlaka juu ya mwili wake bali mumewe, wala mume hana mamlaka juu ya mwili wake bali mkewe.
5 Kati in Karti ace ashi inapum ashe ba, se inka konde avi ma hem, wuza ani me barki ibenki ance in biringara iduku saku ugur na, barki kati bibe bi buru bi rangi shi barki uzatu meki ace ashi me.
Msinyimane, isipokuwa mmekubaliana kufanya hivyo kwa muda fulani ili mweze kujitoa kwa maombi, kisha mrudiane tena ili Shetani asije akapata nafasi ya kuwajaribu kwa sababu ya kutokuwa na kiasi.
6 In boshi anime barki kati imum me icorno me, azo ma wuna shi ba.
Nasema haya kama ushauri na si amri.
7 Ma nyara ko da vi macukuno kasi mi, barki ani me koda vi mazi nu aye urizo ume, uye mazi nu sanda urizo uge uye ugino.
Laiti watu wangekuwa kama mimi nilivyo. Lakini kila mtu amepewa kipawa chake kutoka kwa Mungu, mmoja ana kipawa cha namna hii na mwingine ana cha namna ile.
8 Ahira anu zatu anyah nan anu zatu anu ruma, ya wuna uree wa cukuno sarrki anyah, kasi uzina um.
Kwa wale wasiooa na kwa wajane, nasema hivi, ingekuwa vizuri wasioe.
9 Barki anime inka wada ke wa meki ace awa ba, ya wuna uree wa wuzi anyah, Iteki uni ree wa wuza anyah inu guna wa ceki gmei ma aje.
Lakini kama hawawezi kujizuia, basi waoe na kuolewa, kwa maana ni afadhali kuoa au kuolewa kuliko kuwaka tamaa.
10 Ahira ana tinyah, in nyiza ti tize ti ge me - azo me ba, ugomo Asere mani “Kati uneh ma ceki uruma ume ba”.
Kwa wale waliooana nawapa amri (si mimi ila ni Bwana): Mke asitengane na mumewe.
11 In ka ma ceki uruma umeme, ca ma cukuno sarki anyah nyami ma barka nan uruma umeme, ane ani kati uruma, “ma ceki u me ba.
Lakini akitengana, ni lazima akae bila kuolewa, ama sivyo apatane tena na mumewe. Wala mume asimpe mkewe talaka.
12 Ahira ukasu anu in gusa azo Asere ba inka ure uhena mazin uneh azo unu tarsa Asere ba, Inka ma hem ma cukuno nan me kati ma ceki me ba.
Lakini kwa wengine nasema (si Bwana ila ni mimi): Kama ndugu ana mke asiyeamini, naye huyo mke anakubali kuishi pamoja naye, basi asimwache.
13 Inka uneh mazin unu ruma unu zatu tarsa Asere, In ka ma hem ma cukuno nan me, kati ma game uwuza anya nan me ba.
Naye mwanamke aaminiye kama ameolewa na mwanaume asiyeamini na huyo mume anakubali kuishi naye, basi huyo mwanamke asimwache.
14 Uruma unu zatu ukuba Asere ma cukuno a inko sas barki uneh ume me, uneh uzatu ukabe Asere ma cukuno a inko barki uruma umeme unu kaba Asere barki ane ba ahana ashime wa cukuno ana madini, barki anime we anu inko wani.
Kwa maana huyo mume asiyeamini anatakaswa kupitia mkewe, naye mke asiyeamini anatakaswa kupitia mumewe anayeamini. Kama isingalikuwa hivyo watoto wenu wangalikuwa si safi, lakini ilivyo sasa wao ni watakatifu.
15 Barki ani inka uroni unu zatu tarsa Asere ma suro, ca a ceki me ma suri, usanda imum igino me, uhenu uruma nan uhenu u eh azo atiri ziza we ini unu mko utize tuwe ba, Asere a titan duru ti cukuno anyimo a masaa.
Lakini kama yule asiyeamini akijitenga, basi afanye hivyo. Katika hali kama hiyo mwanamke au mwanaume aaminiye hafungwi, kwa sababu Mungu ametuita tuishi kwa amani.
16 Ane ni urusa awu uneh, ma madi buri uruma uwe me? Nani aneni huu uruma udi buri uneh uweme?
Wewe mke, unajuaje kama utamwokoa mumeo? Au wewe mume unajuaje kama utamwokoa mkeo?
