< 1 Ukorontiyawa 10 >
1 Innyara irusa, ni henu, aka coo uru wara ana dizi Uganjimari wa kuri wa tarsa anyumo uraba udandang.
Ndugu zangu, sitaki mkose kufahamu ukweli huu kwamba baba zetu walikuwa wote chini ya wingu na kwamba wote walipita katikati ya bahari.
2 Vat uwe awuza we ubaptisma angumo ama ganjimari nan uraba udandang.
Wote wakabatizwa kuwa wa Mose ndani ya lile wingu na ndani ya ile bahari.
3 Vat uwe waree imum yarce ibibe biririn usandu inde.
Wote walikula chakula kile kile cha roho,
4 Vat uwe wa si imum usa ibibe biririn usandu inde. Barki sa wa si ahira ani poo nibibe biririn sa na tarsi we, nipoo me ninee nini vana Asere.
na wote wakanywa kile kile kinywaji cha roho, kwa maana walikunywa kutoka ule mwamba wa roho uliofuatana nao, nao ule mwamba ulikuwa Kristo.
5 Daki Ugomo Asere maa kunna urunta uma roo mawe ba, mukizi muwe me mu samirka anija.
Lakini Mungu hakupendezwa na wengi wao, kwa hiyo miili yao ilitapakaa jangwani.
6 Ana me timum tigeme imum ubatta ini ahira aruu, kati ti inki timum tibur amuruba kasi wenne ba.
Basi mambo haya yalitokea kama mifano ili kutuzuia tusiweke mioyo yetu katika mambo maovu kama wao walivyofanya.
7 Kati icukuno anu tarsa umakiri kasi āye sa waa wuzi. Kasi unyertike sa āwuzi, “Anu waka vukuno wa ri wa si wa kuri wahirri wawuzi biranza.”
Msiwe waabudu sanamu, kama baadhi yao walivyokuwa, kama ilivyoandikwa, “Watu waliketi chini kula na kunywa, kisha wakainuka kucheza na kufanya sherehe za kipagani.”
8 Kati timussi wana nee naa anu ruma mabura nan inyani sa inzo aru wani ba, kasi maroo mawe me, roni inde anuu a ino ukiran kana kuru are inkani kataru wa wee.
Wala tusifanye uzinzi kama baadhi yao walivyofanya, wakafa watu 23,000 kwa siku moja.
9 Kati timansa vana Asere kasi sa maroo mawe mawuzi, iwa ihuzzi we.
Wala tusimjaribu Kristo, kama baadhi yao walivyofanya, wakafa kwa kuumwa na nyoka.
10 Kati ticukuno anu humoro kasi weme, wa wiji atari tibibe bika dura ka Asere biwono.
Msinungʼunike kama baadhi yao walivyofanya, wakaangamizwa na mharabu.
11 Timum tigeme takem we bati icuunon duru imum ubatta. A nyertike icukuno imum ikubum, haru ande sa umara unee wa aye ace aruu. (aiōn )
Mambo haya yote yaliwapata wao ili yawe mifano kwa wengine, nayo yaliandikwa ili yatuonye sisi ambao mwisho wa nyakati umetufikia. (aiōn )
12 Barki anime, ca komdevi magamari memmerum, ma wuzi merum kati marizi.
Hivyo, yeye ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke.
13 Umansa uda ayeshi, uge sa wamu aye anyumo uvat anuu ba. Anyo, Asere ahuma ani. Madā cekime amansa shi unu mansa sa udi aki nikara nishi ba. Madi nya shi unaa uroo anyumo ubata me sa adi wuzi shi.
Hakuna jaribu lolote lililowapata ambalo si la kawaida kwa wanadamu. Naye Mungu ni mwaminifu; hataruhusu mjaribiwe kupita mnavyoweza. Lakini mnapojaribiwa atawapa njia ya kutokea ili mweze kustahimili.
14 Barki anime shi ande sa mahemshi cekini utarsa umakiri.
Kwa hiyo wapenzi wangu, zikimbieni ibada za sanamu.
15 Inzi tize nan shi kasi anuu bassa ukang, bati I batti imum sa inboo shi.
Nasema watu wenye ufahamu, amueni wenyewe kuhusu haya niyasemayo.
16 Kusso kuringirka kuge sa tizin unu tingirka me, inzo nigome nine anyumo amaye ma vana Asere? Ubiredi me sa tizin upozo me, inzo nigome nine anyume vana Asere?
Je, kikombe cha baraka ambacho tunakibariki, si ushirika katika damu ya Kristo? Mkate tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo?
