< Salmi 49 >

1 Per il Capo de’ musici. De’ figliuoli di Core. Salmo. Udite questo, popoli tutti; porgete orecchio, voi tutti gli abitanti del mondo!
Sikieni hili, ninyi watu wote; tegeni masikio, ninyi wenyeji wa dunia,
2 Plebei e nobili, ricchi e poveri tutti insieme.
wote walio chini na walio juu, tajiri na masikini wote pamoja.
3 La mia bocca proferirà cose savie, e la meditazione del mio cuore sarà piena di senno.
Mdomo wangu utazungumza hekima na tafakari ya moyo wangu itakuwa ya uelewa.
4 Io presterò l’orecchio alle sentenze, spiegherò a suon di cetra il mio enigma.
Nitaelekeza sikio langu kwenye mfano; nitaanza mfano wangu kwa kinubi.
5 Perché temerei ne’ giorni dell’avversità quando mi circonda l’iniquità dei miei insidiatori,
Kwa nini nilazimike kuziogopa siku za uovu, wakati uovu umenizunguka kwenye visigino vyangu?
6 i quali confidano ne’ loro grandi averi e si gloriano della grandezza delle loro ricchezze?
Kwa nini niwaogope wale wanao amini katika mali zao na kujivuna kuhusu utajiri wao?
7 Nessuno però può in alcun modo redimere il fratello, né dare a Dio il prezzo del riscatto d’esso.
Ni hakika kuwa hakuna yeyote atakaye muokoa ndugu yake au kumpa Mungu pesa kwa ajili yake,
8 Il riscatto dell’anima dell’uomo è troppo caro e farà mai sempre difetto.
Kwa maana ukombozi wa uhai wa mtu ni gharama kubwa, na hakuna awezaye kulipa kile tunacho daiwa.
9 Non può farsi ch’ei continui a vivere in perpetuo e non vegga la fossa.
Hakuna yeyote atakaye ishi milele ili mwili wake usioze.
10 Perché la vedrà. I savi muoiono; periscono del pari il pazzo e lo stolto e lasciano ad altri i loro beni.
Maana yeye ataona uozo. Watu wenye hekima hufa; wajinga pia huangamia na kuacha mali zao kwa wengine.
11 L’intimo lor pensiero è che le loro case dureranno in eterno e le loro abitazioni d’età in età; dànno i loro nomi alle loro terre.
Mawazo yao ya ndani ni kuwa familia zao zitaishi milele, na mahali waishipo, kwa vizazi vyote; wanaita ardhi zao kwa majina yao wenyewe.
12 Ma l’uomo ch’è in onore non dura; egli è simile alle bestie che periscono.
Lakini mtu, kuwa na mali, haimaanishi atabaki hai; kama wanyama walioangamia.
13 Questa loro condotta è una follia; eppure i loro successori approvano i lor detti. (Sela)
Hii ni hatma ya wafanyao ujinga baada ya kufa, .................
14 Son cacciati come pecore nel soggiorno de’ morti; la morte è il loro pastore; ed al mattino gli uomini retti li calpestano. La lor gloria ha da consumarsi nel soggiorno de’ morti, né avrà altra dimora. (Sheol h7585)
Kama kondoo wamechaguliwa kwa ajili ya kuzimu na kifo kitakuwa mchungaji wao. Nao watatawaliwa na wenye haki ifikapo asubuhi, na miili yao italiwa kuzimuni, wakiwa hawana afasi ya kuishi kwa ajili yao. (Sheol h7585)
15 Ma Iddio riscatterà l’anima mia dal potere del soggiorno dei morti, perché mi prenderà con sé. (Sela) (Sheol h7585)
Bali Mungu ataufufua uhai wangu kutoka katika nguvu ya kuzimu; naye atanipokea. (Selah) (Sheol h7585)
16 Non temere quand’uno s’arricchisce, quando si accresce la gloria della sua casa.
Msifadhaike mtu awapo tajiri, utukufu wa nyumba yake uongezekapo.
17 Perché, quando morrà, non porterà seco nulla; la sua gloria non scenderà dietro a lui.
Maana atakapo kufa hataondoka na chochote; utukufu wake hautamfuata yeye.
18 Benché tu, mentre vivi, ti reputi felice, e la gente ti lodi per i godimenti che ti procuri,
Yeye huifurahisha nafsi yake awapo hai na watu hukusifu wewe uishipo maisha yako mwenyewe-
19 tu te ne andrai alla generazione de’ tuoi padri, che non vedranno mai più la luce.
naye atakwenda kwenye ukoo wa baba zake naye kamwe hataiona nuru tena.
20 L’uomo ch’è in onore e non ha intendimento è simile alle bestie che periscono.
Yule ambaye ana mali lakini hana ufahamu ni kama wanyama, ambao wataangamia.

< Salmi 49 >