17 Ca konda avi ma wuzi Imum besa ugomo Asere a inko me, ane ani Asere atita me, Ine ni ubuka a ko di uya udenge Asere.
Lakini kila mtu na aishi maisha aliyopangiwa na Bwana, yale Mungu aliyomwitia. Hii ni sheria ninayoiweka kwa makanisa yote.
18 Unu mazin nigbari uganiya sa a titi me ukaba Asere? Kati ma wuzi dibe ukunna utize, unu mazo me ini gbari uganiya a titi me ukaba utize? Kati ma nyari nigbari.
Je, mtu alikuwa tayari ametahiriwa alipoitwa? Asijifanye asiyetahiriwa. Je, mtu alikuwa hajatahiriwa alipoitwa? Asitahiriwe.
19 Nigbari nan uzatu unigbari azo ine ini anyara ba, Imum Idang me ine ukunna utize nan u inko utize ta Asere.
Kutahiriwa si kitu, na kutokutahiriwa si kitu. Lakini kuzitii amri za Mungu ndilo jambo muhimu.
20 Konde avi ma tunno anyimo utita sa Asere atitime uganiya sa ma kabi tize ta Asere.
Basi kila mmoja wenu na abaki katika hali aliyoitwa nayo.
21 Huu urere mani uganiya sa Asere a titi we? Kati u inki iriba in aneba, inka uzin unu ira upitii kati uwuzi ane ba.
Je, wewe ulipoitwa ulikuwa mtumwa? Jambo hilo lisikusumbue. Ingawaje unaweza kupata uhuru, tumia nafasi uliyo nayo sasa kuliko wakati mwingine wowote.
22 Barki desa Asere atiti me uganiya sa mazi urere, ma buru we Asere ane ani desa abura me uhana ukaba Asere, urere Asere mani akwa shi ini kirfi idang barki kati icukuno arere anabu.
Kwa maana yeyote aliyeitwa katika Bwana akiwa mtumwa yeye ni mtu huru kwa Bwana, kama vile yeyote aliyekuwa huru alipoitwa yeye ni mtumwa wa Kristo.
23 A kpi shi in nu kalu kati icukuno arere anuba.
Mlinunuliwa kwa gharama; msiwe watumwa wa wanadamu.
24 Anu henu ukodi ya uganiya sa ko da avi uru ma ra anyimo a titi duru uhana kaba utize ta Asere, ca ti cukono anime.
Ndugu zangu, kama kila mtu alivyoitwa, akae katika wito wake alioitiwa na Mungu.
25 Andesa da wamu wuza anyah ba, inzom un ure ubuku ba in ani me ingusa desa a hira anipum na Asere, icukuno ani me.
Basi, kuhusu wale walio bikira, mimi sina amri kutoka kwa Bwana, lakini mimi natoa shauri kama mtu ambaye ni mwaminifu kwa rehema za Bwana.
26 Barki ani me in hira barki tize ti buru sa ti hana azo inu dadon kino ba, ya wuna uri inu ma cukuno anime.
Kwa sababu ya shida iliyoko kwa sasa, naona ni vyema mkibaki kama mlivyo.
27 Wa tira vanu eh? Kati unyari ubuka ahira ameme, Da wa tira vanu eh? Kati unyari anya nan vanu eh.
Je, umeolewa? Basi usitake talaka. Je, hujaoa? Usitafute mke.
28 Barki anime inka wa wuza anya da wa wuza inium imadini ba, in ka vanu eh unu zata anya ma wuza anya, da ma wuza madini ba, in ka vanu eh unu zata anya ma wuza anya, da ma wuza madini ba, se andesa wa wuza anya wadi ziti sasas uganiya sa wa zin ini vai, in kuri inyari uhara uwe.
Lakini kama ukioa, hujatenda dhambi; na kama bikira akiolewa, hajatenda dhambi. Lakini wale wanaooa watakabiliana na matatizo mengi katika maisha haya, nami nataka kuwazuilia hayo.