17 Barki ubiredi u'inde uni, haru gbardan ani pum ni'inde. Vat uruu tidi rii ubiredi u'inde nigome.
Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja, kwa kuwa wote twashiriki mkate mmoja.
18 Irani anuu Isaraila; ida rusa shi ba ana katuma udenge Asere wakenzi imum yaree abinime ani ba?
Waangalieni watu wa Israeli: Je, wale wote walao dhabihu si ni wale watendao kazi madhabahuni?
19 Nyani ni in gusan shi ani me? Makiri imum ini? Nani imumare sa anyinza makiri, ire imum ini?
Je, nina maana kwamba kafara iliyotolewa kwa sanamu ni kitu chenye maana yoyote? Au kwamba sanamu ni kitu chenye maana yoyote?
20 Mi inzin tize atimum sa anu zatu tarse Asere wa ninza, wa ninza agberge ne wani inzo asere ba. Inda nyaram Iwuzi tanu nan agbergene ba.
La hasha! Lakini kafara za watu wasiomjua Mungu hutolewa kwa mashetani, wala si kwa Mungu. Nami sitaki ninyi mwe na ushirika na mashetani.
21 Ida saa shi aku soo ku Ugomo Asere ikuri isii ka gbergene ba, ida ree shi imum yaree Ugomo Asere ikuri iree ya gbergene ba.
Hamwezi kunywa katika kikombe cha Bwana na cha mashetani pia. Hamwezi kuwa na sehemu katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani pia.
22 Nani tinyara tiwu Ugomo Asere ni'eru? Titeki me nikara?
Je, tunataka kuamsha wivu wa Bwana? Je, sisi tuna nguvu kuliko yeye?
23 “Kondi nyani izi rep,” Inzo kondi nyani izin katuma ba, “Kondi nyani izi rep” inzo kondi nyanini I'eze unure aje anu ba.
“Vitu vyote ni halali,” lakini si vitu vyote vilivyo na faida. “Vitu vyote ni halali,” lakini si vyote vinavyojenga.
24 Kati uye ma nyari ubura unicee nume ba, anime manyari ubura uhenu.
Mtu yeyote asitafute yaliyo yake mwenyewe, bali kila mtu atafute yale yanayowafaa wengine.
25 Udake uree vat imum me sa azin unu ziza me ukasuwa, sārki ubasa utize.
Kuleni chochote kinachouzwa sokoni, bila kuuliza swali lolote kwa ajili ya dhamiri.
26 Barki “unee nan vat timum me sa tira anyumo me I Ugomo Asere ini.”
Kwa maana, “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
27 Ingi unu zatu uhem in na Asere ma titawe agi irii imum yaree, ahun ini ruba yaree me uree vat imum me sa anya we sārki uhara Iruba.
Kama ukikaribishwa chakula na mtu asiyeamini nawe ukikubali kwenda, kula kila kitu kitakachowekwa mbele yako bila kuuliza maswali kwa ajili ya dhamiri.
28 Ingi uye magunan hu, “Imum yaree ima kiri mani” kati uree ba. Udi wuu anime barki de sa mabuka we, nan bassa.
Lakini kama mtu yeyote akikuambia, “Hiki kimetolewa kafara kwa sanamu,” basi usikile kwa ajili ya huyo aliyekuambia na kwa ajili ya dhamiri.
29 In boo Ubassa ude sa mabuka we inzo ubassa uwe ba. Barki nyanini adi ziki ucara uye acani mi?
Nina maana dhamiri ya huyo aliyekuambia, wala si kwa ajili ya dhamiri yako. Lakini kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?
30 Ingi ma guna ankoi barki imum yarce sa maree nyanini idi wu azogun barki sa maguna ankoi?
Kama nikila kwa shukrani, kwa nini nashutumiwa kwa kile ambacho kwa hicho ninamshukuru Mungu?
31 Barki anime, ingi uzin naree nan usaa, wuza vat barki unonzo asere.
Basi, lolote mfanyalo, kama ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.
32 Kati ucukuno unaa upilko, wa yanhudawa, nan Aheliniyawa nan anuu Asere ba.
Msiwe kikwazo kwa mtu yeyote, wawe Wayahudi au Wayunani, au kwa kanisa la Mungu,
33 Ma wuza morso bati in rumi vati anuu muruba vat atimun. Inzo barki nicee num ba, barki konderi: Ma wuza anime bati wa kem ubara.
kama hata mimi ninavyojaribu kumpendeza kila mtu kwa kila namna. Kwa maana sitafuti mema kwa ajili yangu mwenyewe bali kwa ajili ya wengi, ili waweze kuokolewa.