< Proverbi 29 >
1 L’uomo che, essendo spesso ripreso, irrigidisce il collo, sarà di subito fiaccato, senza rimedio.
Mtu aliyepokea makaripio mengi lakini anashupaza shingo yake atavunjika ndani ya muda mfupi na hata pona.
2 Quando i giusti son numerosi, il popolo si rallegra: ma quando domina l’empio, il popolo geme.
Watenda mema wanapoongezeka, watu wanafurahi, bali wakati mtu mwovu anapotawala, watu huugua.
3 L’uomo che ama la sapienza, rallegra suo padre; ma chi frequenta le meretrici dissipa i suoi beni.
Mwenye kupenda hekima baba yake anafurahi, bali anayeshikamana na makahaba huuharibu utajiri wake.
4 Il re, con la giustizia, rende stabile il paese; ma chi pensa solo a imporre tasse, lo rovina.
Mfalme huimarisha nchi kwa haki, bali mwenye kudai rushwa huirarua.
5 L’uomo che lusinga il prossimo, gli tende una rete davanti ai piedi.
Mtu anayejipendekeza kwa jirani yake anatandaza wavu kwenye miguu yake.
6 Nella trasgressione del malvagio v’è un’insidia; ma il giusto canta e si rallegra.
Mtu mbaya hunaswa kwenye mtego wa dhambi yake mwenyewe, bali yeye atendaye haki huimba na kufurahi.
7 Il giusto prende conoscenza della causa de’ miseri, ma l’empio non ha intendimento né conoscenza.
Atendaye haki hutetea madai ya masikini; mtu mwovu hafahamu maarifa kama hayo.
8 I beffardi soffian nel fuoco delle discordie cittadine, ma i savi calmano le ire.
Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
9 Se un savio viene a contesa con uno stolto, quello va in collera e ride, e non c’è da intendersi.
Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
10 Gli uomini di sangue odiano chi è integro, ma gli uomini retti ne proteggono la vita.
Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
11 Lo stolto dà sfogo a tutta la sua ira, ma il savio rattiene la propria.
Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
12 Quando il sovrano dà retta alle parole menzognere, tutti i suoi ministri sono empi.
Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
13 Il povero e l’oppressore s’incontrano; l’Eterno illumina gli occhi d’ambedue.
Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
14 Il re che fa ragione ai miseri secondo verità, avrà il trono stabilito in perpetuo.
Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
15 La verga e la riprensione dànno sapienza; ma il fanciullo lasciato a sé stesso, fa vergogna a sua madre.
Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
16 Quando abbondano gli empi, abbondano le trasgressioni; ma i giusti ne vedranno la ruina.
Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
17 Correggi il tuo figliuolo; egli ti darà conforto, e procurerà delizie all’anima tua.
Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
18 Quando non c’è visioni, il popolo è senza freno; ma beato colui che osserva la legge!
Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
19 Uno schiavo non si corregge a parole; anche se comprende, non ubbidisce.
Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
20 Hai tu visto un uomo precipitoso nel suo parlare? C’è più da sperare da uno stolto che da lui.
Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
21 Se uno alleva delicatamente da fanciullo il suo servo, questo finirà per voler essere figliuolo.
Mwenye kumdekeza mtumwa wake tangu ujana, mwisho wake itakuwa taabu.
22 L’uomo iracondo fa nascere contese, e l’uomo collerico abbonda in trasgressioni.
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi na bwana mwenye hasira sana hutenda dhambi nyingi.
23 L’orgoglio abbassa l’uomo, ma chi è umile di spirito ottiene gloria.
Kiburi cha mtu humshusha chini, bali mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima.
24 Chi fa società col ladro odia l’anima sua; egli ode la esecrazione e non dice nulla.
Anayeshirikiana na mwizi huyachukia maisha yake mwenyewe; husikia laana na wala hasemi chochote.
25 La paura degli uomini costituisce un laccio, ma chi confida nell’Eterno è al sicuro.
Kumwogopa binadamu ni mtego, bali mwenye kumtumaini Yehova atalindwa.
26 Molti cercano il favore del principe, ma l’Eterno fa giustizia ad ognuno.
Wengi huutafuta uso wa mtawala, bali kutoka kwa Yehova huja haki kwa ajili yake.
27 L’uomo iniquo è un abominio per i giusti, e colui che cammina rettamente è un abominio per gli empi.
Mtu dhalimu ni chukizo kwa wenye kutenda haki, bali mwenye njia ya haki ni chukizo kwa watu waovu.