< Salmi 23 >

1 Salmo di Davide. L’Eterno è il mio pastore, nulla mi mancherà.
Zaburi ya Daudi. Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.
2 Egli mi fa giacere in verdeggianti paschi, mi guida lungo le acque chete.
Hunilaza katika malisho ya majani mabichi, kando ya maji matulivu huniongoza,
3 Egli mi ristora l’anima, mi conduce per sentieri di giustizia, per amor del suo nome.
hunihuisha nafsi yangu. Huniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
4 Quand’anche camminassi nella valle dell’ombra della morte, io non temerei male alcuno, perché tu sei meco; il tuo bastone e la tua verga son quelli che mi consolano.
Hata kama nikipita katikati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya, kwa maana wewe upo pamoja nami; fimbo yako na mkongojo wako vyanifariji.
5 Tu apparecchi davanti a me la mensa al cospetto dei miei nemici; tu ungi il mio capo con olio; la mia coppa trabocca.
Waandaa meza mbele yangu machoni pa adui zangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, kikombe changu kinafurika.
6 Certo, beni e benignità m’accompagneranno tutti i giorni della mia vita; ed io abiterò nella casa dell’Eterno per lunghi giorni.
Hakika wema na upendo vitanifuata siku zote za maisha yangu, nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.

< Salmi 23 >