< Giobbe 40 >
1 L’Eterno continuò a rispondere a Giobbe e disse:
Bwana akamwambia Ayubu:
2 “Il censore dell’Onnipotente vuole ancora contendere con lui? Colui che censura Iddio ha egli una risposta a tutto questo?”
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Allora Giobbe rispose all’Eterno e disse:
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 “Ecco, io son troppo meschino; che ti risponderei? Io mi metto la mano sulla bocca.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 Ho parlato una volta, ma non riprenderò la parola, due volte… ma non lo farò più”.
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 L’Eterno allora rispose a Giobbe dal seno della tempesta, e disse:
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 “Orsù, cingiti i lombi come un prode; ti farò delle domande e tu insegnami!
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 Vuoi tu proprio annullare il mio giudizio? condannar me per giustificar te stesso?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 Hai tu un braccio pari a quello di Dio? o una voce che tuoni come la sua?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Su via, adornati di maestà, di grandezza, rivestiti di splendore, di magnificenza!
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Da’ libero corso ai furori dell’ira tua; mira tutti i superbi e abbassali!
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Mira tutti i superbi e umiliali! e schiaccia gli empi dovunque stanno!
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Seppelliscili tutti assieme nella polvere, copri di bende la lor faccia nel buio della tomba!
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 Allora, anch’io ti loderò, perché la tua destra t’avrà dato la vittoria.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Guarda l’ippopotamo che ho fatto al par di te; esso mangia l’erba come il bove.
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 Ecco la sua forza è nei suoi lombi, e il vigor suo nei muscoli del ventre.
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 Stende rigida come un cedro la coda; i nervi delle sue cosce sono intrecciati insieme.
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 Le sue ossa sono tubi di rame; le sue membra, sbarre di ferro.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 Esso è il capolavoro di Dio; colui che lo fece l’ha fornito di falce,
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 perché i monti gli producon la pastura; e là tutte le bestie de’ campi gli scherzano intorno.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 Si giace sotto i loti, nel folto de’ canneti, in mezzo alle paludi.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 I loti lo copron dell’ombra loro, i salci del torrente lo circondano.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 Straripi pure il fiume, ei non trema; rimane calmo, anche se avesse un Giordano alla gola.
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 Potrebbe alcuno impadronirsene assalendolo di fronte? o prenderlo colle reti per forargli il naso?
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?