29 Barki in boo uhenu uganiya wa aka: ca ande sa wa zin ina neh wazi ticukum kas ande sa wa zin we ba.
Lakini ndugu zangu, nina maana kwamba muda uliobaki ni mfupi. Tangu sasa wale waliooa waishi kama wasio na wake;
30 Ana aso wa cukuno kasi anu zatu aso, anu apuru arum kasi anu zatu apuru arum, anu kpija itimumu kasi anu zatu imum.
nao wanaoomboleza, kama ambao hawaombolezi; wenye furaha kama wasiokuwa nayo; wale wanaonunua, kama vile vitu walivyonunua si mali yao;
31 Ande sa wa wuza tanu nan unee kasi ande sa wa ha nan uni ba, barki tamu tu nee ta aye ubinani umara.
nao wale wanaoshughulika na vitu vya dunia hii, kama ambao hawahusiki navyo. Kwa maana dunia hii kama tunavyoiona sasa inapita.
32 In nyara in suri anyimo uba bgardang, unu zatu anyai mazi nu basa abanga Asere, ane ni madi kabi me.
Ningetaka msiwe na masumbufu. Mwanaume ambaye hajaoa anajishughulisha na mambo ya Bwana, jinsi ya kumpendeza Bwana.
33 Una nya ma basa abanga a timumu tunee, aneni madi hem uneh ume.
Lakini mwanaume aliyeoa anajishughulisha na mambo ya dunia, jinsi ya kumfurahisha mkewe,
34 Iriba imeme ya harzina. Uneh unu zatu anya mazinu basa u timumun ti ugomo Asere, ane ani madi inki nice nume in bibe ba Asere. Uneh una nya mazinu basa abanga unee, aneni madi hem unu ruma umeme.
na mawazo yake yamegawanyika. Mwanamke asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana: lengo lake ni awe mtakatifu kimwili na kiroho. Lakini yule aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia, jinsi atakavyoweza kumfurahisha mumewe.
35 In boshi anime barki ubasa ushi uni, azo barki in gbari shi ba. Ma buka ani barki imum besa izi anime, kasi usanda utarsa Asere sa muriba mushi ma harzina ba.
Ninasema haya kwa faida yenu wenyewe, sio ili kuwawekea vizuizi bali mpate kuishi kwa jinsi ilivyo vyema bila kuvutwa pengine katika kujitoa kwenu kwa Bwana.
36 Inka uye ma basa unuguna imum be sa ya kem kubura kumeme - Inka ma aka tiwe ta nya, ani me ya cukuna - ma wuzi imum be sa ma nyara. Azo madini mani mazinu wuza ba. Ca wa wuzi anya.
Kama mtu yeyote anadhani kwamba hamtendei ilivyo sawa mwanamwali ambaye amemposa, naye akiwa umri wake unazidi kuendelea na mtu huyo anajisikia kwamba inampasa kuoa, afanye kama atakavyo. Yeye hatendi dhambi. Yawapasa waoane.
37 Barki anime inka ma tonno ini kara iribe, imeme, inka mada siza me ubusara ba, mada kem ma inta nice numeme memmerun, ma kuri ma tira iriba imeme ma wuzi ani me, ma rusi utarsa in kubura kumeme ya wuna uri.
Lakini mwanaume ambaye ameamua moyoni mwake kutooa bila kulazimishwa na mtu yeyote, bali anaweza kuzitawala tamaa zake kutomwoa huyo mwanamwali, basi anafanya ipasavyo.
38 Barki anime, sede sa ma wuza anya nan kubura kumeme ya wuna uri, me desa ma zauka uwuza anya ma wuza memmerun.
Hivyo basi, mwanaume amwoaye mwanamwali afanya vyema, lakini yeye asiyemwoa afanya vyema zaidi.
39 A tiriza uneh barki uruma, u vat ticukum tumeme. Barki anime inka uruma ma wono, ma da ke ma wuzi anya nan desa sa hem nan me, ca ma wuzi anyimo Asere.
Mwanamke aliyeolewa amefungwa na sheria maadamu mumewe yu hai. Lakini mumewe akifa, basi mwanamke huyo yuko huru kuolewa na mume mwingine ampendaye, lakini lazima awe katika Bwana.
40 U ira um, madi teki ini riba irum. In kuri in basa izin in bibe ba Asere.
Lakini kwa maoni yangu, angekuwa na furaha zaidi akibaki alivyo. Nami nadhani pia nina Roho wa Mungu.