< Salmi 30 >
1 Salmo. Cantico per la dedicazione della Casa. Di Davide. Io t’esalto, o Eterno, perché m’hai tratto in alto, e non hai permesso che i miei nemici si rallegrassero di me.
Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
2 O Eterno, Dio mio, io ho gridato a te, e tu m’hai sanato.
Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
3 O Eterno, tu hai fatto risalir l’anima mia dal soggiorno de’ morti, tu m’hai ridato la vita perch’io non scendessi nella fossa. (Sheol )
Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol )
4 Salmeggiate all’Eterno, voi suoi fedeli, e celebrate la memoria della sua santità.
Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
5 Poiché l’ira sua è sol per un momento, ma la sua benevolenza e per tutta una vita. La sera alberga da noi il pianto; ma la mattina viene il giubilo.
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
6 Quanto a me, nella mia prosperità, dicevo: Non sarò mai smosso.
Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
7 O Eterno, per il tuo favore, avevi reso forte il mio monte; tu nascondesti la tua faccia, ed io fui smarrito.
Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
8 Io ho gridato a te, o Eterno; ho supplicato l’Eterno, dicendo:
Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
9 Che profitto avrai dal mio sangue s’io scendo nella fossa? Forse che la polvere ti celebrerà? predicherà essa la tua verità?
“Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
10 Ascolta, o Eterno, ed abbi pietà di me; o Eterno, sii tu il mio aiuto!
Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
11 Tu hai mutato il mio duolo in danza; hai sciolto il mio cilicio a m’hai cinto d’allegrezza,
Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
12 affinché l’anima mia salmeggi a te e non si taccia. O Eterno, Dio mio, io ti celebrerò in perpetuo.
ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.